Pre GE2025 Barua ya wazi kwa mheshimiwa ex mayor wa ubungo na mwenyekiti wa chadema kanda ya Pwani

Pre GE2025 Barua ya wazi kwa mheshimiwa ex mayor wa ubungo na mwenyekiti wa chadema kanda ya Pwani

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

KING ASSENGA

JF-Expert Member
Joined
Oct 8, 2016
Posts
928
Reaction score
1,478
Salaam na heshima kwako mheshimiwa Boniface Jacobo Mayor mstaafu na Mwenyekiti wa Kanda ya pwani chama Cha demokrasia na maendeleo CHADEMA.

Kiongozi kabla ya kusema niliyowiwa kuyasema naomba kutambua unao washauri wengi sana wenye vyeo na nafasi kubwa kuliko Mimi ila naomba unipe dakika chache tu kusoma barua hii.

Kiongozi kabla ya uchaguzi mkuu wa chama ulikuwa mtu muhimu sana katika chama na nikiri huo umuhimu wako upo , pengo lako tunaliona ndio maana nimewiwa kuandika barua hii ya wazi kwako .

Kiongozi Kuna matukio mengi sana yametokea nchini ambayo sio kawaida tukose tweet mbili tatu kuyahusu na kuna matukio mengi sana ya kichama ambayo hatukuoni wala kuona mchango wako kwa sasa

Kiongozi naomba nikukumbushe tukio la wewe kurudisha fomu ya kugombea uenyekiti Kanda ya pwani. Wanachama wengi tulikusindikiza kurudisha fomu wengine hata hutufahamu na usisahau hatukukusindikiza kwa sababu ya ukaribu wako na Mbowe tambua hili Kuna wengi tu walipendezwa na Lissu wakati wa uchaguzi na walikuwa wengi tu huenda zaidi ya wafuasi wa mbowe waliokusindikiza . Hivyo tambua tunaokuamini hatukuamini kwasababu yoyote zaidi ya kuwa mwanachama wa chadema na mwenye uwezo mkubwa katika harakati za chama .

Tunatambua umeumia sana kutokana na demokrasia ilivyoamua ila fikiria vizuri sidhani kama mheshimiwa Mbowe anafurahia ukimya wako . Tafadhali ni muda wa kurudi sasa. Tusamehe tuliotoa maneno makali wakati wa uchaguzi wa chama nikiwemo umeniblock kabisa. Uchaguzi umekwisha . Ushapumzika vya kutosha . Pengo lako linakusubiri ulizibe Tafadhali lizibe tusonge mbele.

Nisikuchoshe kwa barua ndefu. Tafadhali rudi kama awali maisha yaendelee

Mwanachama mtiifu wa CHADEMA
Na mwanaharakati wa haki
Assenga

-yervbf.jpg
Kupata taarifa na matukio yanayojiri kuelekea uchaguzi mkuu kwa kila mkoa ingia hapa: Special Thread: Mijadala na Matukio ya Uchaguzi Mikoa yote Tanzania Bara na Zanzibar kuelekea Uchaguzi Mkuu 2025
 
Haya maumivu ni wazi hawa watu walikuwa wamegeuza chama shamba lao la upigaji. Kushindwa kwenye uchaguzi wa kidemokrasia pekee hakuwezi kubeba maumivu makali namna hii.
Anashangaza kwa kweli. Ni ushahidi hawa watu waligeuza chama SACCOS au kuna kitu walipokea. Unawezaje kuwa na chuki hivi. Hata humu JF kuna watu wamekuwa na chuki na sisi tuliomuunga mkono Lissu. Yaani anaweza kukukuta kwenye uzi tofauti tu anaanza harassment
 
Anashangaza kwa kweli. Ni ushahidi hawa watu waligeuza chama SACCOS au kuna kitu walipokea. Unawezaje kuwa na chuki hivi. Hata humu JF kuna watu wamekuwa na chuki na sisi tuliomuunga mkono Lissu. Yaani anaweza kukukuta kwenye uzi tofauti tu anaanza harassment
Wapo walioshauri baada ya Uchaguzi kuwe na Maridhiano ya ndani lakini walipuuzwa
 
Salaam na heshima kwako mheshimiwa Boniface Jacobo Mayor mstaafu na Mwenyekiti wa Kanda ya pwani chama Cha demokrasia na maendeleo CHADEMA.

Kiongozi kabla ya kusema niliyowiwa kuyasema naomba kutambua unao washauri wengi sana wenye vyeo na nafasi kubwa kuliko Mimi ila naomba unipe dakika chache tu kusoma barua hii.

Kiongozi kabla ya uchaguzi mkuu wa chama ulikuwa mtu muhimu sana katika chama na nikiri huo umuhimu wako upo , pengo lako tunaliona ndio maana nimewiwa kuandika barua hii ya wazi kwako .

Kiongozi Kuna matukio mengi sana yametokea nchini ambayo sio kawaida tukose tweet mbili tatu kuyahusu na kuna matukio mengi sana ya kichama ambayo hatukuoni wala kuona mchango wako kwa sasa

Kiongozi naomba nikukumbushe tukio la wewe kurudisha fomu ya kugombea uenyekiti Kanda ya pwani. Wanachama wengi tulikusindikiza kurudisha fomu wengine hata hutufahamu na usisahau hatukukusindikiza kwa sababu ya ukaribu wako na Mbowe tambua hili Kuna wengi tu walipendezwa na Lissu wakati wa uchaguzi na walikuwa wengi tu huenda zaidi ya wafuasi wa mbowe waliokusindikiza . Hivyo tambua tunaokuamini hatukuamini kwasababu yoyote zaidi ya kuwa mwanachama wa chadema na mwenye uwezo mkubwa katika harakati za chama .

Tunatambua umeumia sana kutokana na demokrasia ilivyoamua ila fikiria vizuri sidhani kama mheshimiwa Mbowe anafurahia ukimya wako . Tafadhali ni muda wa kurudi sasa. Tusamehe tuliotoa maneno makali wakati wa uchaguzi wa chama nikiwemo umeniblock kabisa. Uchaguzi umekwisha . Ushapumzika vya kutosha . Pengo lako linakusubiri ulizibe Tafadhali lizibe tusonge mbele.

Nisikuchoshe kwa barua ndefu. Tafadhali rudi kama awali maisha yaendelee

Mwanachama mtiifu wa CHADEMA
Na mwanaharakati wa haki
Assenga

Snitch anasema anataka ajivue uenyekiti wa kanda ya Pwani, kwenda mwana kwenda, tokomea mwana kutokomea
 
Bado sijapata maana kamili ya malidhoano kwenye siasa huwa wana kubaliana nini? Maana kama ni biashara tunajua ni win win situation. Sasa huku kwenye siasa, naomba msaada zaidi.
Umeelewa mada?
 
Haya maumivu ni wazi hawa watu walikuwa wamegeuza chama shamba lao la upigaji. Kushindwa kwenye uchaguzi wa kidemokrasia pekee hakuwezi kubeba maumivu makali namna hii.
Walipania sana ushindi ni Hilo tu. Matokeo yaliwashangaza. Zaidi ni kauli za kwenye kampeni
 
Siasa chafu alizofanya Lisu na team yake dhidi ya team Mbowe yale majeraha kupona sio rahisi

Kuna vidonda vya kawaida na donda ndugu

Bon yai alichofanya ni sahihi ku block kabisa simu nk za wahuni

Tuwe fair Mbowe alichofanyiwa na Lisu sicho kabisaa
 
Siasa chafu alizofanya Lisu na team yake dhidi ya team Mbowe yale majeraha kupona sio rahisi

Kuna vidonda vya kawaida na donda ndugu dugu

Bon yai alichofanya ni sahihi ku block kabisa simu nk za wahuni

Tuwe fair Mbowe alichofanyiwa na Lisu sicho kabisaa
Kugombea haikuwa kosa . Lissu aliongea ukweli tu . Ubaya wake Kuna yakunyamaza angetakiwa anyamaze hakufanya hivyo
 
Back
Top Bottom