Pre GE2025 Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) wajutia tuzo waliyompatia Rais Samia mwaka 2023

Pre GE2025 Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) wajutia tuzo waliyompatia Rais Samia mwaka 2023

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Chachu Ombara

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2012
Posts
6,067
Reaction score
10,938
"Leo (Jumatatu, Septemba 30.2024) Bawacha tumewaita (wanahabari) hapa (makao makuu ya zamani ya CHADEMA) kufanya tukio la kuonyesha hasira zetu dhidi ya Rais (Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania), mwaka jana tarehe 3/8/2023 BAWACHA tulimualika kwenye kongamano la siku ya mwanamke Duniani, kwa upendo kabisa tukitegemea mabadiliko chanya kwenye Taifa letu, tulimpa changamoto tisa za wanawake na Watanzania kama vile uboresha huduma za afya hususani kwa kina mama na watoto, kupunguza kodi na tozo kwa wafanyabiashara wadogo ambao wengi wao ni wanawake na vijana, kupunguza gharama za maisha, kupunguza tatizo la ajira kwa vijana wetu, na kurejesha mchakato wa Katiba mpya" -BAWACHA

"Changamo nyingine ni pamoja na kutatua kero ya maji hasa maeneo ya vijijini maana waathirika wakubwa ni kinana, kuwaondoa 'COVID 19' (Wabunge 19 wa Viti maalum walioko Bungeni wakiongozwa na Mwenyekiti wa zamani wa BAWACHA Halima Mdee ambao wanatajwa kuwa hapo kwa baraka za CHADEMA) Bungeni, kuboresha mfumo wa elimu kwa watoto wetu, kurejea sheria kandamizi kwa wanawake na watoto hasa sheria ya ndoa, katika kongamano hilo tulimpa zawadi ya tuzo ya demokrasia na maridhiano na yeye akatupa zawadi ya vitenge" -BAWACHA

"Hata hivyo hakuna jambo hata moja ambalo Rais Samia amelifanyia kazi, hii ni dharau kwa BAWACHA na dharau kwa wanawake wapenda haki na maendeleo ya Taifa lao, hivyo basi leo tumewaita hapa ili kuonyesha hasira zetu dhidi ya Rais Samia kwa kukokuchukua hatua yoyote dhidi ya mauaji, utekaji na kupotea kwa vijana wetu, BAWACHA Kanda ya Pwani leo tutaenda kuchoma vitenge alivyotupa Rais kama zawadi siku ya mwanamke Duniani mwaka jana" -BAWACHA

Ni sehemu ya yale aliyozungumza Mwenezi wa BAWACHA Taifa Aisha Machano mbele ya wanahabari leo, Jumatatu Septemba 30.2024

Pia soma
- BAWACHA watangaza kuchoma vitenge walivyopewa kama zawadi na Rais Samia mwaka jana
 
Safi
BAWACHA ukiwakeka na UWT unaona kabisa jinsi walivyo mahiri kwenye hojana malengo changa kwa Taifa

UWT ni mipasho na kichaka cha madaraka bila malengo
 
Humanity should be glad the World is ruled by men.
 
..kama Bawacha wanamuita Mama Abduli MUUAJI basi aitupe jalalani tuzo waliyompa.
 
Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) limetoa kauli ya masikitiko kwa Rais Samia Suluhu Hassan, likidai kuwa ahadi walizowasilisha mwaka jana hazijatekelezwa.

Katika mkutano na wanahabari leo, BAWACHA ilisema kuwa mwaka jana walimwalika Rais Samia kwenye kongamano la Siku ya Mwanamke Duniani na kumpa changamoto tisa za wanawake na Watanzania, ikiwemo kuboresha huduma za afya na kupunguza kodi kwa wafanyabiashara wadogo.

Pamoja na kumpa tuzo ya demokrasia na maridhiano, BAWACHA sasa inajutia hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na ukosefu wa mabadiliko.

Soma pia: BAWACHA watangaza kuchoma vitenge walivyopewa kama zawadi na Rais Samia mwaka jana

"Kwa upendo kabisa, tulimpa tuzo hiyo tukitegemea mabadiliko chanya kwenye taifa letu, lakini hadi leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa," alisema Mwenezi wa BAWACHA, Aisha Machano.

Machano alieleza kuwa changamoto nyingine kama utatuzi wa tatizo la maji na tatizo la ajira kwa vijana hazijashughulikiwa, hali iliyopelekea BAWACHA kujutia tuzo waliyoitoa kwa Rais.

Source: Jambo TV
 
Shida ni kwamba hawa wanawake waliendeshwa kimhemko mhemko yaan kiufupi walikurupuka bila kujua ccm ni ile ile ni mfumo na sio mtu badala wapambane na ccm wanapambana na rais 🤣🤣🤣
 
Baraza la Wanawake wa CHADEMA (BAWACHA) limetoa kauli ya masikitiko kwa Rais Samia Suluhu Hassan, likidai kuwa ahadi walizowasilisha mwaka jana hazijatekelezwa.

Katika mkutano na wanahabari leo, BAWACHA ilisema kuwa mwaka jana walimwalika Rais Samia kwenye kongamano la Siku ya Mwanamke Duniani na kumpa changamoto tisa za wanawake na Watanzania, ikiwemo kuboresha huduma za afya na kupunguza kodi kwa wafanyabiashara wadogo.

Pamoja na kumpa tuzo ya demokrasia na maridhiano, BAWACHA sasa inajutia hatua hiyo baada ya kutoridhishwa na ukosefu wa mabadiliko.

Soma pia: BAWACHA watangaza kuchoma vitenge walivyopewa kama zawadi na Rais Samia mwaka jana

"Kwa upendo kabisa, tulimpa tuzo hiyo tukitegemea mabadiliko chanya kwenye taifa letu, lakini hadi leo hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa," alisema Mwenezi wa BAWACHA, Aisha Machano.

Machano alieleza kuwa changamoto nyingine kama utatuzi wa tatizo la maji na tatizo la ajira kwa vijana hazijashughulikiwa, hali iliyopelekea BAWACHA kujutia tuzo waliyoitoa kwa Rais.

Source: Jambo TV
Kawaida ya tuzo hutolewa baada ya kazi kufanyika,nyinyi BAWACHA ilikuwaje mkatoa tuzo kabla ya kazi kufanyika kama si rushwa!!??
 
Leo nimeona BAWACHA wakichoma khanga ambazo walipewa na Raisi Samia.

Ombi langu Dkt Samia usitupe wala kuharibu tuzo waliyokupa BAWACHA kwakua katika kitabu chako cha historia utapiga picha na kuweka katika maandishi na pia pale watakapoanza kukumbuka kwa mema na kusema tulimpa tuzo kwahyo raisi usivunjike moyo.
 
Back
Top Bottom