Barua ya Adam Malima kumpinga Spika!

Barua ya Adam Malima kumpinga Spika!

Status
Not open for further replies.
Hiyo itakuwa maada au semina?Na kama ni mada mtoaji ni nani?au mimi sijaelewa kitakachojiri baada ya hicho kipindi cha maswali?

baada ya maswali na majibu Bunge huendelea..................Kazi vuta subira jumanne sio mbali. Hakuna semina ni kazi za bunge
 
Jamani,
labda mie nimepitwa hapa tafadhali naomba mnielimishe ni wapi palisemwa/kuandikwa kuwa Malima hana hatia?
 
Mzee Ogah,

Paliposemwa na kuandikwa kuwa Mh hana hatia na hapa;

6.0 TAARIFA NA USHAURI WA KAMATI YA KINGA, MAADILI NA
MADARAKA YA BUNGE


6.1 Baada ya Kamati ya Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge kukamilisha uchunguzi wake, iliwasilisha taarifa yake kwangu pamoja na taarifa ya maoni tofauti (dissenting views) ya wajumbe wake wawili.


6.2 Katika taarifa hiyo, Kamati ya Kinga, Maadili na Madaraka ya Bunge Kamati iliridhika kuwa Mhe. Adam K.A. Malima (Mb.), hakusema uongo ndani ya Bunge, na kwamba hakukuwa na uthibitisho wowote kuwa ana maslahi binafsi na kile alichokisema Bungeni.


6.3 Kwa matokeo hayo, Kamati ilishauri Bw. Reginald Mengi aarifiwe kuhusu matokeo hayo ya uchunguzi wa Kamati, na pia Bw. Mengi ashauriwe kuwa makini katika matumizi ya vyombo vya habari, hasa vile anavyovimiliki.


6.4 Aidha, Kamati ilishauri kuwa, Mhe. Malima ajibiwe maombi yake ya Mwongozo wa Spika kuwa, alipokuwa anachangia Bungeni tarehe 2 Agosti, 2006, alikuwa sahihi kulingana na misingi ya Katiba, Sheria na Kanuni za Bunge, na kwamba, akipenda afuate taratibu zaidi za kisheria, kwa kuwa, kushambulia mchango wa mbunge mmoja mmoja wakati anatekeleza majukumu yake ya kikatiba si halali na mhusika wa kutenda kosa hilo anaweza kushtakiwa mahakamani

Mzee ES,

Nadhani umeuona mchango wa Mh Zitto hapo juu kuwa PCB wanachunguza rushwa

Sina shaka sasa umeelewa.

Kuhusu kitabu nami nimo mbioni kukitafuta


Mungu Ibariki Tanzania
 
Phillimon mikael. a.k.a Chief marreale.

ZEE LA UKABILA NA UDINI UMERUDI? au ULIENDA KUFANYIWA OPERATION YA MAKENGEZA YAKO?
STAY TUNED.


mswahili vipi arifu..mbona unanijia na mbinu zako za matusi ....huwa sijibu upupu .kama ni mbinu kama hizo tunazijua 1001 na hatuzitumii...wewe kama ulizipata kivukoni ..watu wamepitia kote korea,russia,america na kufuzu..ets[kiddin]

well back to the point,i am really taken by surprise with this fishy that whenever some firms here in forum are even mentioned ,some guys get hysteria...whats a big deal you better tell...au ukweli unauma.mbona yule mama wa psrf hamumuongelei ....
what i said or meant was " hii hoja ya udini kwenye hii kashfa haipo ila manji na wenzake wameiibua ili kupata sympathy ionekane wanaonewa kwa sababu yeye, na hao wakurugenzi ni dini moja,so symply UDINI HAUPO, ila umeibuliwa"

na manji ni smart wa kucheza na sysytems ya devide and move[rule]...kwani kwenye lile sakata la kiwanja CHA BAKWATA TEMEKE...waislamu walipokuja juu baada ya yeye kuiiziwa "kihalali" yeye aliwachanganya bakwata wakafukuzana ...na hadi leo hii anasubiri waislamu wasahau ili ajenge godown pale ...eleweni huyu ni mtu wa ku take advantage..i dont care who is in his payroll here or anywhere else!!
na kwa upande mmoja mbinu zao na mengi wanafanana ila tatizo kubwa ni pale wanapozidiana ,ndio utasikia mmoja analia!!!!!

who nimekusikia ,ila sioni kama kweli wewe ni mlala hoi au msaka tonge,kuna haja ya kutETEA ufujaji uwe wa magodown ...yet tunasifia oooh fulani ni mchapakazi...bilioni 85 zingetosha kabisa kujenga daraja pale kigamboni..guys call spade a spade !!!! wizi na ufujaji tuuuite hivyo hata akiufanya ndugu au rafiki yangu,nitauita hivyo!!!!!!!!!!

mwalimu alimfunga macarios kwa sababu alisema ameiweka serikali mfukoni...sasa kama leo kuna mtu ametuhumiwa kununua wajumbe wa kamati[na ndessa],,PCB lazima wachunguze...na pia wachunguze madai kwamba malima aliyasema aliyosema bungeni kwa influence ya interest zake QUALITY GROUP..maana hata kabla malima hajasema hayo duru za wachunguzi walikuwa na taarifa ya manji kupenyeza hii hoja kwa baadhi ya wabunge na offcorse pia taarifa za mengi nae kutafuta kuungwa mkono zilikuwepo.....
 
PHILEMON MICHAEL

huko nyuma ulisema hivi:


Quote:
kuhusu propaganda nilisema nilihisi kwamba mswahili anapiga sana propaganda dau...kiasi kwamba hamtyendei haki ...ni sawa na kumuharibia ..dau bado ni kijana na nauwezo wa kufanya zaidi sasa kama atahusishwa na mswahili itafanya mbele ya safari akose SIFA ZA KITAIFA...kama anafanya kazi watu wanaona ,hakuna haja ya kumpigia mayowe,wakurugenzi wa mashirika ya umma wapo wengi wanaofanya vizuri...

wakurugenzi waliotangulia wa NSSF kama sikosei mkullo mustapha ,ndie aliyejenga investments nyingi...zikiwemo hosteli za chuo ...sasa kama ujenzi ulipoisha alishastaaafu ..hilo sijui...ni kama uwanja wa taifa mpya utakapoisha mwezi wa saba ,..je tutasema umejengwa na kikwete au mkapa..kwa kifupi maendeleo ya taasisis yoyote ni TEAM WORK na sio ONE MAN SHOW...anaepokea kijiti anakuwa muendelezaji ....

http://www.jamboforums.com/showthrea...NSSF#post24289


kisha siku chache baadae ukaendelea kusema hivi:


Quote:
kuhusu NSSF naona hakuna tofauti kati ya dau na mkullo au mattaka...tena sanasana DAU bado hajafanya vivid investment kulinganisha na enzi ya kina mkullo au mattaka [hata mkimsema ..jamaa ni kichwa ]....ila aendelee kujitahidi ..na nafikiri ni mtu anayetumia sana propaganda chini chini..natambua ni PAN AFRICA mzuri na mtoto wa mjini ,,,but we want more results...

http://www.jamboforums.com/showthrea...NSSF#post24278

na mimi nilikuuliza BWANA PHILEMON MICHAEL maswali ambayo mpaka leo HUJAJIBU hata moja ku back up arguments zako. na leo ninarudia kukuliza tena hayo maswali na ukiyajibu then tutaendelea kujadiliana based on hoja katika majibu yako


Je,Dr DAU aliingia NSSF lini?

Alikuta makusanyo pale NSSF chini ya MKULO yalikuwa kiasi gani?

Sasa hivi yako kiasi gani?

Je Kulikuwa na investments za kiasi gani?

Sasa hivi investments zimefikia kiasi gani?

Na ni Propaganda zipi anazitumia kuendesha shirika kubwa la wanachi la NSSF?

Na imekuwaje ameweza kusurvive pale muda wote huo tangu MKAPA amuweke pale?

Kuna udini gani kule NSSF? naomba at least ushahidi wa hata wa newsclip.
 
Duh!...amakweli...kwenye makosa madogo madogo mpumbavu hujifanya jasiri!!...........
 
Wandugu

Kitu ninachopenda hapa JF ni watu wanavyokuwa wanaacha ushabiki na kuzungumzia FACTS. ule ushabiki wa wanaosema ndiyo waseme ndio, ndioooooooooo nknk , i.e. ushabiki wa Simba na Yanga hapa JF si MAHALI pake

The Content of the material tells the fact kwamba Mh Malima alisema UONGO period. other than that ni USHABIKI ambao ni waste of time kama ambavyo sasa huyu kid kilaza anajitahidi kufanya (kwenda kwa Makamba). and afterall ITV sio TVT!!!

kwa mabye hakuona hebu soma hapa chini..................
SPIKA ALISEMA---Kauli ya Mhe. Malima kwamba:-
"Nimewahi kushuhudia mimi Rais wa Jamhuri ya Muungano ana habari nzito kwenye taarifa ya habari ya saa mbili anapewa dakika moja na nusu, Waziri Mkuu anataka kuzungumzia njaa anapewa dakika moja na nusu, watoto wa ‘Primary' wanakuja kutoka Zanzibar kutembelea Kiwanda cha Coca-Cola wanapewa dakika kumi. Mmiliki wa TV anakwenda kuongea na watoto wa Madrasa Msasani kwa ajili ya kugombana na Sheikh mmoja anapewa dakika kumi."

SPIKA AKAENDELEA, "Inadhihirisha wazi na kushawishi kuwa Mhe. Malima alikuwa anatoa taarifa ya jambo alilolishuhudia yeye mwenyewe.

Katika kauli yake, Mhe. Malima alikuwa anazungumzia kitu cha kitaalam, yaani muda wa kurusha matangazo hewani (Air time), ambapo muda hupimwa kwa sekunde. Kamati ilifanya uchunguzi kwa kuangalia kanda za televisheni za matukio yote yaliyokuwa yametajwa Bungeni na Mheshimwa Malima. Imedhihirika kwamba, kanda za pande zote mbili yaani za Bw Mengi na alizoziwasilisha Mhe Malima. Imebainika kuwa, si kweli kwamba, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alipewa dakika moja na nusu, watoto wa Primary kutoka Zanzibar waliotembelea Kiwanda cha Coca-Cola walipewa dakika kumi na Mmiliki wa ITV alipokuwa anaongea na watoto wa Madrasa Msasani alipewa dakika kumi.

Katika ushahidi wa kanda iliyowasilishwa na Bw. Mengi, tukio la Bw. Mengi kutembelea Madrasa ya Msasani lilirushwa hewani kwa dakika 4.21, tukio la ziara ya watoto wa Laurent International ya Zanzibar kutembelea ITV Mikocheni lilirushwa hewani kwa dakika 3.17, tukio la Waziri Mkuu akizungumzia njaa lilirushwa hewani kwa dakika 5.04 na tukio la ziara ya Rais Msumbiji lilirushwa hewani kwa dakika 3.31.

7.2.6 Katika ushahidi wa kanda iliyowasilishwa na Mhe. Malima, tukio la ziara ya Rais Msumbiji lilirushwa hewani kwa dakika 3.20, tukio la Waziri Mkuu akizungumzia suala la njaa lilirushwa hewani kwa dakia 4.28, na matukio ya Bw. Mengi kutembelea Madrasa ya Msasani na lile la watoto wa ‘Primary' ya Zanzibar kutembelea ITV na Coca-cola yalirushwa hewani kwa dakika 5.50 kwa ujumla wake.

7.2.7 Matokeo hayo ya uchunguzi wa Kamati hiyo ya Bunge yanaonesha wazi kuwa, matamshi ya Mhe. Malima hayakutimiza masharti niliyoyataja kwenye aya ya 5.4.2.1 hapo juu, yaani kwamba, yamevunja na kukiuka masharti na matakwa ya Kanuni ya 50(1) ya Kanuni za Bunge (Toleo la 2004) ambayo, pamoja na mambo mengine, inapiga marufuku Mbunge yeyote kusema Uwongo Bungeni."


Kwa uelewa mzuri, Kanuni hiyo inatamka kwamba:-

"Ni marufuku kabisa kusema uwongo Bungeni. Kwa sababu hiyo, Mbunge yeyote anapokuwa akisema Bungeni, atawajibika kuwa na hakika kwamba, maelezo anayoyatoa ni sahihi, na siyo mambo ya kubuni au ya kubahatisha tu;"…

Ukweli huo unatusaidia kujibu hoja ya pili kwamba, kutokana na kukiuka masharti ya Kanuni ya 50(1) ya Kanuni za Bunge, matamshi ya Mhe. Malima aliyoyatoa Bungeni hayana kinga inayotolewa na Ibara ya 100(1) ya Katiba na Kifungu cha 3 cha Sheria ya Kinga, Madaraka na Haki za Bunge, 1988.
 
Spika kaboronga.. na hana budi kusahihisha alipoboronga! Hili suala wala lisingechukua muda mrefu hivi na kutumia pesa nyingi kiasi hiki!
 
Mwanakijiji,
what exactly does Honourable Malima want the Speaker to do? He made remarks on the parliament's floor which later were proved to be inaccurate.

My reading is that the Speaker did not want to sanction Hon.Malima and embarrass a fellow CCM member. I think that is why the Speaker tried to sort this issue outside parliament procedures by suggesting that Hon.Malima reconcile with Mr.Mengi.
 
Spika bomu toka anachaguliwa tulilijua hilo.
Anyway kina phillimon mikael wakishirikiana na Mengi wameshamuona tusitegemee haki toka kwake.

Dr.Who Usishughulike sana na Phillimon mikael huyu ni founding member wa Kilimanajaro development forum na Chadema. unategemea nini? ni kulinda maslahi ya wachagga wenzake.

ndio maana suala la TRA aliliwekea vikao lukuki kuwaambia wachagga wenzi wake kuwa kuna vita na mswahili jambo forum.
ile vurugu ya Ndesamburo kwenye kamati ilikuwa ni mpango wa maksudi ili Spika aweze kupeta kwa nafasi.

Phillimon mikael umenitolea matusi mengi tu kwenye ukabila TRA yote nimekusamehe.
nani asiyekujua wewe na uchagga? ni wewe uliyeanzisha thread ya tanzia ya Marealle na kumjenga sana kana kwamba hakuna mashujaa wengine kama KINJEKETILE. MKWAWA. n.k.

wacha tunakutizama tu. kwetu sisi huwashi wala kuzima.

lazima utampigia chapuo Mkullo sababu mizigo na tenda za ubabaishaji zilikuwa za wachagga, sasa kuna Fairness kaisi hata Mzigua au Mkinga akiwa bid tender kama ame meet criteria anachukua kazi au tenda Nssf BILA kutoa sumni yake.
 
Mwanakijiji,
.....My reading is that the Speaker did not want to sanction Hon.Malima and embarrass a fellow CCM member. I think that is why the Speaker tried to sort this issue outside parliament procedures by suggesting that Hon.Malima reconcile with Mr.Mengi.


Joka Kuu.. did I say that Speaker kaboronga? I sure did!
 
Ogah,

Heshima mkuu nakukumbka toka BCS, maneno yako msumari kama Malima hana kosa basi Mengi ndiye mwenye makosa, haiwezekani kuwa wote hawana makosa,

Spika anatakiwa awajibishwe kwenye hili, na inawezekana hiyo kwani yeye pia ni mbunge wa kuchaguliwa kwa hiyo bado anabanwa na sheria za wabunge!

Otherwise respect kwa maneno yako safi!
 
ES,
Finally nakubaliana na wewe kuwa Spika kachemsha na awajibishwe!
 
mswahili kuanzisha thread ni dhambi!!!!? kama tunaingilia ugali wa watu tuambiwe...wengine tunafanyia interest kama jukumu letu kwa taifa na jamii,hatutetei mtu mmoja mmoja kama wale/yule ANAYELIPWA.
 
Hii extract toka Mwananchi (7/4/2007) ina maelezo ya ziada katika sakata hili.


Wanamtandao wamalizana wenyewe kwa wenyewe

Na Waandishi Wetu

MKAKATI kabambe umesukwa kuhakikisha kuwa Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima (CCM) ambaye ameonyesha jeuri ya kudharau maamuzi halali ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta anashughulikiwa na hatafurukuta.

Malima, anadaiwa alikaidi uamuzi wa Spika Sitta ambaye alijaribu kumaliza mzozo uliokuwapo kati ya Malima na mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi.

Kutokana na kuibuka kwake katika sakata hilo, kundi mojawapo kati ya yale ya wanamtandao ‘maslahi’ na wanamtandao ‘matumaini’, limekuwa likimtumia kama chambo na hivyo jingine kuapa kumshughulikia ili kusudi kulipiza kisasi kutokana na kile, kundi hilo linachokieleza kuwa ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu.

Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umegundua kuwa kundi hilo linajumuisha pia baadhi ya mawaziri wa awamu ya nne ambao kwa namna moja ama nyingine wameumizwa na maamuzi ya vigogo wa ngazi za juu na hivyo kujikuta wakiwa na wakati mgumu.

Habari za uhakika ilizonazo Mwananchi Jumapili zimeeleza kuwa upo uwezekano wabunge machachari wanaotoka nje ya mtandao kusimama na kisha kuwasilisha hoja binafsi ya kutaka Mbunge Adam Malima aadhibiwe na kisha kama kanuni zinavyotaka busara ya Spika itachukua nafasi kwa kuwa katika kanuni za bunge hakuna vifungu vinavyomlinda mbunge huyo.

Malima, ndiye ambaye aliyeanzisha mzozo huo kwa kumshtaki Sitta kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Yusuf Makamba, hatua ambayo tayari wachunguzi wa mambo wanaiona kuwa ni jitihada za kujaribu kumdhibiti spika huyo wa bunge.

Pia, uamuzi wa Malima kuamua kumshtaki Sitta nje ya utaratibu na kanuni za Bunge, nao umesababisha kuibuka kwa maswali mengi miongoni mwa wabunge, ambao baadhi yao wameshaanza kukiona kitendo hicho kuwa ni cha kulidhalilisha kimamlaka bunge hilo.

Hatua hiyo ya wabunge inasemekana kuwa inachukuliwa katika kuhakikisha kwamba wanakomesha kabisa kiburi na dharau iliyoanza kujijenga kwa mbunge huyo na wengine wenye tabia kama yake ingawa kwa upande mwingine mbunge huyo na kundi lake wanaonekana kupambana na wimbi kubwa la wanamtandao.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 51 (1), mbunge yeyote anaweza kuamsha hoja kuwa mbunge aliyekiuka kanuni za bunge asimamishwe ubunge na hatimaye mbunge husika ataitwa kujitetea na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge atawasilisha taarifa za mwenendo wa mbunge na hatimaye hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mbunge husika.

Hata hivyo, kwa namna yoyote ile mzigo wa mzozo huo uliochukua sura nyingi, zikiwamo za udini, uanamtandao na visasi, unaelekea kumwangukia Malima kwa kiasi kikubwa.

Awali, katika maamuzi yake wakati akifunga kikao kilichopita cha Bunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, alisema Malima, alishindwa kuthibitisha ukweli wa madai yake dhidi ya Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi kuwa, Rais na Waziri Mkuu, hupewa muda mfupi kwenye televisheni ya ITV wakati wa taarifa ya habari ya saa 2:00 usiku.

Mbunge huyo pia alidai kuwa, wakati viongozi hao wakuu wa kitaifa wakipewa muda mfupi, Mengi ambaye ndiye mmiliki wa kituo hicho cha ITV, hupewa muda mrefu zaidi.

Sitta alisema matamshi hayo ya Mbunge Malima yalikuwa na nia ya kulifanya Bunge liamini maneno yake huku akijua wazi kuwa hakuwa na uhakika wa alichokuwa anakisema.

Maamuzi hayo ya Spika yalikuwa katika kitabu chenye kurasa 32 na alichukua muda wa takriban saa moja kuyasoma.

Alisema ni dhahiri kutokana na ukweli huo, Malima alikiuka kanuni namba 50 (1) inayokataza kusema uongo bungeni na inayomtaka mbunge kuwa na hakika kwamba maelezo anayoyatoa ndani ya chombo hicho, ni sahihi na si mambo ya kubuni au kubahatisha tu.

Tayari, zipo taarifa za uhakika kwamba mbunge mwingine machachari, Chacha Wangwe wa Tarime (Chadema) ameshapanga kuondoa kauli yake dhidi ya spika na hivyo kumuondoa katika orodha ya watakaoadhibiwa katika kikao hiki cha bunge.

Wakati hayo yakiendelea kwa upande mwingine kamati maalumu iliyopanga kula sahani moja na vigogo wa serikali waliohusika na mikataba mibovu ya Richmond, inakutana kesho kulishughulikia suala hilo ipasavyo.

Kabla ya kikao hicho itakumbukwa kwamba kwenye mkutano wa bunge lililopita, suala hilo la Richmond lilitarajiwa kuchomoza, lakini zikafanyika jitihada za nguvu na makusudi na suala hilo likazimwa.

Ni wazi safari hii hoja hii itajadiliwa na Spika Sitta ameshatoa baraka zake zote ili hoja hiyo ifike ndani ya Bunge na kusubiri mjadala mkali.
 
Hii extract toka Mwananchi (7/4/2007) ina maelezo ya ziada katika sakata hili.


Wanamtandao wamalizana wenyewe kwa wenyewe

Na Waandishi Wetu

MKAKATI kabambe umesukwa kuhakikisha kuwa Mbunge wa Mkuranga, Adam Malima (CCM) ambaye ameonyesha jeuri ya kudharau maamuzi halali ya Spika wa Bunge, Samuel Sitta anashughulikiwa na hatafurukuta.

Malima, anadaiwa alikaidi uamuzi wa Spika Sitta ambaye alijaribu kumaliza mzozo uliokuwapo kati ya Malima na mfanyabiashara maarufu, Reginald Mengi.

Kutokana na kuibuka kwake katika sakata hilo, kundi mojawapo kati ya yale ya wanamtandao ‘maslahi’ na wanamtandao ‘matumaini’, limekuwa likimtumia kama chambo na hivyo jingine kuapa kumshughulikia ili kusudi kulipiza kisasi kutokana na kile, kundi hilo linachokieleza kuwa ni utovu wa nidhamu wa hali ya juu.

Uchunguzi wa Mwananchi Jumapili umegundua kuwa kundi hilo linajumuisha pia baadhi ya mawaziri wa awamu ya nne ambao kwa namna moja ama nyingine wameumizwa na maamuzi ya vigogo wa ngazi za juu na hivyo kujikuta wakiwa na wakati mgumu.

Habari za uhakika ilizonazo Mwananchi Jumapili zimeeleza kuwa upo uwezekano wabunge machachari wanaotoka nje ya mtandao kusimama na kisha kuwasilisha hoja binafsi ya kutaka Mbunge Adam Malima aadhibiwe na kisha kama kanuni zinavyotaka busara ya Spika itachukua nafasi kwa kuwa katika kanuni za bunge hakuna vifungu vinavyomlinda mbunge huyo.

Malima, ndiye ambaye aliyeanzisha mzozo huo kwa kumshtaki Sitta kwa Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi, Yusuf Makamba, hatua ambayo tayari wachunguzi wa mambo wanaiona kuwa ni jitihada za kujaribu kumdhibiti spika huyo wa bunge.

Pia, uamuzi wa Malima kuamua kumshtaki Sitta nje ya utaratibu na kanuni za Bunge, nao umesababisha kuibuka kwa maswali mengi miongoni mwa wabunge, ambao baadhi yao wameshaanza kukiona kitendo hicho kuwa ni cha kulidhalilisha kimamlaka bunge hilo.

Hatua hiyo ya wabunge inasemekana kuwa inachukuliwa katika kuhakikisha kwamba wanakomesha kabisa kiburi na dharau iliyoanza kujijenga kwa mbunge huyo na wengine wenye tabia kama yake ingawa kwa upande mwingine mbunge huyo na kundi lake wanaonekana kupambana na wimbi kubwa la wanamtandao.

Kwa mujibu wa Kanuni Namba 51 (1), mbunge yeyote anaweza kuamsha hoja kuwa mbunge aliyekiuka kanuni za bunge asimamishwe ubunge na hatimaye mbunge husika ataitwa kujitetea na Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge atawasilisha taarifa za mwenendo wa mbunge na hatimaye hatua kali zitachukuliwa dhidi ya mbunge husika.

Hata hivyo, kwa namna yoyote ile mzigo wa mzozo huo uliochukua sura nyingi, zikiwamo za udini, uanamtandao na visasi, unaelekea kumwangukia Malima kwa kiasi kikubwa.

Awali, katika maamuzi yake wakati akifunga kikao kilichopita cha Bunge, Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano, Samuel Sitta, alisema Malima, alishindwa kuthibitisha ukweli wa madai yake dhidi ya Mwenyekiti wa IPP, Reginald Mengi kuwa, Rais na Waziri Mkuu, hupewa muda mfupi kwenye televisheni ya ITV wakati wa taarifa ya habari ya saa 2:00 usiku.

Mbunge huyo pia alidai kuwa, wakati viongozi hao wakuu wa kitaifa wakipewa muda mfupi, Mengi ambaye ndiye mmiliki wa kituo hicho cha ITV, hupewa muda mrefu zaidi.

Sitta alisema matamshi hayo ya Mbunge Malima yalikuwa na nia ya kulifanya Bunge liamini maneno yake huku akijua wazi kuwa hakuwa na uhakika wa alichokuwa anakisema.

Maamuzi hayo ya Spika yalikuwa katika kitabu chenye kurasa 32 na alichukua muda wa takriban saa moja kuyasoma.

Alisema ni dhahiri kutokana na ukweli huo, Malima alikiuka kanuni namba 50 (1) inayokataza kusema uongo bungeni na inayomtaka mbunge kuwa na hakika kwamba maelezo anayoyatoa ndani ya chombo hicho, ni sahihi na si mambo ya kubuni au kubahatisha tu.

Tayari, zipo taarifa za uhakika kwamba mbunge mwingine machachari, Chacha Wangwe wa Tarime (Chadema) ameshapanga kuondoa kauli yake dhidi ya spika na hivyo kumuondoa katika orodha ya watakaoadhibiwa katika kikao hiki cha bunge.

Wakati hayo yakiendelea kwa upande mwingine kamati maalumu iliyopanga kula sahani moja na vigogo wa serikali waliohusika na mikataba mibovu ya Richmond, inakutana kesho kulishughulikia suala hilo ipasavyo.

Kabla ya kikao hicho itakumbukwa kwamba kwenye mkutano wa bunge lililopita, suala hilo la Richmond lilitarajiwa kuchomoza, lakini zikafanyika jitihada za nguvu na makusudi na suala hilo likazimwa.

Ni wazi safari hii hoja hii itajadiliwa na Spika Sitta ameshatoa baraka zake zote ili hoja hiyo ifike ndani ya Bunge na kusubiri mjadala mkali.


hiyo article iko page gani?
 
Kama alivyobashiri Mh Zitto Bunge hili huenda likaandika kahistoria kapya! moja ninaloliona hapa ni kwa mara ya kwanza wabunge wa ccm na wapinzani kujikuta ktk kambi moja!

We have to stay tuned!

Mungu ibariki Tanzania
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom