Bashe usitetereke kama Mwigulu, Januari na Nape. Wamekuona tishio kwenye malengo yao ya Siasa ndio maana wamekushikia bango

Bashe usitetereke kama Mwigulu, Januari na Nape. Wamekuona tishio kwenye malengo yao ya Siasa ndio maana wamekushikia bango

ChoiceVariable

JF-Expert Member
Joined
May 23, 2017
Posts
66,537
Reaction score
75,687
Natoka tahadhari Kwa Bashe, Waliokuwhikia Bango Kwa hoja za kizushi na upuuzi ndio hao hao waliokuwa wamemshikia Bango Mwigulu, January na Nape.

Sasa wanaona kabisa unaenda kuwa threats Kwa ambions zao za Kisiasa Kwa vile una deal na sekta ambayo inakufanya kukutana na kucheza na maslahi ya Moja kwa Moja ya wakulima ambao ndio wapiga kura..

Usije kuteteleka, wametumwa Kwa kazi hiyo so komaa maana wanaona Nyota Yako inaend akuwaka na namna pekee ya kukuharibia ni kutunga fitina, uzushi na hoja za kipuuzi.

Madam una backup ya Rais Kamatia hapo hapo sisi wakulima tunakuelewa sana.

Toka Umekuwa Waziri umekiheshimisha Kilimo na Vijana wengi Sasa na wakulima Kwa ujumla wamepata Imani kuwa Kilimo ni biashara na tunalima kinatulipa tofauti ilivyokuwa awamu ya 5.

Sasa hivi hakuna zao ambalo limeanguka bei Bali mazao yote Kwa Sasa yanauzika na sisi ndio tunataka hivyo..

Ni hayo tuu Kasi iendelee 👇
 
Watu wanakwambia ekari Moja ni mil.17 sijui wameitoa wapi
 
Natoka tahadhari Kwa Bashe,Waliokuwhikia Bango Kwa hoja za kizushi na upuuzi ndio hao hao waliokuwa wamemshikia Bango Mwigulu, January na Nape..

Sasa wanaona kabisa unaenda kuwa threats Kwa ambions zao za Kisiasa Kwa vile una deal na sekta ambayo inakufanya kukutana na kucheza na maslahi ya Moja kwa Moja ya wakulima ambao ndio wapiga kura..

Usije kuteteleka ,wametumwa Kwa kazi hiyo so komaa maana wanaona Nyota Yako inaend akuwaka na namna pekee ya kukuharibia ni kutunga fitina,uzushi na hoja za kipuuzi..

Madam una backup ya Rais Kamatia hapo hapo sisi wakulima tunakuelewa sana..

Toka Umekuwa Waziri umekiheshimisha Kilimo na Vijana wengi Sasa na wakulima Kwa ujumla wamepata Imani kuwa Kilimo ni biashara na tunalima kinatulipa tofauti ilivyokuwa awamu ya 5..

Sasa hivi hakuna zao ambalo limeanguka bei Bali mazao yote Kwa Sasa yanauzika na sisi ndio tunataka hivyo..

Ni hayo tuu Kasi iendelee 👇

Bashe amejitahidi sana kuonyesha ubunifu na kusimamia anachokiamini na kwa kweli BBT na uwekezaji knye schemes za umwagiliaji utaleta mapinduzi makubwa sana sana knye kilimo Tanzania, Angalizo tusimchonhganishe na wenzake akina Mwigulu, January na Nape wote wanajenga nyumba moja Boss wao mmoja tu majukumu tofauti
 
Bashe amejitahidi sana kuonyesha ubunifu na kusimamia anachokiamini na kwa kweli BBT na uwekezaji knye schemes za umwagiliaji utaleta mapinduzi makubwa sana sana knye kilimo Tanzania, Angalizo tusimchonhganishe na wenzake akina Mwigulu, January na Nape wote wanajenga nyumba moja Boss wao mmoja tu majukumu tofauti
Kwanza Kilimo cheti kinaenda kuwa Cha umwagiliaji full na sio hadithi ni vitendo..

Ameajiri wahandisi wa umwagiliaji,amewapa magari ya usimamizi,amewapa posho na amewapa vitendea kazi..

Amejitahidi kutafuta soko Kwa mazao ya Kila aina na anajitahidi kulinda soko la ndani.

Ameweka lengo la kuhakikisha tunahifadhi tani za chakula Cha kutosha miezi walau 6 by 2025 na Kwa malengo ya 2030 chakula kitoshe miaka 2..
 
Jamani tuwe wa kweli, Kuna hatua zinapigwa, Jana kwa mara ya kwanza naona kunde kijijini kwangu Mapili ya Newala zinanunuliwa kilo Moja 3000 tshs nikauliza zinaenda wapi, nikapewa jibu soko halisi kwa uwanda wetu lipo Mkunya ( Newala) na huko kilo ni tshs 4000. Hatua hii ni kubwa, maana kunde kwetu ilikuwa mboga na sio biashara. Karanga ilikuwa ni kiungo Cha dagaa na majani ya kunde lakini Leo plastiki Moja ya karanga za maganda ni tshs 10,000. Fursa mpya zipo.
 
Sekta ya kilimo ina uwezo wa kuajiri watu wengi sana. Tanzania inaweza kulisha Afrika nzima, na hata nje ya Afrika kama tutataka hiyo ndiyo iwe identity yetu.

Hivyo, lengo la Serikali ya awamu ya 6 kuwekeza heavily kwenye kilimo, ni wazo jema LAKINI lengo na dhamira pekee, havitoshi kufikia lengo. Kunahitajika mambo mengi kwa pamoja. Mbinu za kufikia huko zinatakiwa kuwa sahihi na zinazofanyiwa review kila hatua, na kufanya marekebisho ya mara kwa mara kila inapobidi.

Mathalani kupeleka kwanza miundombinu ya kilimo kwenye maeneo ambayo hayajawa mashamba bado wakati kuna maeneo ambayo tayari ni mashamba lakini hayana miundombinu wezeshi, ni makosa ya wazi kwenye hatua za awali.

Ilikuwa ni jambo sahihi kwanza kupeleka miundombinu wezeshi kwenye maeneo ambayo tayari ni mashamba. Faida ya kufanya hivyo, kwanza unakuwa na uhakika wa kuanza kupata ongezeko la haraka la uzalishaji, jambo la pili una uhakika kuwa unashughulika na watu ambao tayari wana commitment kwenye kilimo, na pia unashughulika na watu ambao tayari wana ufahamu wa kutosha wa kilimo na changamoto zake, na Serikali ingeenda moja kwa moja kwenye changamoto.

Hii miradi mipya itakuwa na muda mrefu wa kusubiria matokeo. Hii miradi mipya ilistahili kuanzishwa hatua kwa hatua huku ukipima mafanikio ya kule ambako tayari wapo kwenye hatua ya uzalishaji.
 
Mimi namuelewa sana Hussein Bashe kuanzia akiwa mbunge wa kawaida kipindi cha 2010-15, hoja zake siku zote zilikuwa ni kwenye kilimo na biashara. Hatimaye akawa Naibu Waziri 2015-20 aliendelea kung'ara kuliko waziri wake kwenye kilimo.

Sasa amekuwa Waziri full kua zia 2021- onwards Bashe ana WALK THE TALK. Ardhi ya Tanzania inayofaa kulimwa haitumiki ipasavyo. Yasemekeana ni chini ya 15% ya ardhi inayofaa ndiyo inatumika kwa kilimo.

Sera za Bashe zinakwenda kuleta thamani kwenye kilimo kwa kukigeuza kuwa kilimo biashara. Kitatengeneza ajira nyingi kwa multiplier effect hivyo kuwavutia watu wengi kujihusisha na kilimo.

Sera zote zilizotangulia kuanzia Awamu ya JKN kwenye kilimo zililenga kulima kwa ajili ya kuwa na mazao mengi ili kupambana na njaa na kuacha utegemezi kutoka nje. Ni Bashe tu ndiyo amekuja na sera ya kilimo inayohusisha biashara. Vilevile Sera zilizotanguilia ziliategemea uwapo wa mvua, lakini Sera za Bashe zinahusisha umwagiliaji maji.

Ukiona unatupiwa mawe sana ujuwe unayofanya ni mazuri. Bashe ASIOGOPE bali aendelee hivyo hivyo
 
Sekta ya kilimo ina uwezo wa kuajiri watu wengi sana. Tanzania inaweza kulisha Afrika nzima, na hata nje ya Afrika kama tutataka hiyo ndiyo iwe identity yetu.

Hivyo, lengo la Serikali ya awamu ya 6 kuwekeza heavily kwenye kilimo, ni wazo jema LAKINI lengo na dhamira pekee, havitoshi kufikia lengo. Kunahitajika mambo mengi kwa pamoja. Mbinu za kufikia huko zinatakiwa kuwa sahihi na zinazofanyiwa review kila hatua, na kufanya marekebisho ya mara kwa mara kila inapobidi.

Mathalani kupeleka kwanza miundombinu ya kilimo kwenye maeneo ambayo hayajawa mashamba bado wakati kuna maeneo ambayo tayari ni mashamba lakini hayana miundombinu wezeshi, ni makosa ya wazi kwenye hatua za awali.

Ilikuwa ni jambo sahihi kwanza kupeleka miundombinu wezeshi kwenye maeneo ambayo tayari ni mashamba. Faida ya kufanya hivyo, kwanza unakuwa na uhakika wa kuanza kupata ongezeko la haraka la uzalishaji, jambo la pili una uhakika kuwa unashughulika na watu ambao tayari wana commitment kwenye kilimo, na pia unashughulika na watu ambao tayari wana ufahamu wa kutosha wa kilimo na changamoto zake, na Serikali ingeenda moja kwa moja kwenye changamoto.

Hii miradi mipya itakuwa na muda mrefu wa kusubiria matokeo. Hii miradi mipya ilistahili kuanzishwa hatua kwa hatua huku ukipima mafanikio ya kule ambako tayari wapo kwenye hatua ya uzalishaji.
Kwani saizi haianzishwi hatua Kwa hatua? Mradi wako uliouanzisha ni upi Ili tujigunze hizo hatua?
 
Jamani tuwe wa kweli, Kuna hatua zinapigwa, Jana kwa mara ya kwanza naona kunde kijijini kwangu Mapili ya Newala zinanunuliwa kilo Moja 3000 tshs nikauliza zinaenda wapi, nikapewa jibu soko halisi kwa uwanda wetu lipo Mkunya ( Newala) na huko kilo ni tshs 4000. Hatua hii ni kubwa, maana kunde kwetu ilikuwa mboga na sio biashara. Karanga ilikuwa ni kiungo Cha dagaa na majani ya kunde lakini Leo plastiki Moja ya karanga za maganda ni tshs 10,000. Fursa mpya zipo.
Tanzania ukitaka kufanya jambo usisikilize makelele ya loosers na wengi wao wakiona unafaulu watakuja na msululu wa mambo mengi yasiyo na Tija kukosoa

 
Mnapost na kukuoment wenyewe vibaraka wa Bashe
 
Mimi namuelewa sana Hussein Bashe kuanzia akiwa mbunge wa kawaida kipindi cha 2010-15, hoja zake siku zote zilikuwa ni kwenye kilimo na biashara. Hatimaye akawa Naibu Waziri 2015-20 aliendelea kung'ara kuliko waziri wake kwenye kilimo.

Sasa amekuwa Waziri full kua zia 2021- onwards Bashe ana WALK THE TALK. Ardhi ya Tanzania inayofaa kulimwa haitumiki ipasavyo. Yasemekeana ni chini ya 15% ya ardhi inayofaa ndiyo inatumika kwa kilimo.

Sera za Bashe zinakwenda kuleta thamani kwenye kilimo kwa kukigeuza kuwa kilimo biashara. Kitatengeneza ajira nyingi kwa multiplier effect hivyo kuwavutia watu wengi kujihusisha na kilimo.

Sera zote zilizotangulia kuanzia Awamu ya JKN kwenye kilimo zililenga kulima kwa ajili ya kuwa na mazao mengi ili kupambana na njaa na kuacha utegemezi kutoka nje. Ni Bashe tu ndiyo amekuja na sera ya kilimo inayohusisha biashara. Vilevile Sera zilizotanguilia ziliategemea uwapo wa mvua, lakini Sera za Bashe zinahusisha umwagiliaji maji.

Ukiona unatupiwa mawe sana ujuwe unayofanya ni mazuri. Bashe ASIOGOPE bali aendelee hivyo hivyo
Sana! Ukiona unapigwa mawe ujue unafanya vizuri!

Hii inanikumbusha wapumbavu na mataahira yaliyokuwa yanampiga mawe jpm.
 
Peleka barabara za lami hadi vijijini, weka miundombinu ya upataikanaji wa maji na umeme kila kijiji huko ndio kuna wakulima.
Weka mazingira mazuri ya kupata pembejeo za kilimo kwa urahisi na nafuu uone jinsi kilimo kitakavyo stawi bila porojo anazofanya bashe
 
Peleka barabara za lami hadi vijijini, weka miundombinu ya upataikanaji wa maji na umeme kila kijiji huko ndio kuna wakulima.
Weka mazingira mazuri ya kupata pembejeo za kilimo kwa urahisi na nafuu uone jinsi kilimo kitakavyo stawi bila porojo anazofanya bashe
Hiyo ya Barabara ni kazi ya Bashe? By the way kwani hujui kwamba hayao yanafanyika Sasa hivi na awamu ya 6?
 
Sijaona kabisa ununuzi wa matrekta popote...kilimo cha jembe la mkono??
 
Bashe ndo wazir kijana pekee anafaa kuwa Raisi nchi hii , sifa ya kiongozi ni kuwa na msimamo dhabiti hasa kwenye hii nchi yenye wajinga wengi alaf wasomi wachache waliopo ni machawa , wanafiki na Mafisadi ... Bashe anawaelewa Kwa usahihi wananchi wa nchi hii
 
Back
Top Bottom