Tatizo jamaa hawana identity yoyote kama nchi hapa Africa. Yaani ukienda SADC Kenya haeleweki kama nchi zaidi ya kukaa upande wa mabeberu, shombo nyingi. ULIZIA TZ ina alama kwenye independence yao, post independence relations, wameshirikiana mambo mengi, kuna nchi SADC Comoro, Seychelles post Independence zishawahi saidiwa kutuliza Mapinduzi via Tz.
Njoo EAC, Burundi yupo na Tz kuzima chokochoko za PK, PK alipita Tz kusaka ukombozi Rwanda, MUSEVENI ndio huyo aliwekwa Via Kagera War, DRC Kabila kapitia mafunzo huku JKT na TMA Monduli.
Nenda North Africa jiulize Ghaddafi alimjuaje Nyerere hadi kumuweka kwa Shati.
Egypt kipindi cha Nasser kipindi ambacho Kunyan walikua busy kuchomea viongozi wengine no msaada.
Leo kuna jitu linakuja Kuomba kura na kuna nchi nyingi halimjui kabisa kwenye vitabu vyao. Na atapata kweli?
I say nikikumbuka hivyo vyote we have fallen low na viongozi waliopo yaani kuendekeza ujinga badala ya kucapitalize influence maana ilikua kubwa walitakiwa kucapitalize sio kuitumia ovyo na kuruhusu wengine waitie doa benefits of influence mfano mzuri ni South Africa. Badala yake wanatumia machawa.kuponda zile sera za Nyerere zilizowapa influence na wakashindwa itumia.
Badala ya Ubalozi kuhakikisha watanzania wote wapo documented na kupewa mamlaka husika kuepusha kina Nyang'au na Mataifa Mengine ya EA kujifanya watanzania wakiingia SA kwa kutumia loophole mpaka nasi tukaonekana wasumbufu.
Same kwa Passport yetu, nakumbuka nchi za Nordic zilikua na free visa for Tanzania sababu ya Non-Aligned Movements (NAM) same vision yao ya Neutrality kingine hatusafiri sana na hawatuoni sana hivyo kufanya for Africa Passport yetu kuwa na nguvu kwa kuwa kama kawa upuuzi ukazidi Wahindi, Wanigeria wakawa wanachukua passport za Tz unapata free pass ila ukiwa kwa ndege unaflash passport mpaka shirika la ndege wakalalamika visa free bye bye.
Situation naona inaelekea tena China.
I believe tungekua tunacapitalize Influence yetu tusingekua hapa.
Mfano unamlea KABILA unampa mafunzo ya Kijeshi alafu anakua rais upo upo tu.