Bei ya Vifurushi itamuondoa mtu next week..

Bei ya Vifurushi itamuondoa mtu next week..

Wale wana hela sana,,hata wafukuzwe,kianzio cha maisha wanacho
 
Mnamuonea kindugulile bure tuu. Yeye hana mamlaka ya kupandisha wala kushusha.
Lawama zote zinamuangukia Ndugu Lile. Yeye ndiye alisema Bei itapungua kumbe huku alikua na mpango ovu wa kujipendekeza kwa watu Fulani Fulani. Sasa Ndugulile Ali over do. Yaani badala ya kushusha Bei kifurushi Cha ulichokua unapata kwa alfu Sasa unapata kwa alfu nne. Nduguli is responsible for this mess.
Ingekua nchi nyingine angejiuzulu. Wakiendelea kumuacha pale atawavua nguo mchana kweupe.
 
hawajafikiria kabisa kuhusu watu wanaotumia internet kuendeshea maisha yao a. K. A wamachinga wa mitandaoni, wanafunzi wanajisomea kupitia mitandaoni na umuhimu wa internet wakati huu wa corona 💡
 
Jumanne kuapishwa waziri mwengine, aliyepo amepwaya sana, na hili amelipwa fedha na haya makampuni, ili kukomoa wananchi hasa wana -CCM wanaoshinda mtandaoni kuitetea serikali dhidi ya mabeberu.
Tangu juΩi usiku ma-injinia wa mitandao ya simu wanahangaika kurudisha bando kama zamani, ila siri ambayo nawavujishia ni kwamba KUMUM-GANG wapo kazini kumhujumu SAmia suluhu Hassa, na wameshindwa, linaongozwa na yule aluyepewa ubunge viti maalum
 
Nafahamu kwamba huu mchakato wa kupandisha gharama za vifurushi ulianza tangia zamani, nafahamu pia moja ya mbinu za kisiasa ni kutengeneza tatizo na kulitatua mwenyewe hata kama ulikuwepo kwenye jopo la waliofanya maamuzi kufikia kupatikana kwa tatizo hilo.

Serikali ina kiongozi mpya ambaye pamoja na yote lazima aonyeshe amesimama upande wa watu wengi wanaolalamika kwa upandaji holela wa vifurushi ambao sio tuu utainyima serikali mapato bali utarudisha watu nyuma kutoka katika matumizi ya TEHAMA , kwa maana nyingine atajitenga na maamuzi ya kupandisha vifurushi.

Hivyo natabiri kuwa kuna vichwa vinaenda kuliwa pale TCRA na Wizara ya mawasiliano, maboss wote wanaohusika na haya maamuzi wajiandae, hii pasaka itakuwa pasaka yao ya mwisho kama maboss au viongozi wa sehemu husika..

Kama ni wajanja wachukue hatua za mapema sana kuonyesha wamesimama upande wa watu ili waokoe nafasi zao za kisiasa, kwani atakayeliwa kichwa hapa ndio atakuwa amekufa kisiasa na kiutumishi.
Nimepita sehemu ,kulikuwa na jamaa wanasema kuwa makampuni ya simu yanafidia hasara iliyosababishwa na kufunga mitandao ya kijamii wakati wa uchaguzi(uchafuzi)ulio pita.
 
Nch hii kwakweli da watu wako bize navifurushi nendeni muone mfumuko wavifaa vya ujenzi mm nadhani tuongelee kwaujumla mfumuko wabei
 
Back
Top Bottom