Barua ya vitisho atumiwa Anton Ferdinand

Barua ya vitisho atumiwa Anton Ferdinand

Shine

JF-Expert Member
Joined
Feb 5, 2011
Posts
11,481
Reaction score
1,368
Polisi wa Uingereza wanachunguza barua ya vitisho iliyotumwa kwa mchezaji wa QPR Anton Ferdinand.
Maafisa wa Polisi wa Metropolitan wamekataa kueleza kilichoandikwa katika barua hiyo aliyotumiwa Ferdinand au lini walipokea malalamiko kuhusiana na barua hiyo.
Msemaji wa Polisi amesema: "Naweza kuthibitisha maafisa wetu wanachunguza juu ya tuhuma hizo za vitisho zilizotumwa kwa njia ya barua."
Ferdinand yupo katika mzozo unaohusiana na tuhuma za kutupiwa maneno ya kibaguzi na nahodha wa Chelsea na England John Terry, wakati QPR ilipocheza na Chelsea, tuhuma ambazo Terry amezikanusha.
Polis na Chama cha Soka cha England - FA, wanachunguza madai hayo ya kauli za kibaguzi, ambazo Ferdinand anadai Terry alimtamkia mwezi wa Oktoba katika uwanja wa Queens Park Rangers wa Loftus Road.

BBC
 
kwa Terry sishangai,anaweza kuwa kweli alitoa/tamka maneno ya kibaguzi
 
Back
Top Bottom