Bashe anaumwa nini kwanini inakuwa Siri?

Bashe anaumwa nini kwanini inakuwa Siri?

TAARIFA za kuumwa kwa Mheshimiwa Hussein Bashe zimetangazwa na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa lakini hadi sasa haijawekwa wazi anaumwa nini na amelazwa hospitali gani ili watanzania wenye nafasi waweze kumtembelea kama ni hospitali.

Kwanini maradhi ya viongozi inakuwa siri lakini mtu akifa ndio mnakuja kutangaza na kutoa ratiba ya mazishi kumbuka vifo kama vya Dk. Ndugulile, Mafuru, Meja Jenerali Charles Mbuge na wengine tulikuja kutangaziwa msiba na ratiba ya mazishi.

Serikali itoke hadharani ieleze Bashe anaumwa nini na amelazwa hospitali gani kama ni ndani ya nchi au nje ya nchi ili watanzania wajue hali ya kiongozi wao.
Wewe ukiumwa nani huwa anatangaza habari za ugonjwa wako?
 
yeye ni mtumishi wa Umma na analipwa mshahara na umma na anatibiwa na umma hilo nalo ulikumbuke
Kuwa mtumishi umma na kulipwa mshahara na umma hakumaanishi pia kuingilia maisha binafsi ya mtumishi huyo. Umeshaambiwa anaumwa, basi inatosha. Unataka nini zaidi? Endapo mwenyewe au ndugu zake hawapo tayari kutaja ugonjwa wake, hakuna haja ya kulazimisha kutaka kujua zaidi ya hapo.
 
yeye ni mtumishi wa Umma na analipwa mshahara na umma na anatibiwa na umma hilo nalo ulikumbuke
Ugonjwa ni siri ya Ntu kusema au la. Nchii hii kuna Watumishi wangapi wa Uma ? Wote hao wakiumwa hutolewa taarifa zao?
 
Back
Top Bottom