Bashir Yakub: Nitayashitaki makampuni manne ya simu

Bashir Yakub: Nitayashitaki makampuni manne ya simu

NAYASHITAKI MAKAMPUNI MANNE YA SIMU.
BASHIR YAKUB, Wakili.
0714047241


Naishitaki Tigo, Airtel, Vodacom na Halotel. Kwa mujibu ya Sheria Namba 12/2003 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania mashtaka ya aina hii natakiwa kuyaandikia makampuni hayo taarifa kuyataka yarekebishe ndani ya siku 30 ninacholalamikia yakishindwa naendelea mbele,ambapo nimeshayaandikia makampuni hayo.

Kwenye mashitaka yangu ninaomba mambo matano.

JAMBO LA KWANZA. Vifurushi vyote havipaswi kuexpire. Kitu pekee ambacho kinapaswa kumaliza kifurushi inatakiwa iwe ni wewe kuongea hadi dakika zako zikaisha.

Si haki kukata kifurushi cha mtu ambaye dakika zake za kuongea,za data, au sms bado zipo kwa kigezo cha kuexpire au muda wake wa wiki,masaa12,nk kuisha. Nchi nyingi hii kitu imeondolewa imebaki kwetu na pengine pachache.

Mathalan, umejiunga kifurushi cha 1000 na umepewa dakika 10 ndani ya masaa 12. Umetumia dakika 3 tu ambazo thamani yake kifedha ni shilingi 300, na masaa 12 yameisha. Maana yake kwenye 1000 yako zilibaki dakika 7 ambazo thamani yake kifedha ni shilingi 700, ambazo hizo sasa shilingi 700 kampuni ya simu inajirudishia kwa kigezo cha muda kuexpire. Nachelea kuiita huu wizi lakini initoshe kusema hii haiwezi kuwa haki.

Lakini pia ninapolipa 500 na wewe ukaniuzia kifurushi si nimekulipa hela yako yote na wewe hunidai. Sasa kwanini tena unachukua kilekile nilichonunua kwako na hela yako yote nimeshakulipa.

Ni hivi,unaponunua kifurushi ni sawa na umenunua bidhaa, na ukishanunua bidhaa hakuna mtu mwingine yeyote, akiwemo aliyekuuzia bidhaa hiyo, mwenye haki ya kuichukua tena bidhaa hiyo yote au sehemu yake isipokuwa wewe uitumie mpaka iishe.

Tizama Tanesco na LUKU. Tanesco akishakuuzia umeme/units ukamlipa basi hatma ya units zako ni utumie mpaka umalize.Hawezi kuikata na kujirudishia kwasababu anajua alikuuzia bidhaa na wewe ukamlipa na hivyo una haki ya kutumia bidhaa yako mpaka umalize. Hii ndiyo HAKI.

Kinachofanywa na makampuni ya simu ni sawa ununue mkate dukani na mwenye duka umlipe hela yake yote. Halafu mwenye duka huyohuyo akwambie kwamba usipokula mkate huo kufikia saa 12 za jioni au ndani wiki au mwezi nitakuja tena kuuchukua nyumbani kwako, na aje kweli auchukue iwe mali yake tena kwa mara ya pili.

Zaidi ya hayo,ukweli halisi ni kuwa kifurushi kwa muundo wake si bidhaa inayoexpire. Ukinunua mkate ukiexpire utauona, utaona kabisa kwa macho umeoza kadhalika bidhaa nyingine zenye sifa ya kuexpire. Lakini kifurushi kwa uhalisi wake si bidhaa inayoexpire au yenye sifa ya kuexpire.

Hili neno kuexpire limetengezwa ili kuficha neno kupora au uporaji. Ukweli ni kwamba kifurushi kinaporwa makusudi kwa kigezo hovyo kabisa na dhahania cha kuexpire, sijui masaa yako 12, sijui wiki yako, sijui mwezi wako umeisha nk. Kifurushi kinaishaje kabla dakika zangu nilizolipia kwa ukamilifu sijazitumia zikaisha ?.

Yapo haya nayo lazima yaeleweke, mtu amejiunga lakini yuko safarini hawezi kutumia mda wake , mwingine alipo hakuna network, mwingine hajatumia mda wake alikuwa bize na kazi zake, mwingine simu haikuwa na chaji siku nzima, mwingine umeme ulikatika alikosa mawasiliano nk nk, hawa wote pesa zao walizolipia na hawajazitumia au wametumia kidogo zinakatwa na makampuni ya simu yanajirudishia pesa hizo bila kujali.

Nimefungua kesi kuondoa unyonyaji huu na lazima uondoke.Hatuwezi kuendelea kuwa viwanda vya kutengeneza ukwasi wa makampuni ya simu.

JAMBO LA PILI. Haki ya kutochanganyiwa kifurushi na muda wa kawaida wa maongezi bila ridhaa.

Nitatoa mfano, unakuta mtu ameweka shilingi 1000 kwenye simu ambapo anajiunga 500 na 500 inabaki kama muda wa maongezi wa kawaida. Wakati anapokuwa akizungumza au akitumia data kupitia ule muda aliojiunga na ukaisha basi simu haikatiki bali inaunganisha moja kwa moja na ile 500 ya muda wa maongezi wa kawaida ambayo alikuwa hajajiunga.

Hii si sawa hata kidogo na ni vitu ambavyo vinatengenezwa maksudi ili kujipatia fedha bila kujali mtumiaji anaumia kiasi gani. Ni hivi, mtu anapoamua kujiunga 500 na akabakisha 500 bila kuiunga ana maana yake kubwa tu.Hakushindwa kuunganisha 1000 yote.Amechagua 500 kwa maksudi maalum. Sasa iweje unamlazimisha kutumia akiba yake ya 500 hata bila ridhaa yake.

Inatakiwa kuwe na chaguo(option) iwapo mtu anahitaji huduma ya aina hiyo au hapana. Au inatakiwa muda wa kifurushi ukiisha simu ikate halafu kama anataka kuendelea kutumia muda wa kawaida achague mwenyewe kuendelea kuutumia na sio kampuni ya simu kumchagulia.

Au kama anataka kujiunga na hiyo 500 iliyobaki basi ajiunge. Isiwe biashara ya kuviziana kama ilivyo sasa. Hili nalo lazima waliondoe.

JAMBO LA TATU, Haki ya kujua matumizi ya kifurushi.Malalamiko ya vifurushi vya watu kuliwa isivyo kawaida ni mengi mno.

Unanunua dakika 20 unaongea 10 unaambiwa kifurushi kimeisha, unabaki kushangaa. Ni lazima waweke mfumo wenye kutoa taarifa sahihi na za wazi(transparency) ili kumwezesha mtumiaji kumonita matumizi ya kifurushi chake.

Malalamiko ya watu ya kutumia vifurushi chini ya kile walichonunua yanaongezeka siku hadi siku. Kuwaachia makampuni ya simu wao wawe ndio wauzaji wa vifurushi, na wao hao hao ndio wakueleze umetumia nini,kama umemaliza au hujamaliza, huku wewe mteja ukiwa kipofu/gizani ukisubiri kupokea lolote wanalolisema wao, kupigwa hakuwezi kukwepeka.

Waweke mfumo ambao wao pamoja na mteja watamonita matumizi ili mteja aweze kuhoji. Teknolojia imekua hili ni dogo sana.

JAMBO LA NNE. Haki ya kuhamisha kifurushi.

Nimesema hapo juu kifurushi ni mali yako na ndo maana unailipia pesa na hivyo kuwa na haki ya kuitumia kwa uhuru.

Kwa msingi huu makampuni ya simu ni lazima yaweke mfumo unaomwezesha mtu kumhamishia mtu mwingine kifurushi kama ilivyo kwenye muda wa kawaida wa maongezi. Maana yake nikinunua kifurushi cha 1000 labda dakika 10 za maongezi, Mb 100, na sms 50.

Niwe na uwezo wa kumgawia yeyote ninayemtaka kiasi cha muda wangu wa maongezi,sms au Mb. Na hii inafanyika nchi nyingi na inawezekana zaidi kugawiana watu wa mtandao mmoja.Tunahitaji uhuru huu kwetu.

JAMBO LA TANO. Haki ya kupewa tahadhari kuhusu kifurushi au muda wa hewani unapokaribia kuisha. Kuna makampuni wana huduma hii lakini wanaitoa kwa hiari sana na wengine wameacha kabisa. Wengine wanatoa tahadhari muda unapoisha na sio unapokaribia.

Tunataka watoe unapokaribia ili mtu ajipange. Ni haki mtu kupewa tahadhari wakati akizungumza,akiwa kwenye mtandao, au sms, kuhusu dakika zake kukaribia kuisha. Sio sahihi wala ustaarabu simu kukatika ghafla bila tahadhari.

Na wanafanya hivyo maksudi wakijua unapokatakiwa na mawasiliano ghafla ni lazima tu utakuwa hujamaliza haja yako na hivyo utalazimika kuongeza vocha ili umalizie na wao wapate mauzo zaidi.

Wanajua ukipewa tahadhari unaweza tu kufupisha mazungumzo yako na wakati simu inakatika ukawa tayari umemaliza na hivyo usihitaji tena kuongeza vocha. Tabia za hovyo kabisa za kuviziana.

Unawezaje kunipa tahadhari ya muda kuisha ukashindwa kunipa ya muda kukaribia kuisha. Hili nalo tunataka lifanyiwe kazi.

SHERIA
Mambo haya kwa ujumla wake ni kinyume na Katiba ya JMT Ibara ya 18( c ) inayotaka uwepo wa mawasiliano bila kuingiliwa, lakini yanakiuka Kanuni za Kielektroniki na Mawasilano ya Posta kuhusu viwango vya Tozo GN. No 22/2018 hasa Kanuni ya 4 ( 1na 2) inayotaka viwango vyote vya tozo za simu kuwa vya haki na kadri(just and reasonable), yanakiuka Kanuni ya 4 ya Kanuni za Kielektroniki na Mawasiliano ya Posta GN No.61/2018 kuhusu kumlinda mlaji inayotaka mlaji kupewa taarifa kwa usahihi ya matumizi ya huduma muda wote, yanakiuka Sheria ya Ushindani namba 8/2003 inayotaka mtoa huduma kutoa huduma kwa kuzingatia zaidi maslahi ya watu wa hali ya chini, na sheria nyingine nyingi zimekiukwa.

Na tuelewane vizuri hapa, hakuna kitu kinaitwa VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA. Sheria iko wazi kuwa neno,maneno,sentensi au msemo wowote wenye lengo la kusigina haki ya mtu/watu ni batili.

Basi nitaviomba vyombo vya maamuzi vitusaidie kuyaweka sawa haya matano.Tutazidi kupeana taarifa kadri inavyokwenda.
Facts.. Ila shida itakua ni kwenye utekelezaji na hasa ukizingatia kwamba hata kwenye kampuni ya serikali (TTCL) hilo tatzo lipo.. Ila nakuombea ushindi mdau ili iwe faida kwako na Taifa kwa ujumla
 
NAYASHITAKI MAKAMPUNI MANNE YA SIMU.
BASHIR YAKUB, Wakili.
0714047241


Naishitaki Tigo, Airtel, Vodacom na Halotel. Kwa mujibu ya Sheria Namba 12/2003 ya Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania mashtaka ya aina hii natakiwa kuyaandikia makampuni hayo taarifa kuyataka yarekebishe ndani ya siku 30 ninacholalamikia yakishindwa naendelea mbele,ambapo nimeshayaandikia makampuni hayo.

Kwenye mashitaka yangu ninaomba mambo matano.

JAMBO LA KWANZA. Vifurushi vyote havipaswi kuexpire. Kitu pekee ambacho kinapaswa kumaliza kifurushi inatakiwa iwe ni wewe kuongea hadi dakika zako zikaisha.

Si haki kukata kifurushi cha mtu ambaye dakika zake za kuongea,za data, au sms bado zipo kwa kigezo cha kuexpire au muda wake wa wiki,masaa12,nk kuisha. Nchi nyingi hii kitu imeondolewa imebaki kwetu na pengine pachache.

Mathalan, umejiunga kifurushi cha 1000 na umepewa dakika 10 ndani ya masaa 12. Umetumia dakika 3 tu ambazo thamani yake kifedha ni shilingi 300, na masaa 12 yameisha. Maana yake kwenye 1000 yako zilibaki dakika 7 ambazo thamani yake kifedha ni shilingi 700, ambazo hizo sasa shilingi 700 kampuni ya simu inajirudishia kwa kigezo cha muda kuexpire. Nachelea kuiita huu wizi lakini initoshe kusema hii haiwezi kuwa haki.

Lakini pia ninapolipa 500 na wewe ukaniuzia kifurushi si nimekulipa hela yako yote na wewe hunidai. Sasa kwanini tena unachukua kilekile nilichonunua kwako na hela yako yote nimeshakulipa.

Ni hivi,unaponunua kifurushi ni sawa na umenunua bidhaa, na ukishanunua bidhaa hakuna mtu mwingine yeyote, akiwemo aliyekuuzia bidhaa hiyo, mwenye haki ya kuichukua tena bidhaa hiyo yote au sehemu yake isipokuwa wewe uitumie mpaka iishe.

Tizama Tanesco na LUKU. Tanesco akishakuuzia umeme/units ukamlipa basi hatma ya units zako ni utumie mpaka umalize.Hawezi kuikata na kujirudishia kwasababu anajua alikuuzia bidhaa na wewe ukamlipa na hivyo una haki ya kutumia bidhaa yako mpaka umalize. Hii ndiyo HAKI.

Kinachofanywa na makampuni ya simu ni sawa ununue mkate dukani na mwenye duka umlipe hela yake yote. Halafu mwenye duka huyohuyo akwambie kwamba usipokula mkate huo kufikia saa 12 za jioni au ndani wiki au mwezi nitakuja tena kuuchukua nyumbani kwako, na aje kweli auchukue iwe mali yake tena kwa mara ya pili.

Zaidi ya hayo,ukweli halisi ni kuwa kifurushi kwa muundo wake si bidhaa inayoexpire. Ukinunua mkate ukiexpire utauona, utaona kabisa kwa macho umeoza kadhalika bidhaa nyingine zenye sifa ya kuexpire. Lakini kifurushi kwa uhalisi wake si bidhaa inayoexpire au yenye sifa ya kuexpire.

Hili neno kuexpire limetengezwa ili kuficha neno kupora au uporaji. Ukweli ni kwamba kifurushi kinaporwa makusudi kwa kigezo hovyo kabisa na dhahania cha kuexpire, sijui masaa yako 12, sijui wiki yako, sijui mwezi wako umeisha nk. Kifurushi kinaishaje kabla dakika zangu nilizolipia kwa ukamilifu sijazitumia zikaisha ?.

Yapo haya nayo lazima yaeleweke, mtu amejiunga lakini yuko safarini hawezi kutumia mda wake , mwingine alipo hakuna network, mwingine hajatumia mda wake alikuwa bize na kazi zake, mwingine simu haikuwa na chaji siku nzima, mwingine umeme ulikatika alikosa mawasiliano nk nk, hawa wote pesa zao walizolipia na hawajazitumia au wametumia kidogo zinakatwa na makampuni ya simu yanajirudishia pesa hizo bila kujali.

Nimefungua kesi kuondoa unyonyaji huu na lazima uondoke.Hatuwezi kuendelea kuwa viwanda vya kutengeneza ukwasi wa makampuni ya simu.

JAMBO LA PILI. Haki ya kutochanganyiwa kifurushi na muda wa kawaida wa maongezi bila ridhaa.

Nitatoa mfano, unakuta mtu ameweka shilingi 1000 kwenye simu ambapo anajiunga 500 na 500 inabaki kama muda wa maongezi wa kawaida. Wakati anapokuwa akizungumza au akitumia data kupitia ule muda aliojiunga na ukaisha basi simu haikatiki bali inaunganisha moja kwa moja na ile 500 ya muda wa maongezi wa kawaida ambayo alikuwa hajajiunga.

Hii si sawa hata kidogo na ni vitu ambavyo vinatengenezwa maksudi ili kujipatia fedha bila kujali mtumiaji anaumia kiasi gani. Ni hivi, mtu anapoamua kujiunga 500 na akabakisha 500 bila kuiunga ana maana yake kubwa tu.Hakushindwa kuunganisha 1000 yote.Amechagua 500 kwa maksudi maalum. Sasa iweje unamlazimisha kutumia akiba yake ya 500 hata bila ridhaa yake.

Inatakiwa kuwe na chaguo(option) iwapo mtu anahitaji huduma ya aina hiyo au hapana. Au inatakiwa muda wa kifurushi ukiisha simu ikate halafu kama anataka kuendelea kutumia muda wa kawaida achague mwenyewe kuendelea kuutumia na sio kampuni ya simu kumchagulia.

Au kama anataka kujiunga na hiyo 500 iliyobaki basi ajiunge. Isiwe biashara ya kuviziana kama ilivyo sasa. Hili nalo lazima waliondoe.

JAMBO LA TATU, Haki ya kujua matumizi ya kifurushi.Malalamiko ya vifurushi vya watu kuliwa isivyo kawaida ni mengi mno.

Unanunua dakika 20 unaongea 10 unaambiwa kifurushi kimeisha, unabaki kushangaa. Ni lazima waweke mfumo wenye kutoa taarifa sahihi na za wazi(transparency) ili kumwezesha mtumiaji kumonita matumizi ya kifurushi chake.

Malalamiko ya watu ya kutumia vifurushi chini ya kile walichonunua yanaongezeka siku hadi siku. Kuwaachia makampuni ya simu wao wawe ndio wauzaji wa vifurushi, na wao hao hao ndio wakueleze umetumia nini,kama umemaliza au hujamaliza, huku wewe mteja ukiwa kipofu/gizani ukisubiri kupokea lolote wanalolisema wao, kupigwa hakuwezi kukwepeka.

Waweke mfumo ambao wao pamoja na mteja watamonita matumizi ili mteja aweze kuhoji. Teknolojia imekua hili ni dogo sana.

JAMBO LA NNE. Haki ya kuhamisha kifurushi.

Nimesema hapo juu kifurushi ni mali yako na ndo maana unailipia pesa na hivyo kuwa na haki ya kuitumia kwa uhuru.

Kwa msingi huu makampuni ya simu ni lazima yaweke mfumo unaomwezesha mtu kumhamishia mtu mwingine kifurushi kama ilivyo kwenye muda wa kawaida wa maongezi. Maana yake nikinunua kifurushi cha 1000 labda dakika 10 za maongezi, Mb 100, na sms 50.

Niwe na uwezo wa kumgawia yeyote ninayemtaka kiasi cha muda wangu wa maongezi,sms au Mb. Na hii inafanyika nchi nyingi na inawezekana zaidi kugawiana watu wa mtandao mmoja.Tunahitaji uhuru huu kwetu.

JAMBO LA TANO. Haki ya kupewa tahadhari kuhusu kifurushi au muda wa hewani unapokaribia kuisha. Kuna makampuni wana huduma hii lakini wanaitoa kwa hiari sana na wengine wameacha kabisa. Wengine wanatoa tahadhari muda unapoisha na sio unapokaribia.

Tunataka watoe unapokaribia ili mtu ajipange. Ni haki mtu kupewa tahadhari wakati akizungumza,akiwa kwenye mtandao, au sms, kuhusu dakika zake kukaribia kuisha. Sio sahihi wala ustaarabu simu kukatika ghafla bila tahadhari.

Na wanafanya hivyo maksudi wakijua unapokatakiwa na mawasiliano ghafla ni lazima tu utakuwa hujamaliza haja yako na hivyo utalazimika kuongeza vocha ili umalizie na wao wapate mauzo zaidi.

Wanajua ukipewa tahadhari unaweza tu kufupisha mazungumzo yako na wakati simu inakatika ukawa tayari umemaliza na hivyo usihitaji tena kuongeza vocha. Tabia za hovyo kabisa za kuviziana.

Unawezaje kunipa tahadhari ya muda kuisha ukashindwa kunipa ya muda kukaribia kuisha. Hili nalo tunataka lifanyiwe kazi.

SHERIA
Mambo haya kwa ujumla wake ni kinyume na Katiba ya JMT Ibara ya 18( c ) inayotaka uwepo wa mawasiliano bila kuingiliwa, lakini yanakiuka Kanuni za Kielektroniki na Mawasilano ya Posta kuhusu viwango vya Tozo GN. No 22/2018 hasa Kanuni ya 4 ( 1na 2) inayotaka viwango vyote vya tozo za simu kuwa vya haki na kadri(just and reasonable), yanakiuka Kanuni ya 4 ya Kanuni za Kielektroniki na Mawasiliano ya Posta GN No.61/2018 kuhusu kumlinda mlaji inayotaka mlaji kupewa taarifa kwa usahihi ya matumizi ya huduma muda wote, yanakiuka Sheria ya Ushindani namba 8/2003 inayotaka mtoa huduma kutoa huduma kwa kuzingatia zaidi maslahi ya watu wa hali ya chini, na sheria nyingine nyingi zimekiukwa.

Na tuelewane vizuri hapa, hakuna kitu kinaitwa VIGEZO NA MASHARTI KUZINGATIWA. Sheria iko wazi kuwa neno,maneno,sentensi au msemo wowote wenye lengo la kusigina haki ya mtu/watu ni batili.

Basi nitaviomba vyombo vya maamuzi vitusaidie kuyaweka sawa haya matano.Tutazidi kupeana taarifa kadri inavyokwenda.
Dah! Elfu sitini kwa wiki moja nailikuwa iwe kifurushi cha mwezi! Sitasahau!
 
Suala hili lilianzia KENYA kwa baadhi ya wadau kuishitaki safaricom, na wako katika mchakato mzuri wa kuifanikiwa. Ni vizuri kuAdapt walichokifanya wakenya but ushauri wangu kwako inabidi ufuatilie kwa undani kuhusu business law ya telecommunications company kwasababu na wao wenyewe wana-operate kwa sheria zao compared to their business strategies.

Ni wazo zuri but you need to do follow up,otherwise utafeli mahakamani, kingine jaribu kucheki na wakenya strategy yao against safaricom
 
Nilijiuliza sana inakuwaje unanua bundle hata ujalitumia kutokana na ubisy unambiwa limexpire kwangu mimi nachukulia kama ujanjajanja.Bando nikishanunua sipaswi kufungwa na mda wa kulitumia mimi napaswa nitumie mpaka liishe.Wakili tuwakilishe vema.
 
Unajua iko hivi wanapokupa dakika 20 kwa shilingi 1000 maana yake wamekupa chini ya bei halisi Yaani wamekupa dakika moja kwa shilingi 50 sawa Na sekunde moja kwa shilingi 0.833
wakati uhalisia ni shilingi 400 kwa dakika moja Yaani Shilingi 6.66 kwa sekunde sasa kwa vile ni offer ndio maana wanapanga muda ili kujinufaisha Na wao
Yaani iwapo wateja kumi wakijiunga Na wote wakatumia muda wao kamili basi imekula kwao Lakini wakatumia nusu tu basi na wao wanafaidika pia ni Kama bahati nasibu vile
Haya ni maoni yangu tu Nadhani tujiandae Na majibu kama Hayo kutoka kwao
 
Unajua iko hivi wanapokupa dakika 20 kwa shilingi 1000 maana yake wamekupa chini ya bei halisi Yaani wamekupa dakika moja kwa shilingi 50 sawa Na sekunde moja kwa shilingi 0.833
wakati uhalisia ni shilingi 400 kwa dakika moja Yaani Shilingi 6.66 kwa sekunde sasa kwa vile ni offer ndio maana wanapanga muda ili kujinufaisha Na wao
Yaani iwapo wateja kumi wakijiunga Na wote wakatumia muda wao kamili basi imekula kwao Lakini wakatumia nusu tu basi na wao wanafaidika pia ni Kama bahati nasibu vile
Haya ni maoni yangu tu Nadhani tujiandae Na majibu kama Hayo kutoka kwao
Nonesense
 
Kuna kitu watu wengi hawakijui mitandao ya simu haipati hasara kwenye vifurushi kuanzia sms, dakika na Mbs hii ni mtego wa kurudisha gharama za equipment installation, kiuendeshaji (maintanance na operation costs) zirudi na cha juu ambayo ndiyo faida yao so huu mchezo wameuzoea hapa Tanzania ndiyo maana 3G tunadanganywa ni 4G waliowahi kutumia data abroad wanaelewa
 
watu wanapenda bure Sana Lakini ukweli ni kwamba gharama za simu hapa ukilinganisha Na nchi nyingine sie tuna nafuu mara mia kuliko Wengi ne
basi sijui Tunakwama wapi
 
Bashir Yakub,
Well done msomi wetu. Mimi binafsi niko tayari kuunganishwa/kujiunganisha kwenye hii kesi ya kudai hizo haki zinazokiukwa na haya makampuni ya huduma au hujuma za mawasiliano. Halafu, kuna wakati huwa nashanga na kujiuliza, kwani mambo kama hayo uliyoanisha hapo juu, kweli hawa ndugu zetu wa TCRA NA TUME YA HAKI ZA WATEJA WA MAWASILIANO, hawayaoni au hawayajui au wanayafumbia macho kwa maslahi yao wenyewe? Tafadhari zidi kutupa feedback on the development of this important issue. Asante sana msomi.
 
Tanzania inaongoza kwa kutoza viwango vikubwa vya intaneti katika nchi za Afrika Mashariki.
Kwa mujibu wa cable.co.uk,Zimbabwe inangoza duniani kwa na gharama za intaneti ambapo gigabaiti 1(1GB) inagharimu dola za kimarekani 75.2 (TZS.172,847),ikifuatiwa na Equatorial Guinea dola za kimarekani 65.83.
India inaongoza kwa kuwa na kiwango kidogo ambapo1GB ni dola za kimarekani 0.26 (TZS.598).
Huku Tanzania ikiongoza kwa gharama kubwa Afrika Mashariki na Kati.
68340372a2a570fe67556c838074c10b.jpeg
 
Ndugu Bashir Yakub nafurahi kugundua kuwa Lengo lako ni kuwa mmoja wa wapigania haki za wanyonge. Iko gudi.

Nina mashaka na hoja zako (numbered) Kwa nini?.... Ni kwamba umefaninisha kifurushi tunachokupatia (mf. Wajanja night) na vifurushi vya luku, maji nk of which is quite wrong. Kivipi.... Naomba ukumbuke kifurushi tunachokupatia kama voda/tigo/airtel ni OFFER ambapo usipotaka kutumia offer ninayokupa utalazimika kutumia muda wako wa hewani wa kawaida (prepaid or postpaid ). So it's just an offer ambayo ni tofauti na luku au dawasa
Sasa mpaka ukae mkao wa biashara ndo utaelewa ila uking'ang'ania uwakili wako tu kwa hoja hizo ulizoainisha utakusumbua.
Sasa basi kama offer tuna uhuru wa kucustomize offer zetu, kivipi? Ni kwa kukuwekea pia span ya kifurushi. So ni kitu unayoeza kuona from business point of view.

-Swala jingine umezungumzia haki kutochanganya kifurushi na muda wa kawaida wa hewani. Sasa anayechanganya hayo ni mimi (voda/tigo ) au wewe?
Wewe ndo unayeruhusu kwenye simu yako au device yoyote similar to that maana kwenye simu ndo unaeza turn ON or OFF data. Ukiacha ON mimi kama service provider nitatambua kuwa bado unahitaji kuwa mtandaoni ninachokifanya naangalia kama unavigezo kwa aidha kifurushi au salio lako kawaida kama vipo utaendelea kusurf tu bablai. Sasa unataka nikuamulie tena eti sasa ivi Zima data kifurushi kimeisha haah! !!

Sasa wengi jukwaani humu watakusupot kwa sababu (kwa kutotambua wajibu wao) walipigwa na mitandao hiyo.
Hizo sheria unazozijua ukitumia vibaya tunakufunga wewe mwenyewe. So try to have wide overview/perception of your topic.

Kuna eneo uko sahihi nimeona nisilizungumzie.

Thanks
 
Back
Top Bottom