Bei ya mchele yapaa kilo Tsh 2,300 kutoka Tsh 2,000

Bei ya mchele yapaa kilo Tsh 2,300 kutoka Tsh 2,000

Waziri wa kilimo tunaomba zuia nafaka kuuzwa nje ya nchi hali ni tete watu wanalia chakula hakushikiki mitaani bei ipo juu na fedha hamna, mchele awali ulikuwa ukiuzwa tsh 2000 kwa kilo kwa sasa tsh2300/= unga wa mahindi ulikuwa unauzwa tsh 800/=kwa kilo kwa sasa tsh1500/= vyote hivyo vimepanda huku pesa hamna.

Serikali iache kuziba masikio kuhusu hili njaa ndiyo inaleta matatizo kwa wananchi! Endeleeni kusema vita vya Urusi na Ukraine ndoo vimeleta majanga hayo.
Azuie Ili wewe ufurahie harafu mkulima imkate sio?

Tunayembea kwenye kauli za Jiwe,ukiona Bei ni juu kalime na wewe uje kuuza bei ya chini.

Mwisho ni kwamba chakula sio mchele pekee bali kuna viazi mihogo magimbi,mtama uwele,ulezi ,ugali nk nk so acha kukariri maisha.
 
Ni zamu yetu wakulima kulamba asali maza fungua nchi wakulima tupige noti.
 
Serikali shikilia hapo hapo,hao wapuuzi wamerundikana huko mijini wanazurura afu wanataka waishinkwa jasho la mkulima..

Yaani mkulima anunue mbolea Mfuko 160,000-200,000 ,madawa na shubiri kama zote harafu aje auze Bei unayotaka wewe? You can't be serious..

Tokeni mjini kama hamna Kazi mkalime, serikali imeamua kuwaletea kilimo cha umwagiliaji kama hamtaki endeleeni kulia mtaona moto.
 
Huyo Msomalia tuliempa Wizara yeye ana dili na Russia-Ukraine War, badala ya kuingia ground kwa Wakulima.
 
Back
Top Bottom