Bashe punguza kujiamini kana kwamba una hisa ki uongozi na aliyekuteua

Bashe punguza kujiamini kana kwamba una hisa ki uongozi na aliyekuteua

Suzy Elias

JF-Expert Member
Joined
Nov 9, 2021
Posts
1,067
Reaction score
6,200
Bwana mdogo Bashe kwa siku za hivi karibuni umeonyesha hali ya kujiamini iliyopitiliza huku ukisahau kwamba wewe ni mteule na mda wowote uteule wako unaweza kutenguliwa.

Tatizo la vijana wengi huwa mnavimba vichwa mnapopata kuaminiwa na kusifiwa na mteule japo kwa mambo kadha wa kadha mnapotimiza wajibu wenu mfano ni wewe Bashe na wenzako kama kina January.

Wadogo zetu timizeni wajibu wenu pasi na kuvimba kichwa huku mkijibu kwa mbwembwe na nyodo wenzenu wasiyo na madaraka kama yenu.

Yupo wapi leo mjivuni Kigwangala na mbwembwe zake?!

Yupo wapi leo Mpina na ulijali wake?!

Funzo hapa ni muhimu na lazima muwe welevu na muwiwe na kiasi. Madaraka ni dhamana tu na aliyekupa anaweza kukunyang'anya pia.
 
Tuache wivu kutokujiamini ndio kumetufanya tuchukuliwe utumwa.
 
Huyo mwingine si alikuwa anapigia promo mitungi ya gesi, labda wana backing ya rost tamu, nchi isharudi kwa matajiri hii, acha wanyonge tuendelee kulipa tozo na faini za kimchongo za NEMC.
 
Tunataka Viongozi wanaojiamini kama huyu Mlugaluga.

Tena huyu alitufaa sana kwenye Ministry of Defence.

Ili aibe hala za kununulia Vifaru.

#Free Dawa Juma
 
Tanzania ina idadi kubwa ya vijana wasiojiamini. Bashe ni mfano wa vijana wachache wa kitanzania wenye elimu ya wastani wanaojiamini. Bashe mpaka sasa, ameonyesha uthubutu kwenye Wizara ya kilimo anastahili pongezi na kuungwa mkono.
 
Wivu umetawala kwa kijana wetu mchapa kazi na hawa ndio waliopiga "makitaimu" muda mrefu na bado uwaziri umekuwa ndoto kwao,piga kazi Bashe aibu ziendelee kuwakuta wanaokuita msomari mara 16mil/acre.
Wameishiwa mbinu na kuona bora wawatunuku jf members ili waichafue legacy yako.
 
Wasomali asilia ni majasiri na wenye kusimamia vizuri wanachokiamini.
 
Kujiamini ni vizuri Kiongozi ajiamini.

Anakosea pale anapodhani Yeye ana akili kuliko wote nchini na mawazo yake ndiyo Dira ya Taifa, hapo anakosea sana.

Aache KUJITUTUMUA, maana Kwa kufanya hivyo udhaifu wake haijifichi.
 
Back
Top Bottom