BBC NEWS: Milk shake moja ukinywa ni sawa na umeramba sukari kavu vijiko 39

BBC NEWS: Milk shake moja ukinywa ni sawa na umeramba sukari kavu vijiko 39

Herbalist Dr MziziMkavu

JF-Expert Member
Joined
Feb 3, 2009
Posts
42,872
Reaction score
34,363
Nishawaambia Adui wa kwanza Duniani ni SUKARI SUKARI SUKARI SUKARI.

1. Anayekufanya Uwe SHAPELESS na USIFURAHIE hata Mavazi yako NI SUKARI. Nakushangaa kwa nini Unaikumbatia SUKARI.

2. Anayekufanya Unasikia maumivu makali ya Hedhi na Kuharibika Usoni wakati wa hedhi ni SUKARI. Anayekufanya Uwe na Maumivu makali wakati wa tendo la ndoa, hamu ya tendo la ndoa ndogo au hakuna kabisa ni SUKARI.

3. Anayekufanya Unakosa Mtoto unaota ndevu kidevu chote wakati wewe ni mwanamke ni SUKARI. Anayekufanya Unaota matiti unakuwa na hips kama mwanamke wakati wewe ni mwanaume ni SUKARI. Sukari inakufanya maumbile sehemu za siri Yanapungua kila kukicha kadri unavyozidi

KUNENEPESHWA NA SUKARI.
SUKARI IMEFANYA VIJANA WENGI HAWANA NGUVU ZA KIUME KWA KUNYWA HOVYO VINYWAJI VYA SUKARI ETI WANAPOZA KOO NA KUONGEZA NGUVU.

4. Sukari ndiyo Inafanya FAMILIA NZIMA MNANENEPA, Kuanzia BABA, Mama na WATOTO wote Mnakuwa NI KITAMBI. Sukari Sukari.

Tunaposema Sukari Mtambue kwamba Inakuja katika SURA TOFAUTI TOFAUTI wengi tunapumbazika kwamba ni ILE TU INAYOKUJA NYEUPE KAVU.

1. Kwenye Soda Kasome kuna Gram ngapi za sukari halafu jibu utakalopata gawanya kwa 5gram ili upate vijiko. Mfano: Ukikuta kuna gram 37 kwenye kinywaji chako Gawanya kwa 5 utapata vijiko 7 unalamba kila unywapo kinywaji hicho. Fanya Uchunguzi Ujue unalamba vijiko vingapi kwa siku.

Watu wanakunywa soda Zaidi ya 5 kwa siku.

2. Mbali na hivyo Kuna Vinywaji vingine kama MILK SHAKES, MAZIWA YA UNGA, MAZIWA YA MILK FORMULA YA WATOTO, COCKTAILS,huko Pia UTAIKUTA SUKARI.

3. Sukari Pia utaikuta kwenye JUISI TUNAZOTENGENEZA NYUMBANI ¡°SHAKES ZA MATUNDA¡± Mfano: Unachukua Maembe mengi, Machungwa unatengeneza Juisi nzito. Utakutana na neno ¡°NO ADDED SUGAR¡± Usipumbazwe na hilo. Unapokunywa JUISI HIO NI ¡°SUGAR SYRUP¡± Kuna watu wanatupotosha sana.

Unapoambiwa ¡°Embe lina faida kwa afya¡± Haimaanishi Utengeneze Juisi¡± Unapoambiwa ¡°Nyanya, Papai lina lycopene ambayo huua kansa seli haimaanishi utengeneze juisi ya nyanya na Papai upone kansa¡± Unapoambiwa ¡°Beet root na karoti zina faida kiafya haimaanishi utengeneze JUISI¡± Unapoambiwa STAFELI lina ACTIVE INGREDIENTS inayotibu kansa Haimaanishi UNYWE JUISI YA STAFELI UTAPONA KANSA.

Hata hivyo Vitamin ambazo hupatikana kwenye Matunda huitwa WATER SOLUBLE VITAMINS, Ambazo ni B vitamins na Vitamin C. Kisayansi Vitamin hizi huwa Zinapozidi mwilini HUWA HAZIWEZI KUHIFADHIWA MWILINI, ZINATOKA PAMOJA NA MAJI YANAYOTOKA MWILINI. Kwa maana hio KUNYWA GLASI TANO ZA EMBE NA MACHUNGWA UTAKUWA UNAJIUMIZA KIAFYA, UNAMIMINA SUKARI NYINGI KWA MKAO MMOJA KWA LENGO AMBALO HALIENDI KUTIMIA.

Mwili wa binadamu huwa unahifadhi vitamins zinazotembea na MAFUTA ambazo ni Vitamin A,D,E na K hizi huhifadhiwa Mwilini pale unapokula nyingi. Ambapo sasa anayekunywa JUISI ILI APATE VITAMINS NYINGI ANAKULA ANAJIPUMBAZA BURE hakuna CHOCHOTE ANACHOPATA TOFAUTI NA KUUMIZA INI LAKE.

Kwa maana Hio SIKUSHAURI UTENGENEZE JUISI MATUNDA YAKO KWA WATOTO WAKO NA FAMILIA YAKO. Waliotuambia Tunatibu kwa mboga mboga za matunda walitupotosha sana TUMEHAMA KUTOKA KWENYE SODA TUMEAHAMIA KWENYE VIMIMINIKA VYA SUKARI TUNAVYO TENGENEZA SISI WENYEWE.

Athari za Sukari Mwilini.
ZINAKUHATARISHA KUPATA MAGONJWA YA UCHAKAVU WA MWILI MAPEMA SANA KATIKA UMRI WAKO.

MILKSHAKE.jpg
 
Jamani kwa hiyo juice ya embe nikaweka passion bila sukari hats kijiko kimoja ni shida?

Nawaza juice ile ya parachichi mix maziwa ninavyoiependa tena naiongeza na kijiko kimoja cha sukari.
 
Mambo yamekuwa magumu!!! Juice ya kawaida ya matunda nayo hainyweki???

Mzizi mkavu heshima yako.
Japo inaniwia ngumu kuipokea elimi hii!
 
Sasa tutakula upepo.

Hunywi juisi ya kiwandani, hunywi soda, hunywi juisi ya kutengeneza nyumbani.

UNAPATA KANSA UNAKUFA.

Furahia maisha ndugu
 
Nyie mabwana afya mtuache kidogo kufa kupo tu, maana kila kitu mnasema hakifai tunywe nini sasa......Haya basi tutakuwa tunakunywa maji tu
 
Kama ni hivyo makampuni wana hasara kubwa sana

Milk shake 1 ni sh ngapi? Sukari g39 ni sh ngapi?

Chai tuu ya kuweka g5 ya suari ni 200 had 300 kwa mantilie. Sasa huyu ana g39.
 
Kila kitu kikizidi kina madhara. Lakini bora madhara ya matunda na mbogamboga kuliko ya vitu vya kiwandani.

Hizi tafiti kuna kipindi zinatuchanganya tunaamua tuchanganye za kyambiwa na zetu. Wengine wanasema kahawa ni nzuri kiafya, wanascola wengine wanatahadharisha watu matumizi ya kahawa. Tunashauriwa kutumia asali na juice za matunda kadri iwezekanavyo kuepuka madhara ya sukari kavu, sasa na matunda mkisema ni shida tushindie maji?

Hiyo milkshake yenye hicho kiwango cha sukari ni ipi na kwa ujazo gani?
Kiwango cha sukari kitategemea mchangavyiko wa vitu vilivyotumika na kiwango anachotumia mtu.

Ni vizuri kuchukua tahadhari lakini hofu ikizidi inapunguza kufurahia maisha.

Shukrani MziziMkavu
 
Kama ni hivyo makampuni wana hasara kubwa sana

Milk shake 1 ni sh ngapi? Sukari g39 ni sh ngapi?
Chai tuu ya kuweka g5 ya suari ni 200 had 300 kwa mantilie. Sasa huyu ana g39.....
Mkuu hawa wanatumia SUKARI YA VIWANDANI aka KK! Ni balaa!
 
  • Thanks
Reactions: Ok9
Back
Top Bottom