Kuna pull factors na push factors!
Yaani mazingira mabovu ya ndani yanayosababisha wanachama kukikimbia chama, na mazingira mazuri ya chama kingine yanayowavuta wanachama.
Kosa kubwa la CHADEMA ni kuruhusu mtu moja mwenye upeo mdogo wa maono na utambuzi ila mjanjamjanja aliyebebwa na historia atengeneze mtandao wa kumtumikia yeye binafsi badala ya chama. Hivyo kulea uovu wa udikteta, ubadhirifu, udhalilishaji wa kijinsia, kujipendekeza, nepotism, usanii na siasa za maigizo, makundi na madaraja.
Kwangu mimi ubovu wa ndani ya CHADEMA ndiyo chanzo na sababu kubwa ya wanachama na viongozi wengi kuhama CHADEMA.
Natambua mabadiliko makubwa yanayofanywa na serikali ya CCM chini ya kiongozi wa aina yake na mwenye kuleta mabadiliko makubwa, JPM. Hivyo sishangai viongozi wa vyama vingine wanapochoshwa na usanii wa ndani ya vyama vyao na kuamua kujiunga na CCM!