BAVICHA na CHADEMA kazi mnayo

BAVICHA na CHADEMA kazi mnayo

Cvez

JF-Expert Member
Joined
May 19, 2018
Posts
4,405
Reaction score
13,411
Katika moja ya mistake kubwa ilifanyika ni kuanza harakati za Katiba Mpya wakati wanachama wameparaganyika. Enzi za Mwendazake ilikua kufanya siasa ni dhambi kiasi ambacho wengi ya wapinzani waliamua kukaa kimya na kuendelea na maisha yao ya kila siku kwa usalama wao na familia zao. Walioendelea na siasa za upinzani ni wale pekee ambao siasa ni sehemu ya maisha yao ya kila siku.

Mungu si Athumani Mwendazake akaenda mwangaza ukaonekana kidogo ingawa kiuhalisia utawala bado ni ule ule japo huu una nafuu, na hapa CDM ndipo walipokosea badala ya kuwarejesha wale wanachama waliopotezea siasa. Wakajiingiza kwenye Katiba Mpya si kitu kibaya ila kuna hatua zilitakiwa zifuatwe kama kuzunguka mashinani na kufanya mikutano ya ndani ili kurejesha ari ya wanachama wao.

Ni kweli walianza kidogo na mikutano ya ndani kanda ziwa, ila ghafla wakabadilisha gia angani na kuingia na Katiba Mpya na hapa ndio waliharibu, najua CDM wengi watapinga.

Baada ya brain ya movement yote kupigwa pini sasa hivi ni kurukia kila ajenda ndani ya siku 7 hizi, walikua na ajenda ya ZZK, ikaja kukosoa Royal Tour, jana mchungaji Mwigira kawapa mjadala pia. Kesho huenda Rais akapiga selfie na wajukuu zake najua wataruka nayo pia. Kiujumla kila kitu shaghala baghala wanaishi kwa trends. Kwa mwendo huu CCM watawapa topic kila wiki ya kujadili na kuacha kufanya mambo ya msingi.​
 
Katika moja ya mistake kubwa ilifanyika ni kuanza harakati za Katiba Mpya wakati wanachama wameparaganyika. Enzi za Mwendazake ilikua kufanya siasa ni dhambi kiasi ambacho wengi ya wapinzani waliamua kukaa kimya na kuendelea na maisha yao ya kila siku kwa usalama wao na familia zao. Walioendelea na siasa za upinzani ni wale pekee ambao siasa ni sehemu ya maisha yao ya kila siku.

Mungu si Athumani Mwendazake akaenda mwangaza ukaonekana kidogo ingawa kiuhalisia utawala bado ni ule ule japo huu una nafuu, na hapa CDM ndipo walipokosea badala ya kuwarejesha wale wanachama waliopotezea siasa. Wakajiingiza kwenye Katiba Mpya si kitu kibaya ila kuna hatua zilitakiwa zifuatwe kama kuzunguka mashinani na kufanya mikutano ya ndani ili kurejesha ari ya wanachama wao.

Ni kweli walianza kidogo na mikutano ya ndani kanda ziwa, ila ghafla wakabadilisha gia angani na kuingia na Katiba Mpya na hapa ndio waliharibu, najua CDM wengi watapinga.

Baada ya brain ya movement yote kupigwa pini sasa hivi ni kurukia kila ajenda ndani ya siku 7 hizi, walikua na ajenda ya ZZK, ikaja kukosoa Royal Tour, jana mchungaji Mwigira kawapa mjadala pia. Kesho huenda Rais akapiga selfie na wajukuu zake najua wataruka nayo pia. Kiujumla kila kitu shaghala baghala wanaishi kwa trends. Kwa mwendo huu CCM watawapa topic kila wiki ya kujadili na kuacha kufanya mambo ya msingi.​
Huyu naye unaeza kuta kuna mtu anamuita '..Baba'.. Duh!
 
Huyu naye unaeza kuta kuna mtu anamuita '..Baba'.. Duh!
Toa hoja mkuu, mbona mko hivyo siku hizi humu jf? Badala ya kujibu kwa hoja unaingiza kejeli ili iweje? Ikiwa una hoja kuthibitisha si kweli asemalo mleta mada basi ziweke wazi mkuu.
 
Back
Top Bottom