BBI, Handshake breakdown Ruto and Uhuru relations

BBI, Handshake breakdown Ruto and Uhuru relations

Wakenya ni wasomi na Wana akili kubwa , but when it comes to matters politics wanakua wapumbavu ,hata Prof.ataongozwa na mtu wa darasa la pili they are not independent minded when it comes to matters politics.
Kwn wewe huaga unaelewa vitu, sasa anapoongelea siasa za nguvu si bado itakua ana support wahuni...
 
Thank you for understanding me,huyo ndugu yangu hanielewi kabisa.
Nadhani sasa unaelewa ni kiasi gani tunapata taabu ya kujibishana na wakenya, sijui tatizo lenu liko wapi, wakenya wengi hamsomi ili kuelewa kabla ya kujibu, wakati mnasoma, tayari mpo na majibu hata kabla ya kuelewa kinachoelezwa.
 
Wakenya ni wasomi na Wana akili kubwa , but when it comes to matters politics wanakua wapumbavu ,hata Prof.ataongozwa na mtu wa darasa la pili they are not independent minded when it comes to matters politics.
Hapo umeongelea kitu cha maana, mtu mtaishi fresh miaka minne mara kidogo kidogo mwaka wa tano karibia na uchaguzi mnaanza kurushiana maneno ya kijinga..
 
Nadhani sasa unaelewa ni kiasi gani tunapata taabu ya kujibishana na wakenya, sijui tatizo lenu liko wapi, wakenya wengi hamsomi ili kuelewa kabla ya kujibu, wakati mnasoma, tayari mpo na majibu hata kabla ya kuelewa kinachoelezwa.
Km kuelewa ni ku support wanasiasa wenye nguvu katika siasa sasawa...
Manake naona mwenzangu anatumia nguvu nyingi kum support ruto tangia hko juu...
Anyway, hayo ni maamuzi yake..lkn ukija upande wangu, siasa za ukabila na regions nimezifutilia mbali maishani mwangu..
Ndo manake ninapopiga kura namchagua mtu kulingana na manifesto yake na uelewa wake wala sichagui chama..eti km wewe ni jubilee basi kuanzia Mca mpka rais jubilee...yani mtu hataki kujua kabisa,
huo ni utahira...

Na hapa jf wakenya wa sampuli hyo wapo
 
Ruto hana wapiga kura wa kutosha ni.mpaka kuwe na coalition ya kikanda.

Yaani kama hatakaa sahani moja.na kina Jumwa na kina Balala kutoka Pwani na Lamu, akina Mudavadi kutokea hapa kati kusini, lakini pia apate someone kutokea kisii kuja Migori hawezi kushinda.
Ruto hawezi pata kitu nyanza kabisa bila Raila pia

Central ampate Kalonzo Musyoka labda
Wakalenjin ni kabila kubwa, kumbuka chaguzi mbili zilizopita kolabo ya Wakalenjin na Wakikuyu ilikuwa na 45% ya Wapiga kura. Kwa sasa kinachowasumbua wakongwe ni namna gani ya kumtenganisha Ruto na wapiga kura wa Mount Kenya, Wakikuyu. Mpaka sasa hilo halijafanikiwa ukizingatia kuwa kwa Wakikuyu Raila hakubaliki kabisa, historically kuanzia enzi za Baba yake, Jaramogi.

Kwa sasa Wakikuyu wamegawanyika huku wengi wakiwa wamestick na Ruto ukizingatia uadui na mapigano makubwa ya Wakikuyu na Wakalenjin mwaka 2007 yaliyopelekea Kenyatta na Ruto kwenda ICC, muungano wa Uhuru na Ruto uliyaleta makundi haya mawili pamoja na kufuata makavu ya uadui wa miaka mingi, ikumbukwe, Wakikuyu wengi wanaishi eneo la Rift Valley, nyumbani kwa Wakalenjin.Hali ikibaki ilivyo sasa, Ruto ana nafasi kubwa ya kushinda.

Upande wa Pwani Balala na Jumwa hawana ushawishi kwa sasa, Raila wakati wote amekuwa na nguvu Pwani, japo Ruto huko atapigania tu wala 30%.

Wakisii bado hawajawa na nguvu kwenye siasa za Kenya.

Ruto kubwa analohitaji ni:
1. Ahakikishe anabaki na Wakikuyu, kwa kuchagua Mkikuyu atakayeonekana kama mrithi wa Uhuru kwenye Umakamu au sasa Uwaziri Mkuu. Uchaguzi ukiwa Ruto na Raila Wakikuyu watamchagua Ruto.

2. Ahakikishe anapata nguvu upande wa Magharibi, Waluhya, hawa ni kundi muhimu kwenye uchaguzi, au walau alete ushindani mkubwa.

3. Kwa kuwa Raila amekosana na Kalonzo Musyoka na amekuwa karibu sasa na maadui zake, ajenge ushirikiano na Kalonzo kumhakikishia kupata kuwa za Wakamba, Eastern.

Akifanikiwa haya, urais ni wa kwake.
 
Km kuelewa ni ku support wanasiasa wenye nguvu katika siasa sasawa...
Manake naona mwenzangu anatumia nguvu nyingi kum support ruto tangia hko juu...
Anyway, hayo ni maamuzi yake..lkn ukija upande wangu, siasa za ukabila na regions nimezifutilia mbali maishani mwangu..
Ndo manake ninapopiga kura namchagua mtu kulingana na manifesto yake na uelewa wake wala sichagui chama..eti km wewe ni jubilee basi kuanzia Mca mpka rais jubilee...yani mtu hataki kujua kabisa,
huo ni utahira...

Na hapa jf wakenya wa sampuli hyo wapo
Bado kabisa hujamuelewa alichosema. Ila tatizo ninaloliona ni kwamba tayari umeshamuweka upande mmoja wa siasa, kwamba anaunga mkono kundi moja la kisiasa, kwahiyo akili yako imeshajiandaa kumpinga kwa hali yoyote ile.

Mimi ambaye nipo "Neutral" kati yenu, ninaona kwamba unamuhukumu bure, yeye alijenga hoja vizuri sana. Haijalishi kama anaunga mkono upande huo unaosema, lakini hoja yake ilikua ya msingi sana na " very Neutral".

Ombi langu ni kwamba, sisi binadamu tunatofautiana katika mambo Mengi, dini, kabila, rangi na mirengi ya kisiasa, muhimu ni kuvumiliana, kuheshimiana na kusikiliza na.
 
Nilibadilika kitambo tu sisubiri kiongozi atoe kauli ndio nifanye maamuzi Nina akili zangu najiamulia mwenyewe, tofauti yangu na nyie siendi na euphoria eti kwa sababu mtu flani amesema komora yupo hivi halafu nauchukua Kama wimbo naanza kuuimba no I do my independent analysis na ninafanya maamuzi yangu kulingana na akili zangu na ndio maana nikaenda skuli ,kwa hivyo sisubiri mtu a reason on my behalf eti maana yeye ni kiongozi,hata akiwa rais akifanya Jambo lisiloniingia akilini nitamkemea.
Ndio uanze na wewe kubadilika basi, usitegemee wengine wakuanzie
 
Back
Top Bottom