Baraza la sanaa(BASATA) lasitisha usajili wa Msanii Dudubaya

Mama Amon uko vizuri
 
umesomeka tatizo lipo kwenye hii enzi ya 5 sheria kwao ni takataka ila matamko yao ndio shelia
 
We
Wewe Na elimu yako ya darasa la 6
 
Kwa kosa lipi kisheria?.Kisheria Dudubaya hana kosa,ila kimaadili kweli alikosea.
Unajua vifungu vyote vya sheria mkuu???Kosa linaweza likaonekana tu kwa mujibu huo huo wa sheria...Dudu baya wakiamua kufukua makaburi amefanya makosa mengi sana ya kimtandao labda wasitake tu kumshughulikia...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
National Arts Council - BASATA.
Nimependa line na paragraph spacing.... katika hii barua!
 
Basata wanazingua tu. Kama wangekuwa serious na kazi sidhani kama huu mziki wa kusifia ngono na wanawake ungekuwepo maredioni mpaka sasahivi. Asiyeweza kuimba vitu vyenye mantiki na kuburudisha aache usanii nchini.

Sahivi tuna kizazi cha ajabu kupata kutokea katika sanaa ya mziki ikiwa sie tulipokea mziki kutoka kwa akina Msondo, DDC, TOT na wengineo ukaja kwa akina Rip Banza, Mwinjuma muumini Ally Choki ukiwa salama kabisa . Angalia kina Feruzi, Prof. Jay, Afande Sele, Juma Nature wote waliendeleza burudani huku wakiimba vitu vinavyogusa jamii na maisha kwa ujumla.

Sahizi ni upumbavu wa kusifia ngono kwa mafumbo tu, paka mate niteleze. Blah blah kibao. Kwanza mziki hauna vionjo asilia vya kibongo umekaa ki Nigeria sana makelele mengi. Hamna ujumbe mwishowe tunakuza vizazi vya malaya na mashoga tua sasahivi. 80% ya nyimbo inazungumzia nipe vya chumbani...aargh.

Kama nyie BASATA kweli kazi mnaiweza ondoeni upupu unaozagaa maredioni na kwenye TV. Bring back the 1998-2007 bongo flava back. Wekeni katiba inayolinda na kusimamia haki za msanii na mtayarishaji nyimbo. Inasikitisha sana wasio na vipaji leo wanatajirika tu ilihali waasisi wa bongo flava wapo na wanakufa na unga kwa kukoseshwa Airtime. Eti ni wasanii wa zamani...so Ridiculous. Fanyeni vitu vionekane kweli, sio kujihusisha na kesi za kitoto!
 
Hapa ndio unapojua uelewa wa watanzania wengi ulivyo chini basata wanafanya kazi kwa maagizo badala ya kufata Sheria mwakyembe anasahau alipovurunda kwenye ripoti ya Richmond kwa kuficha ukweli na kuingiza siasa kwenye Sheria kwani Nani hajui beef za marehemu na wasanii mbalimbali kuanzia swala la studio ya serikali, lady jaydee na mradi wa malaria bila kusahau ugomvi na diamond pamoja na makonda
 
Na huko Mahakamani atanyimwa dhamana kwa maelekezo kutoka Juu,kwamba ndugu jamaa na marafiki wamejawa na hasira na hivyo anyimwe dhamana kwa ajili ya usalama wake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…