Barcelona Vs AC Milan a.k.a Rosonelli

Barcelona Vs AC Milan a.k.a Rosonelli

Ac milan anachezea goli 4-0..ligi ya italia hakuna kitu siku hizi..ac milan kwa england wana kiwango kama cha wigan.
 
Ac milan anachezea goli 4-0..ligi ya italia hakuna kitu siku hizi..ac milan kwa england wana kiwango kama cha wigan.
....

kwa kuwa una uhuru wa kuandika ushuzi utakavyo basi ni heri yako...

Ila kwa mtu anayejuwa soka hao Manchester UTD wako huwezi kuwapandisha ndege moja na AC Milan
 
ama kwa hakika ni tarehe 13 ya mwezi wa 9 ktk dimba la Nou Camp ambapo kutakuwa na mechi kati ya mabingwa watetezi wa klabu bingwa barani Ulaya yaani Barcelona watakapo pambana na mabingwa mara 7 wa kombe hilo na pia ni timu yenye mafanikio yaani makombe mengi zaidi ya kimataifa kuliko klabu yoyote hapa ulimwenguni hapa naizungumzia klabu ya Rosonelli au AC Milan yenye maskani yake barabara ya Turati mjini Milan Italia.
kocha wa Barca Giussepe Guardiola kama jina lake linavyotamkwa kwa kitaliano ameizungumzia AC Milan kuwa ni timu kubwa na yenye hadhi ya juu kabisa ktk utawala wa soka hapa ulimwenguni na ameeleza wazi kutoisahau kumbukumbu ya kipigo cha Mbwa koko cha goli 4-0 walichokipata Barcelona toka kwa AC Milan na yeye akiwa uwanjani kama mchezaji wa Barca mwaka 1994, ikumbukwe hii ilikuwa ni ktk mechi ya fainali ya kombe hilo.
''Sijawahi kupata fedheha kama ile, hakika Milan walitukamata, na wakatufanya walichotaka, hakika sikuweza kuwa na ujanja, Desaily na Albertini walinifunika ktk kiungo''...amenukuliwa Guardiola mapema leo.


Milan itaingia uwanjani ikiwategeme wachezaji wake mahiri kama sentahafu bora ulimwenguni Alesandro Nesta ambaye inaaminika hajawahi kutokea mkoba mahiri na imara kama yeye tangu alipoondoka Franco Baresi ambaye ni nahodha wa zamani wa AC Milan.
Pia Milan itawategemea viungo mahiri na wenye uzoefu mkubwa mno hapa nawazungumzia MVB yaani Mark Van Bommel, Brigadia Jenerali masimo Ambrosini na Dikteta wa kiungo Clarence Seedorf.

Pia Milan watakuwa na nguli mwenye uwezo wa kupiga mashuti na miguu yote hapa namzungumzia kevin Prince Boateng.


Pia safu ya ushambuliaji ya Buluda itakuwa na kiungo mwenye uwezo wa kupeleka pasi Mlandizi kisha akaifuata na kuichukua tena na kuipeleka Kigamboni kabla ya kupiga pasi ya mwisho itakayomkuta mfungaji.
Kiungo huyu ni Alberto Aquilani atakayekuwa anawalisha mipira Super Pato na Antonio ''MUSOLIN'' Casano.


Kwa upande wa Barca wao watakuwa na Refa, Line men wawili pamoja na kamisaa kama ilivyokawa kawaida yao.

Kawaulize shemeji zako Man U watakupa habarin ya Barca.
 
....

kwa kuwa una uhuru wa kuandika ushuzi utakavyo basi ni heri yako...

Ila kwa mtu anayejuwa soka hao Manchester UTD wako huwezi kuwapandisha ndege moja na AC Milan

Stop living in the past kaka!!! Zungumzia kiwango cha sasa. I hope baada ya mechi leo tutakuwa wote hapa.
 
ulikuwa bado mdogo labda...
Hiyo Barca iliyobakwa 4-0 ilikuwa na watu kama Romalio, Eusebio na Hristo Stoichkov...

Achana na ushuzi huu unaouona wewe bora ila kwa wanaojuwa hii ni wazi kuwa Barca anabebwa na marefa live live...

Kama unaamini hii basi waweza amini chochote
 
ulikuwa bado mdogo labda...
Hiyo Barca iliyobakwa 4-0 ilikuwa na watu kama Romalio, Eusebio na Hristo Stoichkov...

Achana na ushuzi huu unaouona wewe bora ila kwa wanaojuwa hii ni wazi kuwa Barca anabebwa na marefa live live...

Du!! Ya kweli haya?
 
Kawaulize shemeji zako Man U watakupa habarin ya Barca.
....

narudia kukwambIa Barca alishabakwa 4-0 na huyo kocha wao Guardiola akiwa uwanjani.

So usiifananishe Milan na wasichana kama hao uliowataja.

Naomba kuwasilisha hoja
 
Stop living in the past kaka!!! Zungumzia kiwango cha sasa. I hope baada ya mechi leo tutakuwa wote hapa.
...

Nipo, so sema unachotaka kukisema.
Mechi imekwisha kwa matokeo ya magoli mawili kwa mawili na kukamilisha ule usemi ''dobi wa kweli utamjuwa siku akipewa nguo nyeupe''.

Hawa Barca watawafunga watoto wenzao, lakini sio wazee Sugu kama Milan.
 
dah unajua baada ya Real madrid timu inayofuata kwa kutamba ulaya ni AC Milan mabingwa mara 7 kombe la ulaya. Barcelona hawapo kwenye timu zilizochukua mara nyingi kombe la Ulaya wamezidiwa na Liverpool. AC Milan wanauwezo wa kuifunga barcelona. sidhani mchezo wanaocheza barcelona utaendelea kutamba kwa muda mrefu. next stop is san ciro! karibuni sana ingawa nyumbani kwangu ni pale torino inapopatikana JUVE!
 
dah unajua baada ya Real madrid timu inayofuata kwa kutamba ulaya ni AC Milan mabingwa mara 7 kombe la ulaya. Barcelona hawapo kwenye timu zilizochukua mara nyingi kombe la Ulaya wamezidiwa na Liverpool. AC Milan wanauwezo wa kuifunga barcelona. sidhani mchezo wanaocheza barcelona utaendelea kutamba kwa muda mrefu. next stop is san ciro! karibuni sana ingawa nyumbani kwangu ni pale torino inapopatikana JUVE!
.....

Teh teh mi nakwambia Chimungulu umenena vyema kabisa.
Kuna wakurupukaji hawaijui Milan na wako kwa ajili ya kuibeza na kusifia vitimu vyao vIilivyokuja na DSTV.
Wanashindwa kabisa kutambua kuwa Soka ni mchezo unaokwenda kwa historia zaidi na si kukurupuka tu kama watu wa mataifa.

Milan bila Ibra na Robinho, bila Flamini na Gatusso wameweza kupata patulo Nou Camp kwa Barca ambao wenyewe walikuwa full...

Ni punguwani tu ndie anayeweza kudhani Barca watatawala milele.

Forza Milan...
Sempre Milan
 
Aaaaaaaah gang chomba naona chama limekamilika sio ngoja tuone hapo milan itakuwa vp maana umeibeza si kitoto MAN UTD na unajua mziki uko vp?
Hongera sana tunangoja second leg...............
 
<font color="#0000cd"><font size="4"><span style="font-family: courier new">Aaaaaaaah gang chomba naona chama limekamilika sio ngoja tuone hapo milan itakuwa vp maana umeibeza si kitoto MAN UTD na unajua mziki uko vp?<br />
Hongera sana tunangoja second leg...............</span></font></font>
...

dawa ya hivi vitoto wanayo wataliano.
Inter walivipiga na kuvitoa misimu miwili ilopita, na kisha Milan wamepata patulo wakiwa na majeruhi wa kumwaga...

Jiulize kama Ibracadabra angekuwa pale mbele huku akikaa na mipira kusubiri suporter ya wenzake, wakati huo huo Robinho akivitikisa vibeki vyao kwa chenga na kisha kuvitoa baruti kila upande, then Flamini na Gatusso wakikaba mwilini na kutibua mipango ya Barca yoote huku wakiwafokea na kuwabughuzi hakika Barca wangekula za uso palepale kwao...
 
kwa mujibu wa Goal.com Alesandro Nesta yule beki bora wa kati tangu alipoondoka Franco Baresi amechaguliwa kuwa Man of the Match kwa kupata maksi 8.5.

Flop of the match amechaguliwa Sergio Busquets wa Barca.

Forza Milan.
Sempre Milan
 
Back
Top Bottom