BBA 2: Mtanzania ashinda!

BBA 2: Mtanzania ashinda!

Kip it up rich.Na wale mafisadi walioitangaza Tanzania hadi ikajadiliwa kwenye house of commons kuhusu ununuzi wa rada?
Na hao mawaziri na wabunge watakaoenda kumpokea Huyu jamaaa nao watakua mashabiki wa uzinzi?
Watampokea Rich kishujaa,je watoto wakiuliza ni shujaa wa nini hao mawaziri watakaporudi home watawaeleza ukweli?

Maadam amenyanyua Bendera yetu akatutangaza basi hatuna budi kumpongeza
 
Hapa India wanajifanya ni watu wenye msimaamo saana na culture yao lakini lilipokuja suala la Priyanka Chopra kuvaa vichupi jukwaani Miss world afu akaibuka mshindi basi wahindi ndipo walipoonyesha unafiki wao mbele ya dunia

Leo hii ukiangalia bollywood yao ni hatari tupu ka Sodoma na Gomora
 
Hofu yangu ni kuwa wanasiasa wanaweza wakachukulia huo ushindi kama nafasi yao ya kuwasahaulisha watanzania matatizo yao. Utashangaa atapokelewa na hata viongozi wa serikali, ataitwa hata ikulu, ataitwa Bungeni Dodoma kupata pongezi kwa kuitangaza Tanzania.
]

Ikiwa hivi nitashangaa, nitajua kweli hawa jamaa zetu wa CCM wamekosa pakutokea. Yaani waamua kuchukua credit kwenye hili. Ila sidhani kama Naibu Waziri wa Michezo ataenda kumpokea kutakuwa na ubaya, lakini siyo waziri. In case hili jambo limetusaidia kuonyesha kwamba kumbe nasi watanzania kuna sehemu tunaweza kujikakamua, hata kama ni mambo ya ngono! Lakini hatupaswi kulishikia bango na kuona kwamba ni jambo la maana sana, hakuna.

Baada ya kusema haya, nami I am out here. Ingekuwa mimi ndiye moderate, basi hii kitu ingetoka haraka sana hapa na kwenda kwingine. For sure this is not politics-it is sometthing like entertainment, utamaduni, ngono, etc. Take it there please!
 
I hope hakuna msafara wa mawaziri utakao enda kumpokea, sababu itakuwa ni kusababisha traffic barabarani for no reason

mie sitaki hata kusikia JK atamkaribisha Ikulu,Mtaji wa kisiasa wa CCM,mie huwa nashangaa sana kwanini kuwang'oa mafisadi isiwe mtaji wa kisiasa wa CCM
 
Sidhani kama Richard atakaribishwa ikulu lakini hata akikaribishwa sitashangaa maana tumeona jinsi ikulu ilivyogeuka na kuwa dangulo.

Tumeona jinsi mamisi wanvyokaribishwa na wapambe wao wakifanyiwa sherehe ndani ya fensi ya ikulu

kumkaribisha mtu ikulu si mbaya lakini kuna madhara yake kama kila mtu ataingia hasa kwa kufanyiwa sherehe na kama tunvyojua sherehe huambatana na matukio ya upigaji picha mbalimbali kama ukumbusho akiwa ikulu.

Picha hizi za kumbukumbu ndani ya ikulu zinaleta kero na watu wanazitumia vibaya ikiwa ni pamoja na utapeli

Nani ankumbuka officer mmoja wa jeshi la polisi alitapeliwa shs 2.4 milion kwa kuahidiwa kuwa atakuwa IGP kabla ya Mwema? Watu walifika offisini kwake wakiwa na vielelezo kadha ikiwa na picha mbalimbali za ikulu na kujitambukisha wao na mtandao.

Picha hizi naamini zinatumika vibaya jiulize mtu akufikie nyumbani kwako na anadocument za ikulu na picha akiwa ikulu hutamwamini kwa atakachokuambia hasa sisi tulio huku mbugani?

Naomba ikulu ilindwe, iheshimiwe na kama umefurahishwa na kikundi chochote au mtu yeyote unataka umfanyie sherehe tuna mahoteli chungu mzima na kumbi nzuri tu kwa ajili ya kazi hizo; ndiyo maana wananchi nao wanabadili residential placess kuwa commercial, bar, ukumbi, petrol station nk wanaona hata ikulu ni sehemu kumbi za starehe.

Na hii nimeanza kuona kipindi hiki cha JK sina uhakika hata kitcheni part zaweza fanyika huma na hata segere na midundikoooo

Cha Msingi IKULU iheshimiwe

Mungu ibariki Tanzania
 
DK ndiyo hivyo hali ilivyo,ndiyo katabia ketu kubadilika ni ngumu.Ila nimeangalia ni kwamba jamaa anatesa (sijui hio msamiati ni outdated).Ameonyesha talents zake.Cha muhimu ni determination na seriousness ya mtu anachofanya ili afanikiwe.Wenzetu walioendelea walitumia principles alizotumia Richard na wakafika walipo sasa.Nachoweza kusema alichofanya Richard siyo longolongo,alikuwa na determination, hivyo vijana inabidi waige vigor yake,nadhani ndiyo ujumbe muhimu aliyotupelekea.
 
Watanzania tujivunie kwa ushindi wa Richard.
There must be something right in this country after all,maana yule Mwisho alikuwa wa pili na huyu Richard kashinda.Maybe our honesty and originality ndio umeleta ushindi wa Richard na Mwisho kabla yake.Sasa basi if that is the case,maybe theres something here for our politicians to get a few pointers...
Kuhusu ngono na kadhalika,i'm sure leo hii wote tukiwekewa camera makwetu wataona tu.Huyu jamaa na wenzake walifungiwa miezi mitatu,no communication with the outside world kabisa.Mana hata wafungwa wa jela huwa wanatembelewa.Then to top it up,unakutana na mtoto mzuriiii humo ndani ambaye anakupenda kikweli.....he summed it it up well in the end,he said "after all,i'm like you...i'm human!"
Tunaweza kulaani yanayoendelea ndani ya Big Brother,lakini lazima tukubaliane kuwa hii ndio entertainment ya sikuhizi...reality tv,na huu ndio moja ya global utamaduni ambao tumeukubali,na tumeshinda!
Lets rejoice.
 
I hate the guy but nilimpatia vote yangu kwani niligundua namchukia kwa tabia ambazo hazina tofauti na zangu. yaani kukosa uaminifu kwa mkewe. ila tukubali kuwa big braza ilitazamwa na watu wengi zaidi kwa sababu ya richard. hata nilipokuwa nje ya nchi nilikuwa nakesha usiku kuangalia afanyacho na tatiana.

naamini kuwa uamuzi wa kuparamia mabinti utamsaidia zaidi maana yule kaka yetu wa awali pombe zilimparamia baada ya yeye kuziparamia.

dola laki moja duh?? mara ya mwisho mimi kuziona ni juzi ndotoni. namfurahia pia kuwa ameonesha utanzania wake na kuutukuza mbele ya halaiki. nampongeza tatiana pia kwa ahtua aliyofikia maana walikuwa good perfomers ktk jumba lile pweke. sijui next tyme tanzania itawakilishwa na kijana wa tabia ipi walah maana tabia njema zooote zimeshatuwakilisha naombea asituwakilishe mtu mwenye tabia ya kikaramagi ohoooo

hongereni watanzania kwa kumsaidia richard kushinda
 
Jamani humu ndani kuna watu huwa wanaingia wakiwa wamelewa.Hii ni thread ya Michezo na burudani.Kuna mtu kasema itolewe humu kwenye siasa hataki kuiona....jamani mniache kwanza nicheke...haya ni matege ya macho.
Kijana kashinda Mi dollar yake kwa technique ya ajabu uku tanzania mlioko mbali mgeona walivyo shangilia huwezi amini.
Nipeni njia ya kuweka picha niwawekee humu ndani.
 
Hapa sio kwenye siasa boss....angalia heading ya thread sio kukurupuka na kuanza kuandika lawama.Hapa ni burudani na michezo.Harafu kashashinda Dogo.Alikuwa anatafuta pesa..na sio kuosha jina la tanzania.Mbona watu kibao mtoni wanafanya kazi za kudhalilisha lakini kwa kuwa hatuwaoni basi nyie ndio waongeaji kama.
 
Hongera kwa mara ingine Richard.

Wana JF, wakati mwingine tunakuwa wanafiki kupita kiasi, na wengi wameonyesha unafiki wao kwa kusema huyu dogo ni mzinzi ila jiulize yafuatayo.

Umefanya ngono na watu wangapi maishani mwako ukiwa ndani ya ndoa au kabla ya ndoa.

Richie walau kaongeza pato la taifa kwa 139,000,000 kwa mwaka huu wa fedha bila kujali ameipataje. Wewe umeliongeza kiasi gani hata kwa kuuza bangi, madawa ya kulevya au haata kwa fedha halali?

Richie tangu aliiingia kweny lile jumba amekuwa akisifia Serengeti, Ngorongoro, na kusifia tanzania kwa ujumla na hata kupepea bendera ya Tanzania ndani na nje ya jumba hilo na tayari baadhi ya washiriki wameahidi kwenda Tz kutembelea mbuga hizo, Je wewe mwana JF umefanya lipi?

Kuna msemo unaosema fanya kazi kama mtumwa mwishoni uishi kama mfalme, na mwingine mtumikie kafiri upatee.... Huoni ndicho alichokifanya mwenzetu?

Watz wangapi wanishi ulaya na US illegally lakini wanatafuta maisha na bado tunawapongeza pale wanaposaidia maendeleoya nyumbani kwao, wangapi wanauza madawa bongo, wanafanya umalaya, Ufisadi, ujambazi, wanakwepa kulipa kodi kisha wanajenga majumba ya kifahari tunawasifia kuwa wajanja. Inapofika kwa Richie eti ni kichefuchefu?

Kwa mtazamono wangu Richie kufanya ngono ni kuonesha kwamba yeye alikua kijana rijali mwenye feelings na alikua na mmoja tu ndani ya ile nyumba kuonesha kwamba bado alikua mwaminifu katika ''Dunia'' ile aliyopelekwa maana walitenganisha na outside world.

Bigup Richie. Hoja hujibiwa kwa hoja.

Nawakilisha
 
sasa subirini kuona JK atakavyo mparamia huyo Richie

Aluu u were right wehsiadaka hii tayari!



Kati ya waliokuwa wa kwanza kumtumia salamu za pongezi ni CCM, ambacho Katibu wake wa NEC (Itikadi na Uenezi), Kapteni Mstaafu John Chiligati alimpongeza Richard kwa ushindi huo.


"Chama Cha Mapinduzi kinauona ushindi huo kuwa ni ushindi wa Watanzania wote. hali hii inatokana na malezi mazuri wanayopewa vijana wa Tanzania hasa kwa kuzingatia sera nzuri za Chama Cha Mapinduzi kuhusu vijana," inasema taarifa yake kwa vyombo vya habari.

http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2886
 
Aluu u were right wehsiadaka hii tayari!





http://www.mwananchi.co.tz/newsre.asp?id=2886


Nakulilia Tanzania!

Mama yangu, sana hii irudishwe kwenye siasa haraka.

Hawa CCM waajabu kweli, yani Chanua Chukua Ma....ndio wanaona ndio sera bora ya malezi ya Taifa?

Ama kweli CCM wanapaswa kupimwa akili! Halafu huyu Chiligati si ndio waziri wa vijana? Shame on him.

Nampongeza Rich 4 getting Rich lakini sio hawa malaya wa kisiasa! Wanadakia kila kitu...hata fisi anachagua.

Yani wanaume kama hawa sijui niwaiteje mie Asha

Nimekereka
 
nimeshangaa kusikia na wanaccm nao wanaandaa mapokezi eeh shughuli ishakuwa yao, raha raha sana.
 
Mmesikia ya Mh. chiligati amesema UVCCM wameandaa mapokezi makubwa kwa Richard???? Vipi kama Richard sio CCM??? mbona wanakimbelembele?

Wanaacha mambo ya muhimu wanajiingiza kwenye mambo ya burudani, mbona alivyokuwa kule kwenye jumba kabla ya kushinda hawakumfanyia kampeni?
 
sisiemu kwa uvamizi nawaaminia, hayo malezi mazuri wanayopewa vijana ndani ya chama hicho yalomwezesha richard kushinda ni yapi? Hawana kazi ya kufanya hadi waandae wao mapokezi? kujipendekeza tu, au ndo wanataka kumpa ukada?
 
Anafika kesho jioni saa moja EAT.Kutakuwa na mapokezi then kuna party vanue bado haijatangazwa.Then ijumaa tena kutakuwa na hafla ya kumpogeza.Tuombe azitumie pesa hizo vyema kwa maendeleo yake.
 
Unajua waBongo ni hatari sana. Nimesoma article moja freemedia, eti umoja wa vijana CCM wanahamasisha watu kwenda kumpokea uwanja wa ndege, na kwamba ushindi wake ni moja ya mafanikio ya sera ya CCM kuhusu kuwawezesha vijana. Jamani hiki si kituko
 
Jamani naomba pamoja na furaha tuliyo nayo watanzania hebu kama kuna mtu anayeijua vizuri Big brother anielezee kwa ufasaha nini maana yake faida yake na hasara zake maana mimi siielewi elewi
 
Back
Top Bottom