Uchaguzi 2020 Bashiru: Kuna mtu unakuta ndani ya miaka mitano tu kapata vyeo vikubwa viwili kwa mpigo halafu kabla hajakomaa pale, anataka Ubunge. Sigombei

Uchaguzi 2020 Bashiru: Kuna mtu unakuta ndani ya miaka mitano tu kapata vyeo vikubwa viwili kwa mpigo halafu kabla hajakomaa pale, anataka Ubunge. Sigombei

The Sheriff

JF-Expert Member
Joined
Oct 10, 2019
Posts
747
Reaction score
2,112
BASHIRU.jpg

Kuhusu kutenda haki kwa wagombea wote, Dkt. Bashiru amesema:

”Nadhani kama umemsikiliza Mwenyekiti wetu jana wakati anaapisha baadhi ya viongozi, alisema yeye kama mwenyekiti wa chama hana mgombea, na akaenda mbali kusema Makamu wa Rais, hana mgomnea; akamtaja Waziri Mkuu, hana mgombea; akamtaja Makamu Mwenyekiti, Mzee Mangula, hana mgombea; akanitaja mimi, sina mgombea.”

“Matarajio yetu, viongozi wanaokaa kwenye vikao vya uteuzi wana dhamana kubwa ya kutenda haki kwa wagombea wote. Hata kama ni mkeo, hata kama ni mwanao, hata kama ni rafiki yako mulisoma wote, hata kanma ni tajiri yako kakuajiri – unalinda maslahi ya chama siyo maslahi ya mgombea. Na kwahiyo upo upande wa chama, si upande wa wagombea”

Kuhusu wanaoachia nafasi zao na kuusaka ubunge, Dkt. Bashiru amesema:

"Na ndiyo maana hairuhusiwi mtu anayegombea kushiriki katika vikao. Naomba nitaje jambo ningependa mtusaidie. Kuna baadhi ya wenyeviti wetu wa mikoa; sasa hivi wamefikia watatu -- mikoa mitatu. Wanaopaswa kukaa kwenye vikao vya kamati za siasa za mkoa (ndiyo wenyeviti); Kamati ya Usalama na Maadili (ndiyo wenyeviti); Halmashauri Kuu ya Mkoa (ndiyo wenyeviti). Sasa wameamua wao waache kiti wajadiliwe badala ya kuwajadili wengine. Na wakati wanaomba uongozi walikabidhiwa dhamana ya kusimika uongozi madhubuti wa kukiletea chama ushindi. Sasa wamaemua kuingia kwenye foleni ya kujadiliwa."

Kanuni yetu inasema:

Mwanachama atakuwa na haki ya kugombea nfasi yoyote ya uongozi lakini edapo kugombea nafasi nyingi kutasababisha kuzorota kwa uhai wa chama, hatateuliwa.

"Una haki ya kugombea lakini vikao vikisema wewe unafaa zaidi kuwa mwenyekiti, na ukitoka kwenye uenyekiti mkoa utayumba, sasa unafaa uenyekiti kuliko ubunge, unaweza ukaambiwa kaa kwenye uenyekiti kwa maslahi ya chama na uhai wa chama. Na wanajua hayo hao viongozi wetu."

“Ukishakuwa kiongozi hutakiwi kuwa na tamaa, ndiyo ujumbe Mwenyekiti ametuambia. Unatakiwa kutosheka, na ni moja ya sifa za kiongozi. Tosheka na dhamana uliyopewa na ukamilishe hiyo dhamana, upimwe kwadhamana hiyo – siyo unatangatanga tu.”

“Ni haki yake, ni haki yake; lakini ajue angepimwa vizuri kwa ngazi yake ya ukuu wa Mkoa. Najua baadhi ya wakuu wa mikoa ambao wamekaa kwa muda mrefu na majina yale utafikiri ni cheo yale. Nsa Kaisi watu wengine wangedhani kuna cheo kinaitwa Nsa Kaisi, lakini kwa kwasababu amekaa kwenye nafasi ile na ameitumikia kama Mkuu wa Mkoa.”

“Kuna mtu unakuta ndani ya miaka mitano tu kapata vyeo vikubwa viwili kwa mpigo alafu kabla hajakomaa pale, anataka ubunge. Ni haki yake lakini ni vizuri kujitathmini na kujitafakari.”

Msimamo wake wa kutogomea nafasi yoyote

Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi Dr. Bashiru Ally Kakurwa ameweka wazi msimamo wake wa kutogombea nafasi yoyote katika Chama hicho kwani ameridhika na nafasi aliyonayo.

“Mimi sigombei na siwezi kugombea, nimeshakuwa Katibu Kuu nagombea cheo gani?, cheo gani cha maana kuliko kazi hii ya kusimamia haki katika Chama” Katibu Mkuu CCM, Dkt.Bashiru

“Ukishakuwa kiongozi hutakiwi kuwa na tamaa ndio ujumbe Mwenyekiti ametuambia, unatakiwa kutosheka ndio moja ya sifa za kiongozi, tosheka na dhamana uliyopewa na uikamilishe hiyo dhamana na upimwe kwa dhamana hiyo sio unatangatanga tu” Dkt. Bashiru Ally
 
Kamuiga Dk John Mnyika.
Mnyika tena! Unalinganisha Katibu Mjuu wa CCM, chama tawala na wa vyama vingine vya siasa?

Isitoshe kutakuwa na mabadiliko ya chama kikuu cha upinzani, kwa mwelekeo wa sasa wa siasa Tanzania hivyo CHADEMA kubaki chama kidogo tu kusichokuwa na 'impact" kisiasa nchini
 
Bashiru waache watu watimize ndoto zao, kama wewe unawaona hao watu wana vyeo vikubwa wenzako wanajiona bado hawajafika wanapopataka, vumilieni kutofautiana mitazamo huo ndio ukomavu wa kisiasa, sio kuhubiri tu kwa maneno chama kikongwe.
 
Wanajua hao. Wanajua jinsi ya kubebana. Tuendelee kufanya kazi za kutupa riziki wakuu angalao na sisi tuinjoy mema ya nchi
 
Mbona nyingi mliacha ajra zenu mkaingia kwenye siasa huko mkisababisha upungufu katika sehemu mlizokuwa mmeajiriwa?
 
Nimemkumbuka Nape, hivi kachukua fomu?

Yuko kimya.
Duniaaa, haina huruma eeeh! ×2

Nimejikuta namuimbia Nape kawimbo.
Anapitia kipindi kigumu sana awamu hii. Mara anyooshewe mguu wa kuku hadharani, hatujakaa sawa anapiga magoti kuomba radhi, na Sasa anajificha hata kuchukua fomu.

Nape, ooooh Nape!
 
Mnyika tena! Unalinganisha Katibu Mjuu wa CCM, chama tawala na wa vyama vingine vya siasa?

Isitoshe kutakuwa na mabadiliko ya chama kikuu cha upinzani, kwa mwelekeo wa sasa wa siasa Tanzania hivyo CHADEMA kubaki chama kidogo tu kusichokuwa na 'impact" kisiasa nchini

Tofauti kubwa ya katibu mkuu wa ccm na cdm ni kuwa wa ccm anaweza kupata mbeleko ya vyombo vya dola, tena kwa matumizi hasi. Lakini katika uga wa siasa kwa maana ya siasa halisi, the difference is minimal.
 
CCM kila kitu wanafanya kwa maslahi ya mwenyekiti na chama, hakuna sehemu utaona wanasema kwa maslahi ya watanzania. A gang of wicked selfish monsters wanajali matumbo yao tu. Nchi iko palepale haiendelei. Africans kazi ipo sana kutoka kwenge umaskini sio leo wala kesho kwa akili za kishenzi hivi
 
Tofauti kubwa ya katibu mkuu wa ccm na cdm ni kuwa wa ccm anaweza kupata mbeleko ya vyombo vya dola, tena kwa matumizi hasi. Lakini katika uga wa siasa kwa maana ya siasa halisi, the difference is minimal.
Hoja ya Chama Tawala kutumia vyombo vya Dola ni hoja hafifu sana ya mwanasiasa aliyeishiwa nguvu za kisiasa kushawishi wapiga kura.

Ni ukweli mtupu wapiga kura wengi, kwenye nchi maskini au zinazoendelea, wanapenda maendeleo ya vitu na nadharia. Ni kwa sababu hiyo wagombea, kwenye kampeni, watatoa ahadi kibao za maendeleo ya vitu.

Uongozi wa CCM, katika miaka 5 ya utawala wa Serikali yake inayoongozwa na Magufuli, umelitambua hitaji hilo la wapiga kura, wakalisimamia kwa umakini kiasi kwamba kero nyingi za wapiga kura zimeshughulikiwa. Kwa ufasaha zaidi, wametumia vyombo vya Dola, siyo kukandamiza upinzani, ila kuhakikisha watendaji wa Serikali wanatimiza wajibu wao. Matokeo yanaonekana wazi.
 
KUGOMBEA N HAKIYAO
KUPITISHWA NA CHAMA HAKIYAOO
KUCHAGULIWA HAKI YA WANANCHI

HIZI KKK WAJULISHENI WAGOMBEA WOTE WA CCM
CCM OYEEEE
 
Bashiru waache watu watimize ndoto zao, kama wewe unawaona hao watu wana vyeo vikubwa wenzako wanajiona bado hawajafika wanapopataka, vumilieni kutofautiana mitazamo huo ndio ukomavu wa kisiasa, sio kuhubiri tu kwa maneno chama kikongwe.
Ukitolewa Mavumbin kubali kutoka ulipo kuta husu walio kutoa mavumbin ila ukijifanya unaweza basi una achwa urud Mavumbini this time utakuwa matope kwa huyo kijana wa mkoa hana mvuto na kamwe hatokuwa nao this time atarud topeni vyombo vya habari vitakuwa mbali naye kama maji na mafuta
 
Hoja ya Chama Tawala kutumia vyombo vya Dola ni hoja hafifu sana ya mwanasiasa aliyeishiwa nguvu za kisiasa kushawishi wapiga kura.

Ni ukweli mtupu wapiga kura wengi, kwenye nchi maskini au zinazoendelea, wanapenda maendeleo ya vitu na nadharia. Ni kwa sababu hiyo wagombea, kwenye kampeni, watatoa ahadi kibao za maendeleo ya vitu.

Uongozi wa CCM, katika miaka 5 ya utawala wa Serikali yake inayoongozwa na Magufuli, umelitambua hitaji hilo la wapiga kura, wakalisimamia kwa umakini kiasi kwamba kero nyingi za wapiga kura zimeshughulikiwa. Kwa ufasaha zaidi, wametumia vyombo vya Dola, siyo kukandamiza upinzani, ila kuhakikisha watendaji wa Serikali wanatimiza wajibu wao. Matokeo yanaonekana wazi.

Nikikuambia kuwa ccm wanatumia mabavu ya vyombo vya dola kuongoza kwa shuruti, sina chembe ya shaka na maelezo yangu. Kutekeleza mipango ya maendeleo ya vitu au watu, ni wajibu wa serikali yoyote, hata wakoloni walifanya hilo. Kwamba vyombo vya dola vimetumika kukandamiza upinzani, hilo halihitaji hata kuishi hapa nchini kujua hayo.
 
Back
Top Bottom