Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania latoa Waraka wa Kwaresma, lazungumzia upatanisho

Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania latoa Waraka wa Kwaresma, lazungumzia upatanisho

Inside10

JF-Expert Member
Joined
May 20, 2011
Posts
29,909
Reaction score
32,414
a0a3877f3c79eabb443c94ad4eff7cf2

Rais wa TEC, Askofu Mkuu, Gervas Nyaisonga

BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limetoa waraka wa Kwaresima wa mwaka 2022 ambao kwa sehemu kubwa umejikita kuzungumzia umuhimu wa upatanisho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Waraka huo wenye kurasa 44, umetolewa na maaskofu hao katoliki 35 ikiwa leo ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresima ‘Jumatano ya Majivu’ tarehe 2 Machi 2022.

Waraka huo, umebeba ujumbe unaosema “Tunawasihi kwa jina lake Kristo, Mpatanishwe na Mungu” (2 Kor 5:20).
Katika sura hii, Mtume Paulo ametoa maelezo mbalimbali kumhusu Kristo na mwishoni anahitimisha na kumsihi kila mmoja ajitahidi kupatanishwa na Mungu.

Mwaliko huu ni kiashirio kwamba, maisha ya mkristo lazima yaambatane na jitihada ya kutaka kupatanishwa na Baba wa mbinguni kwa sababu baada ya maisha haya tutarudi kwake.
“Mafundisho yote yanayohusu upatanisho ni kipengele muhimu katika mpango wa Mungu wa wokovu. Upatanisho ni neno ambalo mwanadamu hukutana nalo mara nyingi asomapo Maandiko Matakatifu na ndani ya jamii anamoishi. Upatanisho ni sehemu ya wokovu wetu; unakuza mahusiano yetu na Mungu na pia kati yetu,” unaeleza waraka huo

Kisiasa, maaskofu hao wakiongozwa na Gervas Nyaisonga, Askofu Mkuu ambaye pia ni Rais wa Baraza hilo wanasema, upatanisho husaidia watu kuwa huru, kuwajibika, kwa kutetea haki zao na za wengine; kushiriki katika ujenzi wa Taifa kwa umoja, juhudi na maarifa; na kujenga demokrasia kwa kushiriki katika chaguzi zilizo huru na za haki.
Wanasema, mchakato wa upatanisho husaidia watu kuishi kwa umoja na amani. Lakini uovu hauwezi kuisha maadamu tunaishi katika ulimwengu huu uliogubikwa mafarakano; na upatanisho wa kweli ni tumaini la binadamu yeyote anayemwogopa Mungu.

Dunia inahitaji kwanza kupatanishwa na Mungu na kisha upatanisho ndani ya jamii. Pasiwepo watu ambao maisha yao yote ni ya manung’uniko sababu tu njia za upatanisho zimefungwa na upande wa pili. Sote tunaalikwa ndani ya jamii ya kitanzania kulitazama na kulifanyia kazi hilo katika ukweli na uadilifu.
“Kisiasa, ‘upatanisho’ wa kweli hupatikana katika kuitafuta, kuiishi na kuilinda demokrasia na amani dumifu,” unaeleza waraka huo na kuongeza:

“Ili kufikia demokrasia ya kweli kama njia ya kuelekea mapatano ya kweli, bado yanahitajika majadiliano kati ya wadau mbalimbali wa kisiasa na hasa katika vikao muhimu vya kutoa uamuzi.”

“Hivyo basi, viongozi wetu hawana budi kubadilika kuona kwamba demokrasia na utawala bora vinashika hatamu kwa ajili ya manufaa ya wengi.”
718d7f291a0e1849bf249a1ba53e06a9

Baadhi ya maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania
Maaskofu hao wanasema, “wakati huu wa Kwaresima, kila mmoja katika Taifa la Mungu anahimizwa kutekeleza wajibu wake, kwa njia ya toba, kujenga na kudumisha moyo wa mapatano na uelewano katika jamii.”

“Huu ni mwaliko wa kuondokana na ubaguzi wa aina yoyote ile, hususan ubaguzi wa kisiasa. Wakristo hawana budi kuwa ni wadau wa amani ili kudumisha mapatano ya kweli. Haya yote yatawezekana iwapo tu haki, amani, ukweli na uwazi vitatamalaki,” wamesisitiza

Waraka huo unahitimishwa ukisema, “ujumbe huu wa Kwaresima kwetu ni mahususi kwa ajili ya ujenzi wa jamii mpya yenye nia ya kuishi kwa umoja na amani kama asemavyo Mzaburi “Tazama, jinsi ilivyo vyema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja kwa umoja” (Zab 133:1).
“Kukaa huku pamoja haimaanishi kwamba ni kukaa bila tofauti za kimawazo na kimtazamo. La hasha. Bali ni kule kukaa kwa kukubali tofauti hizo bila ya kufarakana,” wanasema

Maaskofu hao wanasema, yumewaandikia ujumbe huu wa Kwaresima kwa Mwaka 2022: “Tunawasihi kwa jina lake Kristo, mpatanishwe na Mungu” (2 Kor 5:20), tukitambua kwamba hapa na pale jamii zetu zinafarakana kwa mawazo, kwa maneno, kwa matendo, na kimtazamo.
“Ndiyo maana tumesisitiza na tunasisitiza kwamba hayo yanapotokea tunahitaji kupatanishwa. Lengo kuu la upatanisho si kuonekana kwamba mmoja ameshindwa bali ni “kuanza maisha mapya; maisha ya neema.”
 
Demokrasia kote duniani ikiachwa ifuate mkondo wake hapatakuwepo na chuki na hasira, haki za kila raia zikiheshimiwa kwenye mfumo bora wa sheria hapatakuwepo na unyanyasaji na uonevu.

Malalamiko yote yanayotokea yanasababishwa na watawala kujisahau na kujiona wao ndio wenye hati miliki ya kila kitu, hali hii ndio husababisha kundi fulani la watu wajione wanaonewa ndani ya nchi yao na kusababisha pawepo na sintofahamu miongoni mwa vyama pinzani na chama tawala.
 
Demokrasia kote duniani ikiachwa ifuate mkondo wake hapatakuwepo na chuki na hasira, haki za kila raia zikiheshimiwa kwenye mfumo bora wa sheria hapatakuwepo na unyanyasaji na uonevu.

Malalamiko yote yanayotokea yanasababishwa na watawala kujisahau na kujiona wao ndio wenye hati miliki ya kila kitu, hali hii ndio husababisha kundi fulani la watu wajione wanaonewa ndani ya nchi yao na kusababisha pawepo na sintofahamu miongoni mwa vyama pinzani na chama tawala.
wanakula jaramba
 
Maaskofu tuliowqpa ruhusa kuzungumza katika zama hizi ni Askofu Shoo, Mwamakula na Bagonza tu... wengine wanyamaze kama walivyofanya kwa jiwe.
 
Maaskofu tuliowqpa ruhusa kuzungumza katika zama hizi ni Askofu Shoo, Mwamakula na Bagonza tu... wengine wanyamaze kama walivyofanya kwa jiwe.
Uliowapa ruhusa wewe na nani?

Chadema imefuga watu wa ajabu sana

I am sure hata viongozi wanajuta kuwa na baadhi ya fanatics kama wewe
 
Maaskofu tuliowqpa ruhusa kuzungumza katika zama hizi ni Askofu Shoo, Mwamakula na Bagonza tu... wengine wanyamaze kama walivyofanya kwa jiwe.
Unajua NIWEMUGIZI..?
 
a0a3877f3c79eabb443c94ad4eff7cf2

Rais wa TEC, Askofu Mkuu, Gervas Nyaisonga

BARAZA la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), limetoa waraka wa Kwaresima wa mwaka 2022 ambao kwa sehemu kubwa umejikita kuzungumzia umuhimu wa upatanisho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Waraka huo wenye kurasa 44, umetolewa na maaskofu hao katoliki 35 ikiwa leo ni mwanzo wa kipindi cha Kwaresima ‘Jumatano ya Majivu’ tarehe 2 Machi 2022.

Waraka huo, umebeba ujumbe unaosema “Tunawasihi kwa jina lake Kristo, Mpatanishwe na Mungu” (2 Kor 5:20).
Katika sura hii, Mtume Paulo ametoa maelezo mbalimbali kumhusu Kristo na mwishoni anahitimisha na kumsihi kila mmoja ajitahidi kupatanishwa na Mungu.

Mwaliko huu ni kiashirio kwamba, maisha ya mkristo lazima yaambatane na jitihada ya kutaka kupatanishwa na Baba wa mbinguni kwa sababu baada ya maisha haya tutarudi kwake.


Kisiasa, maaskofu hao wakiongozwa na Gervas Nyaisonga, Askofu Mkuu ambaye pia ni Rais wa Baraza hilo wanasema, upatanisho husaidia watu kuwa huru, kuwajibika, kwa kutetea haki zao na za wengine; kushiriki katika ujenzi wa Taifa kwa umoja, juhudi na maarifa; na kujenga demokrasia kwa kushiriki katika chaguzi zilizo huru na za haki.
Wanasema, mchakato wa upatanisho husaidia watu kuishi kwa umoja na amani. Lakini uovu hauwezi kuisha maadamu tunaishi katika ulimwengu huu uliogubikwa mafarakano; na upatanisho wa kweli ni tumaini la binadamu yeyote anayemwogopa Mungu.

Dunia inahitaji kwanza kupatanishwa na Mungu na kisha upatanisho ndani ya jamii. Pasiwepo watu ambao maisha yao yote ni ya manung’uniko sababu tu njia za upatanisho zimefungwa na upande wa pili. Sote tunaalikwa ndani ya jamii ya kitanzania kulitazama na kulifanyia kazi hilo katika ukweli na uadilifu.
“Kisiasa, ‘upatanisho’ wa kweli hupatikana katika kuitafuta, kuiishi na kuilinda demokrasia na amani dumifu,” unaeleza waraka huo na kuongeza:

“Ili kufikia demokrasia ya kweli kama njia ya kuelekea mapatano ya kweli, bado yanahitajika majadiliano kati ya wadau mbalimbali wa kisiasa na hasa katika vikao muhimu vya kutoa uamuzi.”

“Hivyo basi, viongozi wetu hawana budi kubadilika kuona kwamba demokrasia na utawala bora vinashika hatamu kwa ajili ya manufaa ya wengi.”
718d7f291a0e1849bf249a1ba53e06a9

Baadhi ya maaskofu wa Kanisa Katoliki Tanzania
Maaskofu hao wanasema, “wakati huu wa Kwaresima, kila mmoja katika Taifa la Mungu anahimizwa kutekeleza wajibu wake, kwa njia ya toba, kujenga na kudumisha moyo wa mapatano na uelewano katika jamii.”

“Huu ni mwaliko wa kuondokana na ubaguzi wa aina yoyote ile, hususan ubaguzi wa kisiasa. Wakristo hawana budi kuwa ni wadau wa amani ili kudumisha mapatano ya kweli. Haya yote yatawezekana iwapo tu haki, amani, ukweli na uwazi vitatamalaki,” wamesisitiza

Waraka huo unahitimishwa ukisema, “ujumbe huu wa Kwaresima kwetu ni mahususi kwa ajili ya ujenzi wa jamii mpya yenye nia ya kuishi kwa umoja na amani kama asemavyo Mzaburi “Tazama, jinsi ilivyo vyema, na kupendeza, ndugu wakae pamoja kwa umoja” (Zab 133:1).
“Kukaa huku pamoja haimaanishi kwamba ni kukaa bila tofauti za kimawazo na kimtazamo. La hasha. Bali ni kule kukaa kwa kukubali tofauti hizo bila ya kufarakana,” wanasema

Maaskofu hao wanasema, yumewaandikia ujumbe huu wa Kwaresima kwa Mwaka 2022: “Tunawasihi kwa jina lake Kristo, mpatanishwe na Mungu” (2 Kor 5:20), tukitambua kwamba hapa na pale jamii zetu zinafarakana kwa mawazo, kwa maneno, kwa matendo, na kimtazamo.
“Ndiyo maana tumesisitiza na tunasisitiza kwamba hayo yanapotokea tunahitaji kupatanishwa. Lengo kuu la upatanisho si kuonekana kwamba mmoja ameshindwa bali ni “kuanza maisha mapya; maisha ya neema.”
Ahh remote .
Bado uko hai? Dah....
 
Back
Top Bottom