Barbara Gonzalez na Wallace Karia watangazwa kuwa Wajumbe wa Kamati za CAF

Barbara Gonzalez na Wallace Karia watangazwa kuwa Wajumbe wa Kamati za CAF

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
1663750870848.png

Mkurugenzi Mtendaji wa Simba SC, Barbara Gonzalez ametangazwa kuwa Mjumbe wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Vilabu vya CAF na Usimamizi wa Mfumo wa Leseni za Klabu

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia ameteuliwa kuwa mjumbe kwenye Kamati mbili.

Kamati hizo ni ya Maandalizi ya Fainali za Mataifa ya Afrika (AFCON) pamoja na Kamati ya Fedha.

Makamu wa Kwanza wa Rais wa TFF, Athumani Nyamlani ameteuliwa kwenye Kamati ya Soka la Ufukweni (Beach Soccer).

Mjumbe katika Kamati ya Mpira wa Miguu wa Wanawake ya CAF kutoka Tanzania ni Katibu Mtendaji wa Baraza la Michezo la Taifa (BMT), Neema Msitha.
 
Kamati ya maandalizi ya mashindano ya vilabu, mbona haieleweki maana mashindano ya Caf Kwa ngazi ya vilabu ndio Yanaendelea kwasasa Sasa yeye kateuliwa aandae kitu gani, Mfumo wa Leseni kama Club licensing wenyewe ulisha tolewa muongozo tangu Zamani ni jukumu la FA za nchi mbalimbali kusimamia zoezi jinsi linavyo kwenda.
Isije ikawa mtu kampa Chaka lisilo na mashiko Ili aka funue miwani yake!!!
Ebu mleta Mada fafanua tuelewe majukumu yake hasa Yana husu mashindano gani? Caf champion league and confederation cup, Caf club women's champion league,New Elite Caf champion league?
 
Kwa ujumla kinacho onekana Rais wa CAF ndugu Motsepe kashapewa udhaifu wote wa CEO na mshkaji wake Senzo, Kwakua wamegundua CEO anapenda Publicity (Umaarufu) wakaona waanze na Chambo kikubwa.
Kinachofuatia ni kumtakia majukumu mema, ila nampa Big up Motsepe, Motsepe mtu mmbad sana, Kila mbuzi ale urefu wa kamba yake. Kinacho fuatia apo ni safari za marakwamara za vikao Tena inaweza kua nje ya Africa [emoji2][emoji2][emoji2]
 
Walau hii itawafariji mashabiki lia-lia wa simba ambao wamekua wakiumia mnoo kwa kuwa wateja wa yanga mfululizo.
 
Kwa ujumla kinacho onekana Rais wa CAF ndugu Motsepe kashapewa udhaifu wote wa CEO na mshkaji wake Senzo, Kwakua wamegundua CEO anapenda Publicity (Umaarufu) wakaona waanze na Chambo kikubwa.
Kinachofuatia ni kumtakia majukumu mema, ila nampa Big up Motsepe, Motsepe mtu mmbad sana, Kila mbuzi ale urefu wa kamba yake. Kinacho fuatia apo ni safari za marakwamara za vikao Tena inaweza kua nje ya Africa [emoji2][emoji2][emoji2]
Unamuonea wivu mwanamke mwenzio?
 

Mkurugenzi Mtendaji wa Simba SC, Barbara Gonzalez ametangazwa kuwa Makamu wa Rais wa Kamati ya Maandalizi ya Mashindano ya Vilabu vya CAF na Usimamizi wa Mfumo wa Leseni za Klabu

Barbara ndiye mwanamke pekee kwenye orodha hiyo na Rais ni Ahmed Yahya.
Halafu yanakaa matahira kina GENTAMYCINE na wajinga wenzie huko utopolo yanamtukana na kumkosoa
 
Back
Top Bottom