Barnaba: Diamond sio Mwanamuziki

Haya makasheshe na wanawake yatampoteza dogo, badala ya kuwaza muziki ye anawaza kushindana na watalaka wake na scandal zao, mara bifu na alikiba, pia naskia ana nyodo sana now days hasa katika malipo ya show zake, naliona anguko lake
 
Masikini Barnaba! Bora ungebaki na hili jambo moyoni tu maana wenzio huku tuna maadui wengi sana kisa kusema ukweli kua Diamond sio mwanamuziki na hajui kuimba!

Kama sio mwanamziki ni mwana nani? Barnaba hajui aina za muziki zilizoko duniani ndio maana kasema hivyo, kuna siku atasema hata Saida karoli si mwanamziki kwa kuwa kakulia shamba.

Kuna mziki wa kufundishwa kidigitari,
Kuna mziki wa mapokeo yaani umejikita kwenye jamii husika bila kuusisha vifaa vya technologia ya kizungu. hivyo basi huenda barnaba hajui mziki kwani analazimika kutumia vyombo zaidi vya kumsaidia kuimba.
 
Mara kwa mara watu wanachanganya sana haya mambo kwa sababu wengi wanaongea vitu kwavile walisikia mahali na wala hawana utaalamu wa jambo lenyewe! Katika hili, wengi sana utawasikia fulani sio mwanamuziki bali ni muimbaji! Kwa mtaalamu wa muziki akishakusikia unatoa hiyo hoja moja kwa moja anafaamu kwamba taaluma ya muziki hauifahamu!

Jambo la kwanza watu wanalotakiwa kulifahamu ni kwamba mwanamuziki anatokana na muziki! Kutokana na hilo, mtu anaye-perform muziki ndie anaitwa mwanamuziki! Ukirudi kwenye muziki wenyewe, pia unagawanywa katika makundi mawili makuu, vocalists yaani waimbaji na instrumentalists ambao ni wacheza ala za muziki! Ukitaka kusema mwimbaji sio mwanamuziki ni kwamba unataka kusema mpiga ala peke yake ndie mwanamuziki wakati hata tafsiri rasmi ya muziki ni kwamba "ni sauti/vocal au ala au mchanganyiko wa vyote kwa pamoja..." Kwahiyo hata mtu anayefanya akapela peke yake, kwa kuzingatia tafsiri ya muziki nae ni mwanamuziki na mwanamuziki wala sio kutembea na gitaa!

Aidha, huyu muimbaji hata kama hafahamu kupiga ala bado katika uimbaji wake analazimika kufuata ala za muziki kama ambavyo wakati mwingine mpiga/waiga ala za muziki (w)anapolazimika kutengeneza ala kulingana na uimbaji wa vocalist na ndio maana hata muimbaji akienda studio na hana uzoefu, kitu cha kwanza atakachoambiwa aimbe akapela ili mtengeneza beats afahamu ni beat za aina gani anaweza kwenda nazo! Ni kama ambavyo mpiga tumba, guitar, saxophone, violin, keyboard na kadhalika anapolazimika kubaki kwenye kifaa chake (eneo moja la muziki as instrumentalist) ndivyo muimbaji anapolazimika kubaki kwenye eneo lingine la muziki as vocalist!

Hoja ya Barnaba angekuwa ameongea kitaalamu angesema Diamond sio profession musician na kimsingi, alichokisema Barnaba kinamaanisha hivyo kwamba Diamond sio professional musician kwa sababu kutokujua kuimba sio kigezo cha kutokuwa mwanamuziki! Profession musician ni yule ambae amesomea muziki, anafahamu staff, notes na clefs kwenye muziki na maana na pia application zake! Hizi staffs, clefs na notes nazo zimegawanyika hadi unachanganyikiwa! Na katika hili, I doubt kama kuna mwana bongo flavor tunayeweza kumuita professional musician... katika hili ni lazima uende music school!

Tofauti ya Barnaba na wamamuziki wengine (including Diamond) ni kwamba, tukichukua pande mbili za muziki, kwamba ni uimbaji na uchezaji ala, Barnaba ni mwimbaji na vile vile ana "idea" na baadhi ya ala za muziki wakati wengine wengi ni waimbaji peke yake!
 
haya makasheshe na wanawake yatampoteza dogo, badala ya kuwaza muziki ye anawaza kushindana na watalaka wake na scandal zao, mara bifu na alikiba, pia naskia ana nyodo sana now days hasa katika malipo ya show zake, naliona anguko lake

usiogope najua maisha magumu ndo tatizo lako
 
Nimesoma comment za wengi... karibu wote hawafahamu mwanamuziki hasa ni nani na muziki hasa ni nini! Hata Barnaba mwenyewe anachanganya kati ya professional musician na ordinary musician na hata maelezo yake yanaelezea unprofessional and professional musician. Na katika muziki, kutokujua kuimba wala sio kigezo cha kutokuwa mwanamuziki na hata kama una sauti mzuri kuliko watu wote duniani na unaimba vizuri kuliko wote duniani bado hicho peke yake hakiwezi kuwa kigezo cha kuwa professional musician or professional singer! Watu hawajui kwamba hata akapela peke yake ni muziki!!
 
Mimi bado S ijaelewa mwanamuziki ni yule anayejua kuimba kwa noten if my spelling is correct au yule mwenye sauti Nzuri hata kama ni cabbo snoppy yule chizi wa Angola.?

kigezo kikubwa kimojawapo cha mtu kuitwa mwanamuziki ni kujua kupiga ala za muziki primarily piano na gitaa.
ukiachana na hilo, mwanamuziki inabid aweze kusoma nota za muziki kwenye karatasi na kuuimba hata kama aliyeandika nota hizo ni mtu wa taifa lingine anayetumia lugha tofauti na yake.
si lazima awe na uwezo wa kutunga wala kuwa na sauti nyororo.
tukija kwa domond, yeye ni just a msanii tu na wala sio mwanamuziki kutokana na kutokuwa na qualification za pale juu.
kwa bongo wanamuziki wapo wachache sana mfano mzuri ni BANANA & BARNABA, at least hao ndio waliokuja kichwan fasta.
 
Huyu barnaba akalale mbele wivu tu, yeye anayemjua muziki basi mbona hata hajulikani kama Diamond duniani?

Wivu...

Haya Diamond kashusha mwimbo mpya na Khadija Kopa kasikilize na video juu bomba yaani usikose utapitwa
 
Bila kumtaja Diamond wanajua interview itaishia kwenye matundu ya masikio ya watu....

Chibu oyeeeeeeeeee wapelekesheeeeeeeeeeeeee

Lazima huyu anatumia Chibu keshokutwa tutasikia anatoa nyimbo mpya
 
Haya makasheshe na wanawake yatampoteza dogo, badala ya kuwaza muziki ye anawaza kushindana na watalaka wake na scandal zao, mara bifu na alikiba, pia naskia ana nyodo sana now days hasa katika malipo ya show zake, naliona anguko lake

Mwanamuziki gani anafunha suruali eti sababu atashuka kimuziki?

Wanawake hao hao wanaompapatikia ndio wanampa chati.

Lini umesikia ametoka na wanawake wawili au watatu kwa wakati mmoja?

Mwanaume gani anafinga suruali kwa wanamuziki tena wengine wachafu haswa kwa tabia zao.

Wamemsema hazai akitoka na single girls sasa kaamua kutoka na mdada aliyeachana na mume mwenye watoto nayo shida.

Wivu unawasumbua kujaji ka vile nyie Mungu na wanawake hawajui ku do na wanaume hawajawai ku do.

Tatizo lake ni nyota
 
Bila kumtaja Diamond wanajua interview itaishia kwenye matundu ya masikio ya watu....

Chibu oyeeeeeeeeee wapelekesheeeeeeeeeeeeee

Lazima huyu anatumia Chibu keshokutwa tutasikia anatoa nyimbo mpya

Sikashatoa nyimbo jana sijui leo hehehe wabongo wanapenda mitelezo sna,ukiwa juu mpaka wakushusha tuu sahz kila mtu anamchukia wakati kAtuweka kwenye ramani siku akiwa kama kina tid na qchif ndo utaona unafki ooh diamond yuko pouwa,ngoja watoto wa pwani tukaangalie mauno
 
Diamond si mwanamuziki ni muimbaji. kwa hiyo Barnaba is right..
 
Bila shaka unafahamu mwanamuziki anatokana na muziki? SWALI: MUZIKI ni nini? Kutokana na maelezo yako nina mashaka ukiwa unafahamu nini maana ya muziki kwa sababu, ala ni sehemu moja ya muziki kati ya sehemu kuu mbili za muziki ambazo ni vocal na instrumental... muziki ni ama vocal au ala au mchanganyiko wa vyote kwa pamoja! ukisema kigezo kimoja wapo cha kuitwa mwanamuziki ni kujua kupiga ala ni kwamba unataka kubadili tafsiri ya nini maana ya muziki na kuondoa kile kipengele cha "ama vocal" na kubakiza vocal na instrumental... na kwa maana hiyo, wapiga ala wote ambao wengi wao sio waimbaji unataka kusema nao sio wanamuziki unless kama tubadilishe tena definition ya muziki kutoka kuwa vocal na instrumental na kubaki kuwa instrumental peke yake!!!
 

So what? Anataka kutuambia kuwa pia 50 cent hajui kuimba nae kutokana anaongea tu au rap ? Kila msanii ana style yake mziki.
 
Huyo Barnaba mwenyewe ufundi wake umemfikisha wapi? Huo ni wivu tu wa maendeleo na aendelee kuimbia puani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…