Stuxnet
JF-Expert Member
- Feb 12, 2011
- 13,417
- 23,310
Kila mmoja ana uhuru wa kutoa mawazo yake ila akipotosha hatuwezi kukaa kimya. Nakuhakikishia umemsingizia Baba wa Taifa huko alipo. Kwa wanao mfahamu Julius Kambarage Nyerere KAMWE ASINGEMUUNGA MKONO Magufuli kwa namna anavyoendesha nchi hususan katika mambo yafuatayo;Salaam Wana JF,
Naanza andiko hili fupi kwa kumshukru Mungu kwa wema wake wote kuendelea kutupenda sisi Watanzania na kutujalia kheri za kila namna katika shughuli zetu za kila siku.
Baada ya Salaam hizo niangazie kusudi la barua hii fupi, Andiko hili kimaudhui ni kutambua Mchango wa kipekee kisiasa, Kijamii, Kiuchumi na kiutamaduni uliofanywa na awamu ya tano chini ya Rais John Pombe Magufuli katika miaka yake 5 ya awali, Bila shaka hakuna Mtanzania yeyote asiyetambua mchango wa Mzalendo huyu namba moja.
Awamu ya tano imekuwa awamu ya kipekee katika falsafa mpya za uwajibikaji tofauti na awamu nyingine zilizopita, Aidha Kitu kinachoitambulisha awamu hii ni "Utu wa Watu, Kazi na Maendeleo ya nchi Kwanza" Falsafa hii kimaudhui inaendana na ile ya Mwl. Nyerere ya "Ujamaa" Kwa nukta hiyo unaweza kuziona fikra za John Pombe Magufuli katika utawala wa watu dhidi ya Mwl. Nyerere na fikra zake.
Rais Wangu John Pombe Magufuli Salaam Kwako na pongezi sana kwa kulihe shimisha taifa langu la Tanzania, umefanya makubwa ambayo Sisi Watanzania wenye nia njema na nchi yetu tunajivunia na uwepo wako, Mhe. Rais maneno yote unayoyasikia kutoka kwa wakosoaji wako yapo yenye tija katika ujenzi wa taifa letu, lakini wengi kati ya wakosoaji hao ni Wanafiki sawa na Mafarisayo waliokuwa wakimjaribu Yesu kwenye Masinagogi huku wangali wanaujua ukweli wa mambo, Aidha ni Watu wanaotumika kuivuruga nchi yetu kwa maslahi yao binafsi na familia zao ambao asilimia yao ni kidogo kulinganisha na sisi tunaokuunga mkono.
Mheshimiwa Rais wapo wanaotumia jina vibaya la Mwasisi wa taifa hili kuwa "Kama angelikuwa hai asinge kubaliana na utaratibu wa sasa katika dhana ya demokrasia inavyotendewa" Wanaojenga hoja hii ni "Washamba kisiasa na pengine hawaijui historia ya taifa letu tokea tulipo pata uhuru" Pengine warejee maandiko ya Prof. Shivji watapata mantiki ya demokrasia katika mataifa ya Afrika.
Mheshimiwa Rais ukweli wa kitafiti ni kwamba Mwalimu Nyerere angekuwepo bado angeungana na wewe na kukupa sifa unazostahili kwa hiki unachokifanya kwa sasa, rejea viongozi wastaafu wa awamu zilizopita wamekukubali na kukupa ushirikiano unaohitajika Why Nyerere? bila shaka hii si hoja Rais wangu zaidi ya kuipuuza na kutambua ugumu wa siasa za Kiafrika kwa maana uongozwa na hila, chuki na uasi kwa waafrika wenyewe hivyo basi puuza na chapeni kazi kwa tija ya taifa zima.
Mheshimiwa Rais nimalizie barua hii fupi kwa kukutakia heri ya mwaka mpya wa 2021, Aidha niombe Falsafa na mitindo yako ya kiutawala uliyoitumia katika kipindi chako cha kwanza cha miaka mitano ya awali uendelee nayo katika kipindi chako hiki cha pili unapoelekea kuhitimisha miaka yako kumi, tunakuombea na sisi Watanzania wazalendo tupo tayari kusaidia kwa namna yoyote tutakapo hitajika kufanya hivyo, Kila la Kheri na Mungu akutangulie.
Ndimi, Deogratias Mutungi.
1. Utawala wa Sheria, kamwe Nyerere hajawahi kuingilia Uhuru Mahakama pamoja na kuwa alitawala kwenye mfumo wa Chama Kimoja
2. Kupendelea Maendeleo Wilaya yake, Nyerere aliingalia Tanzania nzima kwa uzito ulio sawa katika miaka 25 aliyotawala hata barabara lami Butiama ilikuwa haijajengwa mpaka alipotoka. Huyu miaka 3 tu kapeleka Airport, Mbuga ya wanyama, Hospitai ya Mkoa na Uwanja wa mpira wa miguu uko mbioni
3. Kuua wakosoaji, Nyerere hakuwaua japo aliwaweka kizuizini kwa wakati fulani. Huyu kamuua Ben Saanane, Azory Gwanda, na kmashambulia Tundu Lissu kwa risasi
4. Kubambikiza wakosoaji kesi, wakosoaji kama akina Eric Kabendera, Tito Magoti, Mdude Chadema nk
5. Kuwanyanga'anya fedha matajiri , kama akina James Rgemalira kwa kisingizio cha Plea Bargaining
6. Ufujaji au Ufisadi. Huyu kwa miaka 4 CAG aligundua kuwa fedha zipatzo Tsh 2.4 Trilioni hajulikani ziko wapi
7. Vyama vya upinzani, Nyerere ndiye mwasisi wa vyama vingi na aliviunga mkono. Huyu anataka utawala wa KIDKTETA na hapendi vyama vya upizani kabisa
Nataja hayo machache tu ili kulinda hadhi ya Baba wa Taifa. Niko tayari kuwajibika kwa maneno yangu katika kutetea jina la Baba wa taifa ambalo linachafuliwa makusudi na Deogratias Mutungi