Bei ya mafuta yapanda kwenye soko la dunia

Bei ya mafuta yapanda kwenye soko la dunia

BARD AI

JF-Expert Member
Joined
Jul 24, 2018
Posts
3,591
Reaction score
8,826
Bei ya mafuta ya petroli imepanda leo Desemba 6, 2022 kwa asilimia 2 na kufikia dola 87.3 kwa pipa, saa chache baada ya kuanza kutekelezwa kwa hatua kadhaa za mataifa ya magharibi zinazolenga kupunguza mapato ya Urusi katika sekta yake ya nishati.

Ongezeko hilo limeshuhudiwa baada kuanza kufanya kazi kwa azimio la mataifa ya magharibi la kuweka ukomo wa bei kwa mafuta ya Urusi pamoja na marufuku ya Umoja wa Ulaya ya kuingizwa mafuta ya Urusi yanayosafirishwa kwa njia ya bahari.

Wanasiasa wa nchi za magharibi wanatarajia hatua hizo zitavuruga uwezo wa Urusi kifedha na kuilazimisha nchi hiyo kuachana na vita vinavyoendelea nchini Ukraine.

Hata hivyo tayari kuna wasiwasi kwamba uamuzi wa kudhibiti bei ya mafuta ya Urusi kwa hadi dola 60 kwa pipa, utapunguza kiwango cha nishati hiyo kwenye soko la dunia na kupandisha zaidi bei ya petroli.
 
Ila EU wameniprove wrong sana aiseee

Nilikuwa nawaona kama watu wenye akili sana kuliko viongozi wengi wa Africa kumbe nilikuwa wrong saana

Wanisamehe viongozi hao wa Africa.
Hawa jamaa wanazidi kuyakoroga
 
Kwa hili linaloendeleq tutegemee ufaransa wingereza vugu vugu litaanza upya ...na kwa hili hawatashinda , ila wataambulia maumivu makali sana
 
Hawa jamaa wanazidi kuyakoroga
Ile kauli ya kutumia nguvu nyingi kuliko akili ndio naiona kwa EU

Mmarekani anatumia akili nyingi kuliko nguvu ndio maana kawajaza vizuri sana na wao wapo kusema ndio mzee.
 
Back
Top Bottom