Pre GE2025 BAWACHA Mbeya wamuunga mkono Lissu

Pre GE2025 BAWACHA Mbeya wamuunga mkono Lissu

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Mambo yanazidi kunoga wakati tunaelekea 2025.

===

Screenshot_20241213_191612_Instagram.jpg

Siku moja tangu Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tanzania Bara Tundu Lissu atangaze nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa katika mchakato wa ndani wa uchaguzi unaoendelea leo, Ijumaa Desemba 13. 2024 Baraza la Wanawake la chama hicho (BAWACHA) mkoa wa Mbeya limesema linamuunga mkono kwenye dhamira yake hiyo kwa kuwa anatekeleza haki yake ya Kikatiba.

Akizungumza na wanahabari mkoani humo, Mwenyekiti wa BAWACHA mkoa wa Mbeya Elizabeth Mwakimomo amesema yeye kama mwanachama na kama kiongozi anatambua kuwa hiyo ni haki yake ya msingi.

"Sio jambo baya yeye (Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara na mtia nia wa nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa) kugombea nafasi ya Mwenyekiti lakini ni utaratibu tu, ni utaratibu ambao unatakiwa kusubiriwa pindi uchaguzi utakapotangazwa watu watagombea kwa sababu chama chetu kina demokrasia" -Mwakimomo

Pia soma: Tundu Lissu atangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA

Akizungumzia suala la ukomo wa madaraka ambalo ni sehemu ya ajenda za Lissu, Mwenyekiti huyo wa BAWACHA mkoa wa Mbeya amesema suala hilo ni la Kikatiba, na kwamba Katiba ya chama hicho haijaweka ukomo wa madaraka badala yake imeacha wazi kwa kusema kuwa kila mtu anayo uhuru wa kugombea

"Kwenye hili suala la ukomo wa madaraka labda tuende kwenye mabadiliko ya Katiba yetu kwamba tuende tukabadilishe hicho kipengele ili kuwe na ukomo wa madaraka kama ni miaka miwili iwe miwili, kama miaka mitano iwe mitano, kwa hiyo suala la ukomo wa madaraka pia ni jambo jema" -Mwakimomo

Aidha, Elizabeth Mwakimomo amesema mtazamo wake anaona wazi kuwa Tundu Lissu yuko sahihi, kwa kuwa ni wengi wanataka kuona nafasi za Viti maalum vinakuwa na ukomo (Wabunge na Madiwani wa Viti maalum) ili watu wengine waweze kupata nafasi kwa sababu mara zote wamekuwa wakisema kila mmoja apate nafasi ya kupata nafasi ndani ya chama hicho

"Kwa hiyo inaweza kuwa miaka mitano, au miaka miwili basi, tuwe na ukomo isiwe miaka 10, miaka 20 kama mimi basi niwe mimi tu hapana, wakati kuna mtu mwingine pia hiyo nafasi anatakiwa akomazwe katika huo utaratibu" -Mwakimomo
 
bila mbowe hio chadema isingekuwepo lissu anashupaza shingo tu

akipewa anakiua chama hana busara
 
bila mbowe hio chadema isingekuwepo lissu anashupaza shingo tu

akipewa anakiua chama hana busara
Kwann mnageuza kua vita?Simple and clear hata kama umefanya makubwa mithili ya almasi,lazima utatoka na kupisha mawazo mapya ndo Dunia ilivyo
 
bila mbowe hio chadema isingekuwepo lissu anashupaza shingo tu

akipewa anakiua chama hana busara
Acha uoga mkuu, mabadiliko ni muhimu.
Ma ccm ni wahuni hayahitaji busara hata chembe...ni mwendo wa ubaya ubwela tuu!!.
 
Mwamba Mbowe katutoa mbali sana, lakini sasa ni wakati wa Tundu Lissu, sote tunajua tofauti ya Viongozi hawa wawili, Mwamba anapenda Siasa za Kistaarabu na uvumilivu kitu ambacho CCM inavitumia kama Advantage.

Kwa upande Lissu kama tumjuavyo ni Mtu wa Jino kwa Jino, Mkuki kwa Mkuki, Ngumi kwa Ngumi, Mapanga kwa Mapanga, Daadeki... 😂😁

1200px-Honey_Badger.jpg

Piga Mkuki anakuja tu mpaka unajifia au unakimbia muulizeni Mchato.
 
Wakuu,

Mambo yanazidi kunoga wakati tunaelekea 2025.

===


Siku moja tangu Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA Tanzania Bara Tundu Lissu atangaze nia ya kugombea nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa katika mchakato wa ndani wa uchaguzi unaoendelea leo, Ijumaa Desemba 13. 2024 Baraza la Wanawake la chama hicho (BAWACHA) mkoa wa Mbeya limesema linamuunga mkono kwenye dhamira yake hiyo kwa kuwa anatekeleza haki yake ya Kikatiba.

Akizungumza na wanahabari mkoani humo, Mwenyekiti wa BAWACHA mkoa wa Mbeya Elizabeth Mwakimomo amesema yeye kama mwanachama na kama kiongozi anatambua kuwa hiyo ni haki yake ya msingi.

"Sio jambo baya yeye (Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA Tanzania Bara na mtia nia wa nafasi ya Mwenyekiti wa chama hicho Taifa) kugombea nafasi ya Mwenyekiti lakini ni utaratibu tu, ni utaratibu ambao unatakiwa kusubiriwa pindi uchaguzi utakapotangazwa watu watagombea kwa sababu chama chetu kina demokrasia" -Mwakimomo

Pia soma: Tundu Lissu atangaza nia ya kugombea nafasi ya uenyekiti CHADEMA

Akizungumzia suala la ukomo wa madaraka ambalo ni sehemu ya ajenda za Lissu, Mwenyekiti huyo wa BAWACHA mkoa wa Mbeya amesema suala hilo ni la Kikatiba, na kwamba Katiba ya chama hicho haijaweka ukomo wa madaraka badala yake imeacha wazi kwa kusema kuwa kila mtu anayo uhuru wa kugombea

"Kwenye hili suala la ukomo wa madaraka labda tuende kwenye mabadiliko ya Katiba yetu kwamba tuende tukabadilishe hicho kipengele ili kuwe na ukomo wa madaraka kama ni miaka miwili iwe miwili, kama miaka mitano iwe mitano, kwa hiyo suala la ukomo wa madaraka pia ni jambo jema" -Mwakimomo

Aidha, Elizabeth Mwakimomo amesema mtazamo wake anaona wazi kuwa Tundu Lissu yuko sahihi, kwa kuwa ni wengi wanataka kuona nafasi za Viti maalum vinakuwa na ukomo (Wabunge na Madiwani wa Viti maalum) ili watu wengine waweze kupata nafasi kwa sababu mara zote wamekuwa wakisema kila mmoja apate nafasi ya kupata nafasi ndani ya chama hicho

"Kwa hiyo inaweza kuwa miaka mitano, au miaka miwili basi, tuwe na ukomo isiwe miaka 10, miaka 20 kama mimi basi niwe mimi tu hapana, wakati kuna mtu mwingine pia hiyo nafasi anatakiwa akomazwe katika huo utaratibu" -Mwakimomo
Kazi kazi Mbowe
 
Back
Top Bottom