Bei ya sukari Tanzania ni zaidi ya 3000 wakati Msumbiji, Malawi, Kenya, Uganda na Zambia haizidi 2500. Kwani sisi dhambi yetu nini?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Sio siri hili jambo linaniumiza sana moyo wangu sijui kuna ushirikina gani kwenye suala la sukari hapa nchini kwetu.

Maana licha ya kuwa tuko jirani na bahari kuu tuna ardhi nzuri na tuna kila fursa ya kunufaika kuliko majirani zetu lakini bado tunapata mateso ya kununua sukari kwa gharama kubwa kuliko jirani zetu wote.

Tangu nakua mpaka sasa ni mtu mzima mwendo ni uleule nakumbu ka nilisoma na jamaa mmoja alikuwa akienda na baiskeli kuchukua sukari za magendo Zambia na kuiuza Tanzania Kisha analipa ada.

Ndugu zangu wafanya maamuzi hebu kuweni serious basi.

Pia, soma=> Munde Tambwe: Kwanini Tanzania Bei ya Sukari ni kubwa kuliko Zambia, Malawi na Rwanda? Kuna Tatizo mahali tuambiane ukweli!
 
Dhambi ni kuzaliwa na wazazi wa oga na watoto wakawa waoga na wajukuu ni waoga, kwahiyo hi nchi inatawaliwa kwa utashi wa wenye mamlaka sio raia.
 
Zambi ya Watanzania anaijua Bashe na Tulia!!
 
Kama BASHE yupo humu jukwaani aje ajibu au waliopo karibu nae waje humu kumjibia..

Naomba kuwasilishaa
 
Uchumi wa kati. Lazima uwazidi uliowazunguka kwa daraja na bei.
 
Kuikumbatia CCM ndiyo dhambi yenyewe,nyuki hakumbatiwi kamwe
 
Yani wenye bandari bei ni kubwa kuliko wanao pitisha bidhaa kwenye bandari yetu ...
 
USIOE KAMA SIO BIKRA
 
hayo ndiyo anayoyapigania Bashe. Kishaiona "cartel" ya wale wazee waliokuwa wanajitetea kijinga juzi, Bashe kishaipatia muarubaini.

Ndani ya mwaka huu ni lazima watashusha bei iendane na uhalisia au wafunge viwanda tuagize sukari ya rahisi kama wanavyoagiza wenzetu, miwa ya wakulima wadogo wadogo tutaipatia soko lingine.

Hawa wenye viwanda hawana huruma kabisa na wananchi wao.
 
Bei ya kinywaji cha Coca-Cola marekani ni TZS 4000-6000.Bei kwa Tanzania ni tzs 600 - 1000. Umegundua nini?
Hacha kulinganisha mbingu na dunia,linganisha uhalisia.
Wamarekani hawawezi kulalamikia bei hiyo kwa sababu inaendana na kipato chao.
Ndio maana mleta uzi amelinganisha amezitaja nchi zinazoendana na Tanzania kiuchumi.
 
Bashe ni mtuhumiwa na fisadi!
 
Bashe ni mtuhumiwa na fisadi!
Lazima iwe hivyo, kwa sababu anawapigania Watanzania bei ishuke.

BBashe anapigwa vita kuagiza sukari ya dharura tu, iliyoshusha bei ya sukari kutoka shilllingi elfu kumi mpaka kufikia elfu tatu. Bashe anapigwa vita kubadili sheria iliyokuwa inawalinda hao mafisadi.

Labda poyoyo tu asiyeziona jitihada za Bashe kupambana na hiyo "cartel".
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…