Mwan mpambanaji
JF-Expert Member
- Apr 3, 2008
- 482
- 131
Wanabodi salaam
Hii ni barua ya wafanyabiashara mkoa wa Arusha wakilalamika bwana mmoja, huyu jamaa bado yupo enzi zile za pontio plato za kutishia watu ili ajipatie fedha, anakufanyia upepelezi feki ili iwe rahisi kukufanya utoe fedha
Taarifa za uhakika huyu bwana ana ukwasi mkubwa na amejenga shule moja huko Moshono/Mwanama inaitwa Luomo school.
Mbaya zaidi amefanya kazi kituo kimoja kwa miaka 15, ni wazi kuna wakubwa ambao wananufaika na huyu bwana.
Tunaomba Mamlaka ichukue hatua za kisheria dhidi yake!
Wafanyabiashara tunaomba huruma ya Mh Rais Samia Suluhu
===
ATT: ALPHAYO J. KIDATA
KAMISHNA MKUU
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA
S.L.P 11491
DAR ES SALAAM.
YAH:MALALAMIKO DHIDI YA MTUMISHI WA TRA/ARUSHA BW. LOSHIE LAIZER.
Somo hilo hapo juu lahusika.
Sisi wafanyabiashara wakubwa katika Mkoa wa Arusha tunapenda kuchukua fursa hii kukupongeza kwa moyo wa dhati kwa kuteuliwa kwako na tena na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mheshimiwa SAMIA SULUHU HASSAN kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Tunaamini kuwa uteuzi huu uliofanywa na Mheshimiwa Rais Wetu mpendwa uunaoonyesha imani kubwa juu yako kuwa utarekebisha na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara nchini ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo wanaounda kundi linaloongoza katika ukusanyaji wa mapato ya nchini.
Kwa msingi huo tunaamini kwamba utasikiliza malalamiko na kilio chetu kuhusu baadhi ya watumishi ndani ya Mamlaka (TRA) ambao wamekuwa mwiba kwa wafanyabiashara kwa kubambikizia makadirio makubwa ya kodi yasiyozingatia sheria za nchi hivyo kutengeneza mianya ya kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara.
Mheshimiwa Kamishna,
Tunaomba kuchukua nafasi kuwasilisha kwako malalamiko yetu kuhusu mtumishi wa TRA Arusha Bw.Loshie Laizer wa kitengo cha uchunguzi/upelelezi kuwa amekuwa na tabia ya kuwanyanyasa wafanyabiashara hasa wakubwa kwa kubambikia makadirio ya malimbikizo ya kodi baada “kuchungulia” akaunti zao binafsi katika mabenki na pia akaunti za biashara wanazomiliki.
Mtumishi huyo amekuwa akitumia njia za vitisho dhidi ya wafanyabiashara kuwa endapo hata kubaliana na matokeo ya uchunguzi “feki” kuwa anadaiwa malimbikizo makubwa ya kodi basi ataagiza mamlaka nyingine za kiserikali kumfungulia mfanyabiashara husika kesi ya uhujumu uchumi au ya utakasishaji fedha (ML).
Kutokana na vitisho hivyo wafanyabiashara wengi wameingia katika mtego wa mtumishi huyo wa kutoa chochote (rushwa) ili kuepuka usumbufu na pia kuogopa kufunguliwa kesi hasa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Mheshimiwa Kamishna,
Taarifa zinaonyesha kuwa mtumishi huyo amekuwa akifanya kazi katika eneo moja (Mkoa wa Arusha) kwa zaidi ya miaka 15 jambao ambalo si la kawaida kwa watumishi umma hivyo kuzua maswali yasiyo na majibu kwa wadau na wafanyabiashara.Kuna madai kuwa kila mamlaka ilipojaribu kumhamisha mtumishi huyo alitumia njia mbalimbali kuzuia umahisho huo.
Kuna madai kuwa mtumishi huyo ana ukwasi mkubwa kwa kumiliki mali kadhaa kama nyummba za kupanga mashamba na hisa katika baadhi ya biashara kubwa mjini Arusha ikiwemo shule ya LOAMO iliyopo eneo la Olorien katika Jiji la Arusha ambayo ni moja katika ya shule kubwa mjini Arusha.
Mheshimiwa Kamishna tunaomba uchunguzi huru na wa haki ufanyike dhidi ya mtumishi huyo ili kuwaondoelea adha,manyanyaso, na hofu wanayopata wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha na tunaamini kuwa kilio chetu kitafanyiwa kazi.
Tunatangauliza shukrani zetu.
Omar SS.
Kwa niaba ya wafanyabiashara
Arusha.
Hii ni barua ya wafanyabiashara mkoa wa Arusha wakilalamika bwana mmoja, huyu jamaa bado yupo enzi zile za pontio plato za kutishia watu ili ajipatie fedha, anakufanyia upepelezi feki ili iwe rahisi kukufanya utoe fedha
Taarifa za uhakika huyu bwana ana ukwasi mkubwa na amejenga shule moja huko Moshono/Mwanama inaitwa Luomo school.
Mbaya zaidi amefanya kazi kituo kimoja kwa miaka 15, ni wazi kuna wakubwa ambao wananufaika na huyu bwana.
Tunaomba Mamlaka ichukue hatua za kisheria dhidi yake!
Wafanyabiashara tunaomba huruma ya Mh Rais Samia Suluhu
===
WAFANYABIASHARA/ARUSHA
13.5.2021.
13.5.2021.
ATT: ALPHAYO J. KIDATA
KAMISHNA MKUU
MAMLAKA YA MAPATO TANZANIA
S.L.P 11491
DAR ES SALAAM.
YAH:MALALAMIKO DHIDI YA MTUMISHI WA TRA/ARUSHA BW. LOSHIE LAIZER.
Somo hilo hapo juu lahusika.
Sisi wafanyabiashara wakubwa katika Mkoa wa Arusha tunapenda kuchukua fursa hii kukupongeza kwa moyo wa dhati kwa kuteuliwa kwako na tena na Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania Mheshimiwa SAMIA SULUHU HASSAN kuwa Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Tunaamini kuwa uteuzi huu uliofanywa na Mheshimiwa Rais Wetu mpendwa uunaoonyesha imani kubwa juu yako kuwa utarekebisha na kutatua changamoto mbalimbali zinazowakabili wafanyabiashara nchini ambao kwa kiasi kikubwa ndiyo wanaounda kundi linaloongoza katika ukusanyaji wa mapato ya nchini.
Kwa msingi huo tunaamini kwamba utasikiliza malalamiko na kilio chetu kuhusu baadhi ya watumishi ndani ya Mamlaka (TRA) ambao wamekuwa mwiba kwa wafanyabiashara kwa kubambikizia makadirio makubwa ya kodi yasiyozingatia sheria za nchi hivyo kutengeneza mianya ya kupokea rushwa kutoka kwa wafanyabiashara.
Mheshimiwa Kamishna,
Tunaomba kuchukua nafasi kuwasilisha kwako malalamiko yetu kuhusu mtumishi wa TRA Arusha Bw.Loshie Laizer wa kitengo cha uchunguzi/upelelezi kuwa amekuwa na tabia ya kuwanyanyasa wafanyabiashara hasa wakubwa kwa kubambikia makadirio ya malimbikizo ya kodi baada “kuchungulia” akaunti zao binafsi katika mabenki na pia akaunti za biashara wanazomiliki.
Mtumishi huyo amekuwa akitumia njia za vitisho dhidi ya wafanyabiashara kuwa endapo hata kubaliana na matokeo ya uchunguzi “feki” kuwa anadaiwa malimbikizo makubwa ya kodi basi ataagiza mamlaka nyingine za kiserikali kumfungulia mfanyabiashara husika kesi ya uhujumu uchumi au ya utakasishaji fedha (ML).
Kutokana na vitisho hivyo wafanyabiashara wengi wameingia katika mtego wa mtumishi huyo wa kutoa chochote (rushwa) ili kuepuka usumbufu na pia kuogopa kufunguliwa kesi hasa katika kipindi cha miaka mitano iliyopita.
Mheshimiwa Kamishna,
Taarifa zinaonyesha kuwa mtumishi huyo amekuwa akifanya kazi katika eneo moja (Mkoa wa Arusha) kwa zaidi ya miaka 15 jambao ambalo si la kawaida kwa watumishi umma hivyo kuzua maswali yasiyo na majibu kwa wadau na wafanyabiashara.Kuna madai kuwa kila mamlaka ilipojaribu kumhamisha mtumishi huyo alitumia njia mbalimbali kuzuia umahisho huo.
Kuna madai kuwa mtumishi huyo ana ukwasi mkubwa kwa kumiliki mali kadhaa kama nyummba za kupanga mashamba na hisa katika baadhi ya biashara kubwa mjini Arusha ikiwemo shule ya LOAMO iliyopo eneo la Olorien katika Jiji la Arusha ambayo ni moja katika ya shule kubwa mjini Arusha.
Mheshimiwa Kamishna tunaomba uchunguzi huru na wa haki ufanyike dhidi ya mtumishi huyo ili kuwaondoelea adha,manyanyaso, na hofu wanayopata wafanyabiashara wa Mkoa wa Arusha na tunaamini kuwa kilio chetu kitafanyiwa kazi.
Tunatangauliza shukrani zetu.
Omar SS.
Kwa niaba ya wafanyabiashara
Arusha.