Bei za mabasi

Hivi Mitsubish fuso Bus seat 56 inauzwa sh ngapi?
 

ndugu yangu nakushauri tu biashara ya mabasi ngumu unagawana na wauza tiketi
 
Kanunue EICHA 1 = 64mil ukimbizane nalo hapa mjini ili upate ujuzi na utaalam wa biashara ya magari. baaada ya mwaka 1 utajua kila kitu kuhusu biashara ya magari
 
Bei 180mil zero km
 

Attachments

  • 1427126899730.jpg
    71.4 KB · Views: 416
  • 1427126948808.jpg
    76.6 KB · Views: 412
Ushauri mmempa kibao.cha msingi muache aingie kwenye 'game' cha kujiuliza kama kaweza kupata 370m kwa ujasiriamali basi mjaja.ingawa hasemi alikua anafanya biashara gani tumshauri aibooreshe.ushauri wangu biashara ya basi ni nzuri kinachoangusha watu ni operators in short MGT ukiweza usimamizi na ukapata watendaji wazuri na chombo kipya uta-win tu
 
Muombe majinja akuuzie unalaka rangi na kubadilisha jina basi unaletewa hesabu kila siku
 
mimi nafikiri mkuu mleta mada umeacha sehemu ya habari.

Kwamba ulikuwa unafanya biashara fulani, au umepata hela sehemu fulani na unajiuliza ni njia ipi ya kuendeleza pesa yako. Wewe mwenyewe umefikiria biashara ya usafirishaji ya mabasi.

Mimi ningeshauri kama ulikuwa na biashara kabla , ufikirie namna ya kuimarisha kwa njia mbalimbali kuifanya kuwa ya kisasa zaidi, kuongeza mambo mapya nk nk.

Au kama ndio umepata hela mahali fulani, cha kufanya cha kwanza , nenda uajiliwe na ufanye kwa kiwango kidogo upate uzoefu halafu ndio uingie kwa kiwango kikubwa baada ya kujua uzoefu katika eneo hilo.

Ukitaka kujua wazo lako kama ni zuri, test kwa kwenda benki kama unaomba mkopo , halafu uone kama benki watakubali kukupa hizo hela unazotaka.

Sababu watakazotumia kukunyima mkopo, ndio maeneo unayotakia kufanyia kazi ili kufanikiwa huko mbeleni.

Mwishoni maono yako ni yapi kwenye jambo lolote? Unasukumwa toka ndani kufanya kitu gani? Hayo ni maeneo ya kuanzia kuyatumia hayo mamiliioni uliyoyapata.
 
Mdau kuna watu wanakukatisha tamaa hapo juu ya hii biashara.
Kwanza nikwambie hii business inalipa sana, tena sana, ili mradi uwe na upate technic zake hasa kama utaweza kucheza na kitu nnachokiita (Udhaifu).
Twende kwenye topic, nijuavyo scania mpya kupitia kwa wakala wao mkuu pale nyerere road haizidi 700mil, yutong kupitia wakala wake benbros watakuchapa na 250mil, ukienda kwa manji -Dar coach kuchongewa body sina hakika sana ila si chini ya 100mil model mpya ya body na ukienda kenya kuna makampuni matatu ambayo ni famous sana kuna choda, LHS na nk.

Hivo basi kwa ushauri wangu mtaji wako ni mdogo kulingana na hitaji lako kwa gari la uhakika lenye uwezo wa kuishi kipindi kirefu.

Kwa hiyo nna ushauri huu hapa, nunua Yutong new model tena usitumie wakala wa hapa bongo ni PM nikupe simple, safe and preserve your money, hapo utapata mbili ambapo hata Sumatra watakupa kibali, kwani ukiwa na gari/bus moja hakuna kibali cha kwenda zaidi ya 320km.

Kwa habari ya kuibiwa na hao wakatisha tiketi kwa ufupi hakuna kitu kama hiyo ndg, ndo maana mdau mmoja kasema watu wasingenunua mabasi kama kuna hasara na wizi.

END.
 
Hiyo hela chukua tata bus 2, ya tatu watakupa kwa mkopo, fanya daladala, uhakika kila mwisho wa wa mwezi kila moja una 4m, hio ni cream. 4m *12 = jibu utajaza, kwa ushauri zaidi npm
 
Kuna gari mupya kibao huku mwambie tu anunue zimechoka alete huku Mtwara Utapanda wewe.. Alete vitu vipya huku kama anataka. #Mtwara
 
Jamani tupeni mlejesho wa muanzisha uzi, au ndo mmiliki wa hizi LEO COACH/LUXURY?
 
Mkuu Nimevutiwa na iyo idea ya Eicher ebu fafanua kidogo nione pesa ivyorudi hapo [emoji39] [emoji39]
 
Mkuu Nimevutiwa na iyo idea ya Eicher ebu fafanua kidogo nione pesa ivyorudi hapo [emoji39] [emoji39]
Hesabu ya bosi kwa bus la tata au eicher kwa siku ni 300,000
Kama kwa mwaka gari inafanya kazi siku 300 inakuwa 300,000*300=90,000,000.
Hizo siku 66 zilizobaki gari inakuwa mapumziko au service.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…