Bayern Munich Nani Kawaroga?

Mitsubish

Member
Joined
Apr 26, 2018
Posts
85
Reaction score
58
Hawa jamaa mechi zote mbili wamecheza soka safi pamoja Na kushambulia, mbele wana watu Na chances nyingi za wazi wamepata lakini wameshindwa kufunga magoli ya wazi! mwisho wa Siku wanatolewa Na Madrid ambayo kimtazamo walionekana kuzidiwa ktk game zote.
Nani Kawaroga Bayern?
 
Siyo kirahisi rahisi kumbuka Madrid wameshachukua kombe hili miaka miwili mfululizo na hasa ukitilia maanani kwamba kwenye laliga msimu huu haukuwa mzuri kwao. Itakuwa patashika nguo kuchanika.
Yah ni kweli nikiangalia timu zote haziko vizuri sana ila najaribu kuona jinsi Liverpool ilivyo kihistoria na jinsi inavyozidi kuimarika kila uchao kupitia kwa washambulizi wake kina mohamed salah
 
Mwenye nyumba hata akijisaidia haja kubwa sebuleni utamfanya nini? Utamfukuza?
REAL MADRID ndiyo Mfalme wa UEFA wa muda wote
 
Japokuwa naipenda R.Madrid kwa Spain ila Shughuli itakuwa ngumu kumtoa Liverpool.

Wasipokuwa makini Kombe laweza kutinga Uingereza.
 
Kibongobongo utasikia wanasema na wao wamekula rambirambi
 
Tatizo wanacheza knock out stages kama ligi. Real ni Kings of knock out stages!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…