Elections 2010 Batilda afunga kampeni NMC

Ngongo

Platinum Member
Joined
Sep 20, 2008
Posts
20,654
Reaction score
35,887
Wakuu Mama Dr Batilda amefunga kampeni zake uwanja wa NMC kwa viroja vya aina yake.Kabla ya mkutano kuanza kuliwa na maandamano makubwa ya magari,pikipiki,baiskeli na waenda kwa miguu.

Nimeshuhudia kwa macho yangu madereva wa pikipiki wakipewa sh 5,000/= kabla ya kuanza maandamano na kumaliziwa sh 2,000/= mwisho wa maandamano.Mmliki wa kampuni ya Riverside alihusika bila shaka yoyote kutoa fedha kwa madereva wa pikipiki na baiskeli nashangaa sana TAKUKURU wanafumbia macho vitendo vya rushwa kwakuwa vinafanywa na MwanaCCM.

Riverside ilihusika pia na upelekaji wa watu kutoka Arusha kwenda Karatu kwenye mkutano wa Kikwete majuzi nashindwa kuelewa Mama Riverside ana interest gani na CCM labda wenye kujua connection zake wanaweza kutusaidia.

Najiuliza Lyimo au Lema wangefanya upuuzi anofanya Batilda tungesha wasahau siku nyingi.Sheria ya uchaguzi ipo kwaajili ya kundi fulani na kwa faida ya kundi fulani wenye akili tumeshagundua CCM haiwezi kuongoza Tanzania.

Mungu ibariki Tanzania kesho mpinzani yoyote anyakue ubunge Arusha mjini hata Lema mwenye elimu duni akishinda sitachukia.

Naomba kuwasilisha.
 
Mungu ibariki Tanzania kesho mpinzani yoyote anyakue ubunge Arusha mjini hata Lema mwenye elimu duni akishinda sitachukia.

Naomba kuwasilisha.

Elimu yetu ya kuazima ya kikoloni unafikiri hata imetusaidia sana?
 
amemaliza kampeni kwa aibu ....alipita mitaa ya stand ndogo na msafara wake alizomewa sana....walivyoona maji yamezidi unga washabiki wake wakaanza kupiga watu...kuna kijana mmoja aliumizwa...lakini kwa sababu chadema ni chama cha watu....simu ilipigwa haraka kwa mbunge Lema na mara moja alifika eneo la tukio na kumchukua kijana na kumpeleka hospitali.......hakika Lema ndio mbunge wa Arusha mjini
 

hata leo magari yake yalikuwepo kwenye msafara.....sio yeye tu hata mmiliki wa Triple A na wengineo wengi ambao wanakikumbatia chama cha CCM kwa interest zao wanazojijua wenyewe walikuwepo.....kilichonichekesha ni kuwa baadhi ya wale waliokuwepo kwenye hayo magari ya ccm walikuwa wanaonyesha alama ya chadema.....hapo walinishangaza kidogo.....sikuelewa
 
naamini wana wa arusha hawadanganyiki kwa hila iwayo yoyote ile!:nono:
 

Mdau wakaribu kanipigia simu na kiniambia kumbe Lema alipita huko na vijana wa batilda wampa zenge na matusi juu?

Pia hata hizo 2000/= pia ati ilikuwa kasheshe kuwapa hao watu wa pikipiki nasikia huyo mama aligoma akadhani wata mla changa la macho na alikuwa akidai kuwa pesa kaitoa mfukoni kwake na anauchungu nayo.

Hii kuingiza matajiri kwenye chama ni tatizo sana sasa kama ametoa hizo kauli mbaya itakuwaje.

Kuna jambo moja tu napenda kuwashauli wana CCM pale viongozi wao wanapo kosea waambiwe ukweli na wakiendelea kuficha kweli 2015 itakuwa ngumu kwao au CCM kusambalatika kwani kuna mapungufu mengi zana kwenye uongozi wa CCM na ndio maana wamekutana na challenge kubwa sana kwenye uchaguzi huu. wajiandae mapema tukiacha siasa za ushabi kuna wakati mgumu sana kwa CCM esp UVCCM ispo kaaa na kuongea kwa lugha mmoja wamepoteza majimbo mengi 2015 kwani wenzao CHADEMA wanajipanga sasa na wanakuja kwa kasi.

CCM ombeni sana huko vijiji wasije ielewa democrasia kwa halaka kwani wakiisha jua vyema basi ndio mwisho wa CCM

 

Asante sana Preta, Mdau wangu toka Mbeya ananiambia kwamba Sugu ndiye mbunge mteule wa Mbeya Mjini

Jamani vipi Regia? I wish her all the best
 
Asante sana Preta, Mdau wangu toka Mbeya ananiambia kwamba Sugu ndiye mbunge mteule wa Mbeya Mjini

Jamani vipi Regia? I wish her all the best


kwa asilimia 100 Jimbo la Uchaguzi la Mbeya vijijini LIMEKOMBOLEWA toka mikononi mwa wakaloni!

Rasmi sina kigugumizi kusema kuwa Tambwee Shitambala ndiye Mbunge mpya wa wana Mbeya vijijini!
 
Batilda hawezi kushinda Ubunge Arusha. Mbunge wa arusha ni G. Lema na Elimu yake inatosha kabisa kutuongoza kwa sababu hata hao wenye elimu kubwa CCM wamesaidia nini cha maana.

Hizo hela alizotoa ni hasara na zitampa tu pressure kwani hata waliokuwa kwenye msafara wengi wao hawatampigia kura.
Leo vifodi vya safari za mjini- Kijenge na Moshono zilipiga kampeni ya aina yake pale zilipoamua kuchukua tu abiria waliokuwa tayari kuwa pa CHADEMA kura kesho. Walisikika wakisema" kama wewe hupigii CHADEMA kura usipande humu"
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…