UWEKEZAJI KATIKA BANDARI UNA MANUFAA MAKUBWA KIUCHUMI: BASHUNGWA
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambeye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa amesema maamuzi ya Serikali kuhusu Uwekezaji na uendeshaji wa bandari ya Dar es Salaam utaongeza ufanisi kiutendaji na manufaa kiuchumi wa nchi kwa kuongeza Mapato.
Ameeleza hayo wakati wa mwendelezo wa ziara yake jimboni ya Kuongea na Wananchi na kukagua miradi ya maendeleo katika Kata za Chonyonyo, Chanika, Rugera na Kihanga wilayani Karagwe.
“Tanzania tuna bandari ambayo ufanisi wake ulikuwa mdogo katika uendeshaji, ndio maana serikali ikaamua kutafuta mwekezaji ambaye ataongeza ufanisi ili tuweze kupata mapato zaidi ambayo yataenda kutoa huduma za kijamii kwa Watanzania” amesema Bashungwa
Bashungwa amewatoa hofu Wananchi wa Mkoa Kagera kwa kueleza kuwa bandari ya haiuzwi wala haibinafishwi bali Serikali inaleta mwekezaji ambaye ataendesha bandari hiyo kwa makubaliano yatakayoongeza ufanisi kiutendaji.
“Ndugu zangu Wananchi naomba tuyapuuze yanayosemwa huko mitandaoni, katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi tuliahidi kutengeneza ajira milioni nane ndio maana tumeamua kukaribisha uwekezaji utakaozalisha ajira kwa Watanzania”
Aidha, Bashungwa amesema Uwekezaji ni moja ya mkakati wa kupanua wigo wa vyanzo vya mapato ili Kondoa usumbufu kwa Wananchi kwa kutoweza tozo nyingi ambazo zingelitumika kutekeleza miradi mbalimbali nchini.
Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ambeye pia ni Mbunge wa Jimbo la Karagwe, Innocent Bashungwa amesema maamuzi ya Serikali kuhusu Uwekezaji na uendeshaji wa bandari ya Dar es Salaam utaongeza ufanisi kiutendaji na manufaa kiuchumi wa nchi kwa kuongeza Mapato.
Ameeleza hayo wakati wa mwendelezo wa ziara yake jimboni ya Kuongea na Wananchi na kukagua miradi ya maendeleo katika Kata za Chonyonyo, Chanika, Rugera na Kihanga wilayani Karagwe.
“Tanzania tuna bandari ambayo ufanisi wake ulikuwa mdogo katika uendeshaji, ndio maana serikali ikaamua kutafuta mwekezaji ambaye ataongeza ufanisi ili tuweze kupata mapato zaidi ambayo yataenda kutoa huduma za kijamii kwa Watanzania” amesema Bashungwa
Bashungwa amewatoa hofu Wananchi wa Mkoa Kagera kwa kueleza kuwa bandari ya haiuzwi wala haibinafishwi bali Serikali inaleta mwekezaji ambaye ataendesha bandari hiyo kwa makubaliano yatakayoongeza ufanisi kiutendaji.
“Ndugu zangu Wananchi naomba tuyapuuze yanayosemwa huko mitandaoni, katika Ilani ya Chama Cha Mapinduzi tuliahidi kutengeneza ajira milioni nane ndio maana tumeamua kukaribisha uwekezaji utakaozalisha ajira kwa Watanzania”
Aidha, Bashungwa amesema Uwekezaji ni moja ya mkakati wa kupanua wigo wa vyanzo vya mapato ili Kondoa usumbufu kwa Wananchi kwa kutoweza tozo nyingi ambazo zingelitumika kutekeleza miradi mbalimbali nchini.