Bayern, Liverpool, Madrid na Roma kukipiga nusu fainali ya UEFA, nani ana nafasi kubwa kuchukua Ubingwa?

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368


Klabu za soka za Real Madrid ya Uhispania na Bayern Munich ya Ujerumani zimefuzu kuenda hatua ya nusu fainali katika michuano ya [HASHTAG]#KlabuBingwaUlaya[/HASHTAG]



Pamoja na jana kufungwa goli 3-1, Madrid inafuzu kutokana na jumla ya magoli 4-3(aggregate) dhidi ya Juventus katika mechi mbili kwenye hatua ya robo fainali



Bayern yenyewe katika mchezo wa marudiano wa jana dhidi ya Sevilla ilitoka suluhu ya bila kufungana. Hivyo Bayern inafuzu kwa jumla ya goli 2-1(aggregate)



Timu nyingine zilizofuzu katika hatua ya nusu fainali ni Liverpool ya Uingereza na AS Roma ya Italia

Droo ya nusu fainali kujua Klabu gani zitakutana katika hatua hiyo itafanyika kesho, Ijumaa Aprili 13.
 
Wazee wa mbeleko naona wamepita kwa kuwekewa ngazi kabisaa!! teh! teh!
Unaleta uzaramo kwenye mambo ya msingi?
 
Liver akikutana na striking force iliyotulia km Bayani au Madrid, watakuwa na wakati mgumu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…