Jackob, jOKA, mZIZI Mkavu mnatia kichefuchefu. Hata kama mmekunywa maji ya bendera ya kijani acheni wazalendo na wapenda haki waongee. Kama mmetumwa semeni. Hivi mnafurahia wenzetu kule Shinyanga, Segerea wanavyoumizwa kwa uzandiki wa Chama chenu cha majambazi CCM? Nchi hii inaharibiwa na CCM na JK lazima nchi imfie. Acha CCM wafanye wanayo yafanya lakini iko siku Mungu mpenda haki atawaanika juani na haki ya kweli kwa wapenda haki itapatikana. Tunawaombea wana CCM maisha marefu ili wapenda haki tutakapo inuliwa wapate kushuhudia. Marehemu Horace Kolimba alisema kuwa CCM imekosa mwelekeo, hakukusea. Matokeo yake tunayaona sasa. Machafuko ya nchi za kiafrika hasa baada ya chaguzi yanasababishwa na chama tawala kwa kung'ang'ania madaraka ili hali wananchi wameshachoshwa. Kibaki, Mugabe walilazimisha kujitangaza washindi wakati nguvu ya umma haiwataki. Kikwete akifuata mkondo atalaaniwa milele.Napenda kuwaambia kuwa, watanzania wa leo siyo wale wa miaka iliyopita, si watanzania wa kudanganyika kirahisi. Kwa mwenendo wa kura unavooenda kama una akili timamu huwezi kusema Kikwete atashinda kihalali, hilo hata mtoto mdogo analifahamu. Haiwezekani Jimbo ambalo Mbunge wa upinzani kamshinda wa CCM kwa zaidi ya 40% halafu jimbo hilo hilo Kikwete ashinde kwa zaidi ya 70% . CCM watachakachua kura, watachakachua roho zetu lakini Mungu wa kweli iko siku atasikia kilio cha watanzania na mapinduzi ya kweli yatapatikana. Tunaomba CCM wasitumie maiti za watanzania kama daraja la kupandia kupata madaraka kwa tamaa zao. Iko siku roho zinazochakachuliwa sasa hivi zitaamka na haki itapatikana. Kwa kinachoonekana sasa hivi majimboni ni uvunjaji wa haki za binadamu na vyote hivi vinaongozwa na CCM. JAMANI CCM kama wananchi hawawataki MSILAZIMISHE. Na viongozi mnaoingia madarakani kwa kuchakachua matokeo hamtakuja kupata amani moyoni kwako kwa dhambi uliyofanya. Kama mwananchi unayetaka kumuongoza hakutaki....na bado unang'ang'ania unataka mwisho wa siku uongozi maiti? Iko siku nguvu ya umma itakapoamua, mtalia na kusaga meno. Ni hayo tu