Barua ya wazi kwa Waziri January Makamba; Tuliamini utaleta mapinduzi kwenye sekta ya NISHATI, lakini matarajio yetu yanapotea

Barua ya wazi kwa Waziri January Makamba; Tuliamini utaleta mapinduzi kwenye sekta ya NISHATI, lakini matarajio yetu yanapotea

Kayombo Tips

JF-Expert Member
Joined
Jun 19, 2020
Posts
461
Reaction score
574
Wakati tunapokea taarifa za uteuzi wa Uwaziri wako bwana January Makamba, watu wengi tuliamini kuwa wewe ndiye utakaye leta mageuzi makubwa sana kwenye Wizara yako. Lakini nasikitika kuona kuwa matarajio tuliyo kuwa nayo kwako yamepotea.

Ulipoteuliwa tu na kuapishwa ulionesha mwelekeo kwamba changamoto za nishati zitapungua sana badala yake changamoto hizo zimeongezeka zaidi.

Umeme umekuwa una katika mara kwa mara, bei ya gesi imezidi kuongezeka zaidi. Licha ya ahadi zako nyingi ulizotoa mara ulipoteuliwa kuwa Waziri wa Nishati ila hakuna hata ahadi moja uliyotekeleza. Zaidi sasa hivi umekuwa mtu wa kuja na matamko yanayopingana na ahadi zako ulizotoa.

Sasa hivi ukiulizwa kwanini umeme unakatika mara kwa mara unajibu kuwa tatizo ni mitambo ya zamani haikufanyiwa matengenezo kwa muda mrefu sana. Mara unajibu kuwa matatizo ya umeme kukatikakatika yataendelea kuwepo. Sasa kwa kauli zako hizi huoni kama unapata sifa ya kuwa kiongozi uliyeshindwa.

Sisi Wananchi hatutaki kusikia maneno ya kuwa umeme utaendelea kukatika mara kwa mara, tunataka kusikia majibu ya namna utakavyo ondoa tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Ulionekana kama kijana ambaye tulikuwa tunatazamia siku moja utakuwa Mkuu wa Nchi ila umeonesha kushindwa kiuongozi. Tabia yako ya kubadilisha badilisha kauli ahadi zako inaonesha kabisa hufai kuwa Mkuu Wa Nchi kwa siku za mbeleni.

Wananchi huu ni muda wa kuwa tazama kwa umakini viongozi vijana waliopewa dhamana ya kiuongozi kuona wanavyotusaliti ili kama siku moja wanatamani kushika nafasi ya juu tujue mapema hawatufai na kwamba ahadi wanazotoa siyo sahihi.
 
Wakati tunapokea taarifa za uteuzi wa uwaziri wako bwana January Makamba, watu wengi tuliamini kuwa wewe ndiye utakaye leta mageuzi makubwa sana kwenye wizara yako. Lakini nasikitika kuona kuwa matarajio tuliyo kuwa nayo kwako yamepotea.
Ulipoteuliwa tu na kuapishwa ulionesha mwelekeo kwamba changamoto za nishati zitapungua sana badala yake changamoto hizo zimeongezeka
Sioni barua naona maelezo tu!

Umeme umekuwa kero, yaani nyama nazoweka kwenye fridge mara kwa mara zinaharibika inabidi nitupe

Watakuja watakwambia
1. Jina
2. Eneo
3. Namba ya simu.
4. Tatizo!
 
Sioni barua naona maelezo tu!

Umeme umekuwa kero, yaani nyama nazoweka kwenye fridge mara kwa mara zinaharibika inabidi nitupe

Watakuja watakwambia
1. Jina
2. Eneo
3. Namba ya simu.
4. Tatizo!
Pole sana mkuu kwa changamoto hiyo.
 
January ni failure
Sana tu, anabadilika badilika sana. Nilipoona ameteuliwa kuwa Waziri Wa Nishati nilijua sasa tatizo la nishati limepata mwarobaini ila naona ndiyo naona tatizo limeota sugu.
 
Wakati tunapokea taarifa za uteuzi wa Uwaziri wako bwana January Makamba, watu wengi tuliamini kuwa wewe ndiye utakaye leta mageuzi makubwa sana kwenye Wizara yako. Lakini nasikitika kuona kuwa matarajio tuliyo kuwa nayo kwako yamepotea.

S U K U M A G A N G
 
S U K U M A G A N G
Sukumagang yupi mkuu? Mtu akitoa mawazo yake tofauti huyo ni Sukumagang? Siyo watu wote wanao onesha kutokubaliana na jinsi serikali ya awamu ya sita inavyoendeshwa ni Sukumagang.
 
Uwaziri wa vimemo upelekea kua uwaziri wa michongo...
Mie kero yangu kubwa ni Rushwa kuota mizizi katika shirika la TANESCO...
Leo huwezi amini kuna watu walilipia tokea Mwaka Jana October to this date hawajaunganishiwa umeme kisa eti Mita za Luku hakuna... Waziri kapoaaaaaa, bora ata Naibu wake Mh Byabato angalau anaviziara uchwara... Mh Rais apa km alishauriwa au alimpa uwaziri kumfurahisha mzee Makamba basi ajue kua amepigwa na kitu kizito kichwani.. Aiba ya uongozi wa Mzee Makamba na Makamba Junior ni vitu viwili tofauti... Huyu Makamba dogo kafail pakubwa Sana,amekosa mamlaka ya usimamizi, amekosa mvuto wakiuongozi kwenye Sekta nyeti km hii... Michongo Michongo sio dili
 
Wakati tunapokea taarifa za uteuzi wa Uwaziri wako bwana January Makamba, watu wengi tuliamini kuwa wewe ndiye utakaye leta mageuzi makubwa sana kwenye Wizara yako. Lakini nasikitika kuona kuwa matarajio tuliyo kuwa nayo kwako yamepotea.

Ulipoteuliwa tu na kuapishwa ulionesha mwelekeo kwamba changamoto za nishati zitapungua sana badala yake changamoto hizo zimeongezeka zaidi.

Umeme umekuwa una katika mara kwa mara, bei ya gesi imezidi kuongezeka zaidi. Licha ya ahadi zako nyingi ulizotoa mara ulipoteuliwa kuwa Waziri wa Nishati ila hakuna hata ahadi moja uliyotekeleza. Zaidi sasa hivi umekuwa mtu wa kuja na matamko yanayopingana na ahadi zako ulizotoa.

Sasa hivi ukiulizwa kwanini umeme unakatika mara kwa mara unajibu kuwa tatizo ni mitambo ya zamani haikufanyiwa matengenezo kwa muda mrefu sana. Mara unajibu kuwa matatizo ya umeme kukatikakatika yataendelea kuwepo. Sasa kwa kauli zako hizi huoni kama unapata sifa ya kuwa kiongozi uliyeshindwa.

Sisi Wananchi hatutaki kusikia maneno ya kuwa umeme utaendelea kukatika mara kwa mara, tunataka kusikia majibu ya namna utakavyo ondoa tatizo la kukatika kwa umeme mara kwa mara.

Ulionekana kama kijana ambaye tulikuwa tunatazamia siku moja utakuwa Mkuu wa Nchi ila umeonesha kushindwa kiuongozi. Tabia yako ya kubadilisha badilisha kauli ahadi zako inaonesha kabisa hufai kuwa Mkuu Wa Nchi kwa siku za mbeleni.

Wananchi huu ni muda wa kuwa tazama kwa umakini viongozi vijana waliopewa dhamana ya kiuongozi kuona wanavyotusaliti ili kama siku moja wanatamani kushika nafasi ya juu tujue mapema hawatufai na kwamba ahadi wanazotoa siyo sahihi.
Akifanya mchezo anaweza kuja kuwa kama Mkuu wa Mkoa Mkuu aliyekuwa anaita Mkoa wangu aliyetamka vitu kibao, bila matokeo. Lakini tumuombee isiwe matatizo ni maslahi ya watu fulani tu ambao wananufaika na kupanda kwa bei holela. Ila Watanzania ni wavumilivu aisee, yaani hadi leo wako kimyaaa
 
Tatizo kubwa la hii nchi ni mfumo
Sana tu, anabadilika badilika sana. Nilipoona ameteuliwa kuwa Waziri Wa Nishati nilijua sasa tatizo la nishati limepata mwarobaini ila naona ndiyo naona tatizo limeota sugu.
 
Mkuu kabla ya kumbatiza jina huyo ukweli ni kuwa umeme ni tatizo, hapa nilipo ushakatwa. Umeme haujifichi ukiwa vizuri unaonekana ukiwa hovyo unaonekana
Sijui labda anakoishi huyo jamaa umeme upo masaa yote
 
Aiseee Mimi pia nilikuwa ni mmoja wao nikijua makamba anafaa kuwa Raisi kumbe nilijidanganya
 
Uwaziri wa vimemo upelekea kua uwaziri wa michongo...
Mie kero yangu kubwa ni Rushwa kuota mizizi katika shirika la TANESCO...
Leo huwezi amini kuna watu walilipia tokea Mwaka Jana October to this date hawajaunganishiwa umeme kisa eti Mita za Luku hakuna... Waziri kapoaaaaaa, bora ata Naibu wake Mh Byabato angalau anaviziara uchwara... Mh Rais apa km alishauriwa au alimpa uwaziri kumfurahisha mzee Makamba basi ajue kua amepigwa na kitu kizito kichwani.. Aiba ya uongozi wa Mzee Makamba na Makamba Junior ni vitu viwili tofauti... Huyu Makamba dogo kafail pakubwa Sana,amekosa mamlaka ya usimamizi, amekosa mvuto wakiuongozi kwenye Sekta nyeti km hii... Michongo Michongo sio dili
Mama amtoe tu huyu Waziri Wa Nishati. Hali ya kukatika kwa umeme kila siku halafu Waziri mwenye dhamana anakuja anatoa majibu mepesi haivumiliki. Haiwezekani Waziri kabisa anatoka kwenye vyombo vya habari anasema tatizo la umeme kukatikakatika lita endelea kuwepo. Ina maana anasema kuwa yeye ameshindwa kuongoza wizara yake.
 
Back
Top Bottom