Batuli Actress aka Cleopatra Nabisha Hodi

Salaam sana wana Jamiiforum

Nimeona ni vema nami nijiunge JF ili kuweza kujifunza mengi na kupata mawazo mbalimbali ya kimaendeleo na ya kujenga.

Mimi ni Actress wa Filamu za Kitanzania.

Asanteni sana.

karibu sana.
wewe ni mrembo balaa, na pia ulipendeza sana kwenye uzinduzi wa filamu ya LULU.
Napenda unavyoigiza.kip it up.
NAOMBA UWE BALOZ WA KUZUIA WASANII WASITUMIE MIKOROGO!
 
Salaam sana wana Jamiiforum

Nimeona ni vema nami nijiunge JF ili kuweza kujifunza mengi na kupata mawazo mbalimbali ya kimaendeleo na ya kujenga.

Mimi ni Actress wa Filamu za Kitanzania.

Asanteni sana.

una kimbelembele cha kujibu kila swali,mengine uyapotezeege,mwanamke anayemkubali kila mwanaume anapunguzaga thamani yake,karibu jf,watata kama sisi hatukosi humu.
 

duh umeniamasisha nianze kukufatilia maana unaonekana unajitambua flani,,,ujue mie nimetokea kuwadharau sana bongo movie...huwezi amini batuli imefikia hatua nikiingia sehemu nikikuta wanaangalia filamu ya kibongo nageuzia mlangoni kwa hasira..ila kusema ukweli nimekupendaje ghafla,,,bongo movie unajua hadi habari za soko la hisa!!!sikuwai kutegemea ilo.


msalimie Malkia nasikia nae ameanza kunusa,,mshaurini aache huo sio ujanja amuulize kiuno bila mfupa.
 
Batuli aka Cleopatra,
zamani nilikua napenda sana maigizo ya kitanzania enzi za kina mzee Jengua, Swebe, Muhogo mchungu, Siyawezi na wenzie kina Uledi (igizo la damu nzito), nk.

Tatizo lilianza pale zilipoibuka hizi zinazoitwa Bongo Movie. Yaani watu hawajui/hawawezi kuvaa uhusika, pia wanaojiita wasanii/waigizaji wa hizi filamu naweza kusema kua ni wezi kupitia kazi zao. Ndiyo ni wezi kwa maana kua unakuta filamu imechezwa nzima lakini inakatwa vipande na kuitwa part 1 na part 2 lakini ukiangalia hakuna ulazima huo.

Kituko kingine utakuta filamu ni ya Kitanzania, imechezwa mazingira ya Kitanzania, lugha iliyotumika ni Kiswahili lakini JINA LA FILAMU NI KINGEREZA mfano "fake smile" (waweza eleza ilikuaje mkaiita hivyo badala ya kutumia Kiswahili?).

Natamani yarudi maigizo ya kina Muhogo mchungu kuliko hizi bongo movie. Vinginevyo karibu Jamiiforums.
 
Last edited by a moderator:
Karibu jf but tunaomba mpunguze kuvaa nguo za nusu uchi...sisi tunataka kazi na si maungo yenu...waambie hao....maana nguo za club ndo wanazivaa kwenye shooting sijui ndo mauzo..mpk ney akawaamba makahaba wenye viwango wako bongo movie...achen
 

Wewe na Rihama nawafeel kinoma pamoja na mjane wa Marehemu Sajuki. Ila imekuwaje jamaa ktk hii thread kakuulizia AY na sio msanii mwingine?
 
Last edited by a moderator:

Yobnesh ni jina la asili ya wapi?

Le Mutuz ni rafiki yako?
 
karibu sana.
wewe ni mrembo balaa, na pia ulipendeza sana kwenye uzinduzi wa filamu ya LULU.
Napenda unavyoigiza.kip it up.
NAOMBA UWE BALOZ WA KUZUIA WASANII WASITUMIE MIKOROGO!

Asante sana kwa kunitia moyo.

Pia nitajitahidi kufanya hivyo.
 
Last edited by a moderator:
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…