Bashe aachie Uwaziri

Bashe aachie Uwaziri

Mtumishiwetu

Senior Member
Joined
Jul 13, 2022
Posts
196
Reaction score
346
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuomba msaada wa mawazo na ushauri wa namna ya kuendesha Wizara ya Kilimo.

"Ukiwa na muda tafadhali nipe mawazo yako kuhusu Kilimo na usalama wa Chakula kwa nchi za Afrika haswa hapa nyumbani kwetu Tanzania Nini kifanyike? Nini kiboreshwe?" amesema Bashe

Maswali ya kujiuliza Bunge la Bajeti limemalizika mwezi Juni. je mambo yote yaliyoshauriwa na wabunge kuhusu Kilimo ameshayamaliza kuyafanyia kazi.?

Je anamuonesha Mhe. Rais kuwa alimteua mtu ambaye hajui cha kufanya Wizara ya Kilimo hadi aanze kuokoteza mawazo kwenye mitandao? na je anaamini wakulima wako Instagramu?

Au ndio ile kauli ya mfa maji haishi kutapata baada ya usimamizi mbovu wa wizara na kusababisha nchi kukumbwa na baa la njaa kutokana na usimamizi mbovu kuruhusu wananchi wa mataifa mengine kuingia vijijini mashambani na kununua mazao moja kwa moja hadi Japan kuamua kuingia kati kusaidia Tanzania fedha kwa ajili ya ununuzi wa chakula?

Mimi nadhani ni muda sasa kwa Waziri Bashe kujiuzulu ili kumpa nafasi Mheshimiwa Rais kutafuta mtu mwingine atakayeweza kusimamia sekta ya kilimo na tuondokane na baa la njaa alilolisababisha Bashe
 

Attachments

  • 20220910_152605.jpg
    20220910_152605.jpg
    112.2 KB · Views: 8
Nimesoma maelezo yako. Nampongeza Sana waziri Bashe Kwa uamuzi huo, naweza kusema amechelewa. Hapa jf Watu walishatahadharisha kuhusu usalama Wa chakula lakini wenye mamlaka hawakujali, kama Leo ameona kuna haja ya kushauriwa basi ni Jambo jema Sana.
Sikubaliani na aya yako ya mwisho, udhoefu yanaonyesha mizigo ni wengi.
 
Kipindi yupo magufuli wafanyabiashara walizuiliwa kupeleka mazao nje ya nchi nazani unakumbuka kilichotokea
 
"Ukiwa na muda tafadhali nipe mawazo yako kuhusu Kilimo na usalama wa Chakula kwa nchi za Afrika haswa hapa nyumbani kwetu Tanzania Nini kifanyike? Nini kiboreshwe?" amesema Bashe
Ni wazo zuri ila swali la msingi ni labda amewatumia kwa kiasi gani washauri wake walioko pale wizarani!!
 
Ni wazo zuri ila swali la msingi ni labda amewatumia kwa kiasi gani washauri wake walioko pale wizarani!!
Kilimo ni zaidi ya kutoa mbolea za ruzuku, sasa wao kwa sasa ni sifa tu kuwa tumetoa mbolea kwa bei nafuu, wakati, kilimo ni zaidi ya mbolea, haya sasa umetoa mbolea hata bure, mvua hakuna, na hakuna mikakati ya kilimo cha umwagiliaji, hayo mavuno yanatoka wapi?
Uuzaji nao ni shida, kwenye bei
 
Yupo sawa kabisa, kongolee Bashe.
Ila mods hiyo heading mliyoweka daah
 
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuomba msaada wa mawazo na ushauri wa namna ya kuendesha Wizara ya Kilimo.

"Ukiwa na muda tafadhali nipe mawazo yako kuhusu Kilimo na usalama wa Chakula kwa nchi za Afrika haswa hapa nyumbani kwetu Tanzania Nini kifanyike? Nini kiboreshwe?" amesema Bashe

Maswali ya kujiuliza Bunge la Bajeti limemalizika mwezi Juni. je mambo yote yaliyoshauriwa na wabunge kuhusu Kilimo ameshayamaliza kuyafanyia kazi.?

Je anamuonesha Mhe. Rais kuwa alimteua mtu ambaye hajui cha kufanya Wizara ya Kilimo hadi aanze kuokoteza mawazo kwenye mitandao? na je anaamini wakulima wako Instagramu?

Au ndio ile kauli ya mfa maji haishi kutapata baada ya usimamizi mbovu wa wizara na kusababisha nchi kukumbwa na baa la njaa kutokana na usimamizi mbovu kuruhusu wananchi wa mataifa mengine kuingia vijijini mashambani na kununua mazao moja kwa moja hadi Japan kuamua kuingia kati kusaidia Tanzania fedha kwa ajili ya ununuzi wa chakula?

Mimi nadhani ni muda sasa kwa Waziri Bashe kujiuzulu ili kumpa nafasi Mheshimiwa Rais kutafuta mtu mwingine atakayeweza kusimamia sekta ya kilimo na tuondokane na baa la njaa alilolisababisha Bashe
Waziri wa Kilimo, Hussein Bashe kwa mara ya kwanza amejitokeza hadharani kuomba msaada wa mawazo na ushauri wa namna ya kuendesha Wizara ya Kilimo.

"Ukiwa na muda tafadhali nipe mawazo yako kuhusu Kilimo na usalama wa Chakula kwa nchi za Afrika haswa hapa nyumbani kwetu Tanzania Nini kifanyike? Nini kiboreshwe?" amesema Bashe

Maswali ya kujiuliza Bunge la Bajeti limemalizika mwezi Juni. je mambo yote yaliyoshauriwa na wabunge kuhusu Kilimo ameshayamaliza kuyafanyia kazi.?

Je anamuonesha Mhe. Rais kuwa alimteua mtu ambaye hajui cha kufanya Wizara ya Kilimo hadi aanze kuokoteza mawazo kwenye mitandao? na je anaamini wakulima wako Instagramu?

Au ndio ile kauli ya mfa maji haishi kutapata baada ya usimamizi mbovu wa wizara na kusababisha nchi kukumbwa na baa la njaa kutokana na usimamizi mbovu kuruhusu wananchi wa mataifa mengine kuingia vijijini mashambani na kununua mazao moja kwa moja hadi Japan kuamua kuingia kati kusaidia Tanzania fedha kwa ajili ya ununuzi wa chakula?

Mimi nadhani ni muda sasa kwa Waziri Bashe kujiuzulu ili kumpa nafasi Mheshimiwa Rais kutafuta mtu mwingine atakayeweza kusimamia sekta ya kilimo na tuondokane na baa la njaa alilolisababisha Bashe
Kuomba ushauri zaidi haimaanishi kushindwa bali anataka ushauri hadi kwa uwakilishi wa levo ya chini.Namwambia mh kuwa zoezi la kujiandikisha mbolea za ruzuku baadhi ya maeneo kuna urasimu.Pili watu kuuza mahindi yao kwa wanunuzi wa nje si mbaya ukizingatia bei za mbolea zilivyokuwa ghali acha wajilipe.Muhimu serikali kama inataka akiba ya kutosha iwe inanunuwa mapema si inakuja baada ya wanunuzi binafsi.La mwisho bei za pembejeo zishuke kwa ujumla si kwa ruzuku tu.
 
Miluzi mingi humpoteza mbwa.

Ngoja apewe ushauri sasa.
Hata hilo la kujiuzulu ni miongoni mwa hayo aliyoyataka ashauriwe na wananchi. Sasa kazi kwake
 
ambao hawajui wafanye nini mbona wengi tu awamu hii.

yaani wamejazana tu kutumbua tozo ila hawana msaada wowote.
 
Wizara ya kilimo iongeze Kasi ya ujenzi wa scheme za umwagiliaji nchini Ili kilimo cha misimu miwili kienee nchi nzima na malighafi za VIWANDA zipatikane za kutosha!

Nchi yangu Tanzania BADO haijawekeza VIZURI KWENYE kilimo!maneno ni Mengi kuliko vitendo!
 
Huyu ni Waziri hodari Wizala ya Hela ndio inapwaya.
 
Watu hamna jema mnapewa fursa ya kusikilizwa mnaleta kebehi
Bashe kaza Baba Mungu akujaalie
 
Kilimo ni zaidi ya kutoa mbolea za ruzuku, sasa wao kwa sasa ni sifa tu kuwa tumetoa mbolea kwa bei nafuu, wakati, kilimo ni zaidi ya mbolea, haya sasa umetoa mbolea hata bure, mvua hakuna, na hakuna mikakati ya kilimo cha umwagiliaji, hayo mavuno yanatoka wapi?
Uuzaji nao ni shida, kwenye bei
Ss si ndo muwasiliane nae kasema
Ungekua waziri wewe ungefanya yote unayotamani at par?.
 
Jambo la heri Sana kusikiliza maoni ya wananchi ukiwemo mfumuko wa bei wa chakula uliosababishwa na mikurupuko ya wanasiasa pasipokufahamu kuwa usalama wa chakula ndyo amani ya taifa. Wananchi wanateseka kwa sababu ya madhara yanayosabishwa na wanasiasa ambao wanaishi maisha ya anasa ya kufuru.

Wanasiasa wanatengeneza tatizo likiwaelemea wanakuja na ndimi za kutaka ushauri (unafiki). Mmeishaharibu mnatakiwa kutubu kwanza ili Mungu atuepushe na baa la ukame kwa sababu mtaji wa mkulima ni nguvu zake mwenyewe na sio propaganda uchwara za wanasiasa uchwara mnaoishi maisha ya peponi.
 
Back
Top Bottom