BASATA nao wamshughulikia Gigy, yamfungia kujishughulisha na sanaa kwa miezi sita na faini ya milioni 1

BASATA nao wamshughulikia Gigy, yamfungia kujishughulisha na sanaa kwa miezi sita na faini ya milioni 1

Replica

JF-Expert Member
Joined
Aug 28, 2017
Posts
1,681
Reaction score
8,887
Baada ya mamlaka ya mawasiliano Tanzania(TCRA) kukifungia kituo cha televisheni cha Wasafi kwa kurusha maudhui ya utupu yanayomuonyesha msanii Gift Stanford Jushua maarufu kama Gigy Money, nalo baraza la sanaa Tanzania(BASATA) limeibuka na kumlamba adhabu ya miezi sita msanii huyo kutojihusisha na sanaa ndani na nje ya nchi.

Pia BASATA imemtaka msanii huyo kulipa faini ya milioni 1. Sehemu ya taarifa yake imesema Gigy alishaitwa na baraza na kuonywa mara kadhaa na aliahidi kutorudia tena.

PIA, SOMA => RUNGU: TCRA imeitaka Wasafi TV kusitisha matangazo kwa Miezi Sita (6) kuanzia leo kwa kurusha Maudhui ya utupu

Gigy 1.jpg
Gigy 2.jpg
 
It was about time. Yule sio msanii bali ni “kahaba” aliyekubuhu. Walidhani CCM itawalinda na kuwatetea baada ya kampeni kuisha?

Sasa awe free kwenda kuuza kwenye macasino maana kule ni ruksa kutembeza utupu bila vikwazo.
 
Diamond anguko lake liko karibu. Ni kosa sana kufanya kazi bila professionalism.

Ujanja ujanja huwa haudumu sana kwenye kazi kama hizi.
Unforgetable
Huwezi kujifunza bila kuanguka, ndiyo anajifunza vizuri, tusipige vita sana uwekezaji wake maana unalipa kodi na kuwalisha baadhi ya watanzania, tusiweke chuki sana kwenye uwekezaji wake bali kumuonyesha anapoanguka
 
Diamond anguko lake liko karibu. Ni kosa sana kufanya kazi bila professionalism.

Ujanja ujanja huwa haudumu sana kwenye kazi kama hizi.
Unforgetable
Hivi hii ilikuwa live show sio? Sasa Gigy kapanda jukwaani ghafla kavua gauni hata ingekuwa TBC wangeweza kukata matangazo ghafla au huyo Gigy aliendelea kuimba uchi show nzima?
 
Hivi hii ilikuwa live show sio? Sasa Gigy kapanda jukwaani ghafla kavua gauni hata ingekuwa TBC wangeweza kukata matangazo ghafla au huyo Gigy aliendelea kuimba uchi show nzima?
Wangekata..mbona kwenye vyombo vya nje vinavyoungana na media za bongo huwa kuna live censorship?..Lissu alikuwa akianza kutema tu cheche wanakata.
 
Diamond anguko lake liko karibu. Ni kosa sana kufanya kazi bila professionalism.

Ujanja ujanja huwa haudumu sana kwenye kazi kama hizi.
Unforgetable
Diamond Yeye ni Level nyingine.angeachana na hawa wasichana wa Uwanja wa Fisi akachukue level zake kama kina Mimi Mars na Maua Sama. Huyu Gift hata akiongea ni Utadhani ni Chokoraa.
 
Wangekata..mbona kwenye vyombo vya nje vinavyoungana na media za bongo huwa kuna live censorship?..Lissu alikuwa akianza kutema tu cheche wanakata.
Vyombo vya nje ni rahisi kama kuzima Tv
 
Vyombo vya nje ni rahisi kama kuzima Tv
Hata hawa wanaweza,si wanazima tu hiyo live na kuweka content nyingine mfano matangazo ya biashara n.k..mbona easy sana

Sema tu labda hawakujua kuwa itakuja kuwa hivi,ila wangejua wangekata tu fasta hiyo live broadcast na kurudi baada ya huyo gigy kumaliza kunengua hapo stejini
 
Back
Top Bottom