Barua ya wazi kwa Dkt. David Mnzava the Medical council of Tanganyika "Secretary and registrar"(The MCT registrar and secretary of the board)

Ni ujinga mkubwa kumfanya mtu aliyesoma Chuo Kikuu masomo ya utabibu sawa na aliyemaliza Form Six. Hasa katika nchi ambayo ina upungufu mkubwa wa watu wenye ufahamu wowote wa mambo ya afya. Wenye mamlaka walitakiwa kuangalia namna ambavyo elimu yao ingeweza kutumika kuwasaidia wananchi na kuwapa credit kwa ujuzi walio nao kwa wale wanaotaka u MD.

Huku kuvimbishiana vifua hakuna faida yeyote kwetu.

Amandla...
 
Ufafanuzi:; Hii kozi kwa lugha ya kigeni ni Bsc in nini??
 
Ufafanuzi:; Hii kozi kwa lugha ya kigeni ni Bsc in nini??
Inaitwa Bachelor of science in Clinical medicine and bachelor of surgery Au Bachelor of science in Clinical medicine ,surgery and Community health
 
Mimi sio MD
 
Uko sahihi kabisa. Na ukweli huko wanakoishi watanzania wengi mtu yeyote anaewatibu watamuita Daktari. Hawajali hayo makaratasi yameandikwa nini bali tiba wanayopata. Badala ya kuwafungia wengine wanatakiwa kufanya jitihada nao wapate nafasi ya kuwasaidia huu mzigo ambao ni mkubwa mno.

Kwangu mimi mtu anayejivunia zaidi title yake kuliko ujuzi wake anakuwa na matatizo. Kila mtu ni muhimu katika nafasi yake na anastahili heshima.

Umefanya kitu kizuri sana kuwasemea. Hawa wa GPA 3.0 wasikuvunje moyo.

Amandla...
 
Wewe fundi mchundo

There will never be a mchundo students t be a doctor or graduate recognized

Hatukusoma waje kumangamanga Kwa mbele
 
Sawa kabisa mkuu unajua vijana wengi wanaoibukia siku hizi ndo huwa na mihemko mingi bila kujali maslahi sahihi ya Mtu ambaye tunaenda kumtumikia ambaye ni mgonjwa...Wanasahau hata hiyo course ya MD ilianza Rasmi kutolewa Mwaka 1991 ambapo kabla ya hpo ilitolewa UDSM kuanzia miaka ya 63's nayo ilikuwa ni course ya uganga na sio Pure MD kwahiyo na baadae ilihamishiwa rasmi Kuwa facult of Medicine katika MUHAS mwkaa 1996 ambayo kiukweli miaka ni kama 30 ambayo ni michache sana , kwahyo bado sisi ni wachanga sana kwenye Mambo na maswala ya Afya tusikurupuke kuzuia kwa miehemko ya kisiasa kwa sababu ya kuhofia kwamba nafasi fulani itakuwaje.... Mbona kwa wenzetu wanafanya na wanatibu wagonjwa na wanashirikiana vizuri tu...
Nilimsikia kiongozi mmoja wa MAT (chama cha shirikisho la Madaktari) Akisema wakiruhusu hilo kutokea itasababisha watu wengi kuacha kusoma MD na kusoma Utabibu na ndo hofu yao kubwa....
 
Wewe fundi mchundo

There will never be a mchundo students t be a doctor or graduate recognized

Hatukusoma waje kumangamanga Kwa mbele
Kwani umeelewa hoja au upo kuipinga bila kujua its contents
 
Wewe fundi mchundo

There will never be a mchundo students t be a doctor or graduate recognized

Hatukusoma waje kumangamanga Kwa mbele
Sasa kwa hicho kiingereza ndio unaringia udaktari wako?

Amandla...
 
Tatizo liko wapi kama watakuwa wanatoa tiba sahihi? Kwa wenzetu kuna chiropractors ambao sio M.D lakini wanatambuliwa kama madaktari wakipata usajili.

India kuna wale wanaosomea Ayurvedic medicine na wanapata degree za BAMS na asilimia kubwa ya wahindi wanawaamini kuliko madaktari wa M.D.

Tunachokitafuta ni tiba na maisha bora kwa wananchi. Tunachotakiwa ni kuhakikisha tu wote hao wanaopata hiyo dhamana hawadhuru wagonjwa wao, full stop.

Amandla...
 
Yaani umeongea kitu kilichopo moyoni mwangu sana mkuu ugonjwa hautambui vyeo vyetu ila unatambua ujuzi wetu

May God bless you!
 
Yaani umeongea kitu kilichopo moyoni mwangu sana mkuu ugonjwa hautambui vyeo vyetu ila unatambua ujuzi wetu

May God bless you!
Kuna "mainjinia" waliosomea Dar Tech enzi zile ambao walifanya kazi ya kutukuka ya uinjinia. Hao ndio walioibeba PWD na wanastahili kuenziwa. Hivi karibuni kulikuwa na ugomvi mkubwa kati ya wahitimu wa DIT na wale wa UDSM ambapo wa UDSM hawakutaka wa DIT watambuliwe kama wahandisi wakati ukweli huko kwenye kazi tofauti yao haionekani.
Hii fixation na titles badala ya ujuzi ndio inafanya watu wengine watafute Ph.D kwa udi na uvumba wakiamini kuwa akiipata ndio itathibitisha weledi wake kumbe sio.

Amandla...
 
Ukweli mtupu
 
Unaongelea jambo la msingi Kwa Taifa natamani mamlaka husika zingekuwepo.
Naomba unisaidie kunipa ufafanuzi au tofauti ya hizo course mbili 1.Bachelor degree in medical doctor
2.Bachelor degree in dental surgery
 
Unaongelea jambo la msingi Kwa Taifa natamani mamlaka husika zingekuwepo.
Naomba unisaidie kunipa ufafanuzi au tofauti ya hizo course mbili 1.Bachelor degree in medical doctor
2.Bachelor degree in dental surgery
Sijaelewa ufafanuzi wa hizo kozi juu au ufafanuzi wa kozi ulizoandika...
Anyway..
Doctor of medicine (MD) .{au kama ulivyoandika Bachelor degree in medical doctor} Ni kozi inayoandaa wataalamu wa Afya kufanya Matibabu kwa wagonjwa ikiwemo kufanya upasuaji wa dharula na unaoruhusiwa kulingana naa elimu yake kisheria
Na Doctor of dental surgery (DDS) {au kama ulivyoandika Bachelor degree in Dental surgery} Ni kozi imayoandaa wataalamu wa Afya kufanya matibabu ya kinywa na Menu ikiwemo kufanya shughuli za upasuaji wote wa Kinywa na meno....

Doctor of Medicine huitwa Medical Doctor au medical officer while Doctor of dental surgery huitwa Dental Surgeon
Wote wanatambukika kisheria kama Madaktari kamili...
Nafikiri nimejaribu kukudadavulia
Thanks
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…