Bei za vitu kushuka Kenya, sisi tunakwama wapi?

Bei za vitu kushuka Kenya, sisi tunakwama wapi?

Allen Kilewella, denooJ na wote mnaotaka mabadiliko kwa kutegemea wananchi kuamka wenyewe bila kuhamasishwa kupambana kama mvua, bila kuwa organized wala mchango wowote wa viongozi, kuna wito wenu mahsusi hapa.
Nyie wakosoaji wetu field huwa hampo. Sisi tunapambana sana na tena katika hali ya ukata na kama si hivyo leo hii CCM ingekuwa iko yenyewe tu. Hamuoni jinsi tunavyopambana kuifanya CHADEMA iendelee kuwepo hata kama inapata mashambulizi makubwa kiasi gani??

Nchi nzima shughuli za chama zimekuwa zikiendelea kwa bidii sana, lakini bado mnadhani tatizo ni sisi na si watanzania. Sisi tunaongea na watanzania na wengin wao wanadhani maisha waliyo nayo ni majaaliwa ya Mungu.

Hata wakati wa utumwa wapo watu weusi waliokuwa wanapinga utumwa lakini walizidiwa nguvu na ndugu zao walioamini kwamba wazungu ni watu bora zaidi kuliko wao.
 
brazaj Kenya siasa zao zimekuwa - Shaped na ukabila. Kwa ivo hata watu wanaojitokeza mara nyingi kuunga mkono upande fulani hufuata sana mkondo huo wa ukabila.

Kwenye chaguzi za Kenya Profesa Mutahi Nguyi hutabiri kwa usahihi matokeo ya Uchaguzi kwa kuwa husema chaguzi za Kenya hufuata mkondo wa kikabila. Sasa huko watu kikuunga mkono chama "chao" na kukichangia ni rahisi sana na Kenya tuwe wakweli tu, kuna taasisi imara za kiraia kuliko huku.

Kwa mfano unaweza kuifananisha Knut na CWT?
 
Nyie wakosoaji wetu field huwa hampo. Sisi tunapambana sana na tena katika hali ya ukata na kama si hivyo leo hii CCM ingekuwa iko yenyewe tu. Hamuoni jinsi tunavyopambana kuifanya CHADEMA iendelee kuwepo hata kama inapata mashambulizi makubwa kiasi gani??

Nchi nzima shughuli za chama zimekuwa zikiendelea kwa bidii sana, lakini bado mnadhani tatizo ni sisi na si watanzania. Sisi tunaongea na watanzania na wengin wao wanadhani maisha waliyo nayo ni majaaliwa ya Mungu.

Hata wakati wa utumwa wapo watu weusi waliokuwa wanapinga utumwa lakini walizidiwa nguvu na ndugu zao walioamini kwamba wazungu ni watu bora zaidi kuliko wao.

Ninatambua umetenganisha makundi mawili bila vigezo wala hata ya kuwa na msingi wowote.

Kuna ninyi na sisi unaotuita wakosoaji. Niwe wazi kuwa sikuelewi una maana gani.

Kwamba hatuonekani field bila kuainisha field huko ni wapi ni maelezo yasiyo na maana yoyote. Kumbe basi nyie ni nani na sie ni nani?

Huku nikiwa nimetupia utambulisho ghushi unaupata wapi ujasiri kujitambulisha wewe na wenzao kama nyie dhidi ya nani wengine nikiwemo miye kuwa ni sie?"

Labda tujaribu kutambuana ndugu Ili tuepushe mikanganyiko isiyo na tija. Field tunakokutambua wapigania haki na uhuru ni huku:

Tunataka haki? Hatutaki tozo? Tukutane Tahrir.

Hao kama ndiyo uliolenga kutuita sisi, nitakukubalia kwa moyo mmoja. Huku tuko na waungwana wengine. Huku wapo kina Zawadini, kina Mag3 na wa namna hiyo. Kama hao ndiyo ulilenga kutuita sisi tutaitikika kwa kauli moja "afande!"

Kwa uelewa wetu kinyume cha hapo ni kundi lile jingine lenye kujumuisha magenge ya walamba asali, wahuni, wasaka fursa na yale ma vijana ya hovyo sasa. Yaani kundi lisilokuwa na mchango wowote kwa taifa hili.

Kwa uelewa wetu yapo makundi mawili tu, yaani sisi na wao (dhidi yetu). Huwezi kuwa katikati. Kundi hili lisilokuwa mchango wowote dhidi ya taifa hili wako dhidi yetu. Mfano wao mzuri ni akina joni na wenzao pale Lumumba.

Kwenye kundi hili wamo pia wale wanaosaka (ubunge, udiwani nk ndani ya Chadema na vyama vingine) kama kipaumbele chao na kwa gharama yoyote. Au nawe unausaka ubunge hata kama ni kwa kuachana na hoja ya katiba mpya sasa?

Beberu akisema, "You're either with us, or against us." Kwa maana yake kamili kuwa huwezi kuwa rafiki wa Mungu na Shetani kwa wakati mmoja.

Yawezekana kujaribu kujinasibisha kundi mdomoni lakini si kwa vitendo. Kamanda Asiyechoka ng'oo! ni mfano mzuri wa "wao."

Makundi mawili haya yako kwenye vyama vyote kwa kujua, kutojua, kimchongo mchongo, ki uhujumu, kishabiki, nk. Kulikoni kutaka kujimilikisha chama dhidi ya nani ndugu?

"Mwana wacha kupiga mayowe waache waone wenyewe." -- Tabora Jazz.

Kwamba ninyi bado mko busy mnaongea na watanzania? Jaji Warioba alisema 2013 huko kuwa watanzania walio wengi wanataka katiba mpya. Katiba mpya haitapatikana kwa kuendelea na maongezi yasiyokuwa na ukomo:

Ni Tanzania tu, tunakotaka mabadiliko bila vitendo

Kwani nyie ni Chadema ipi ndugu?

Tuna Imani na CHADEMA hii, wala si nyingine

Kupigania haki na uhuru siyo lelemama. Hata kina Muzorewa, Sithole, na wa namna hiyo Zimbabwe au kina Buthelezi SA, walijitanabaisha kuwa katika vita hivyo hivyo.

Angalizo: nilipendekeza kuepuka mjadala wa kuruka ruka.

Sikuona majibu yako kutoka kwenye majibu yangu kufuatia nilizoona kuwa zilikuwa ni hoja zako hizi:

a) Kwamba watanzania ni waoga.
(b) Kushindwa kutambua umuhimu wa Raila kwenye mapambano haya.
(c) Maandamano huratibiwa.
(d) Kumhusu Liz Truss.
(e) Siyo Kenya yote inayoandamana.

Umeonakana kuyapita majibu yale yote juu kwa juu kama kina joni tu.

Nikazie hapa tena kwenye umuhimu wa kuziona posts na nyuzi zote za rejea ili kuepuka kuhitaji kuandika yale yale tena tena. Nimemwelezea Hilo pia huyu ndugu denooJ kama ikimpendeza.
 
brazaj Kenya siasa zao zimekuwa - Shaped na ukabila. Kwa ivo hata watu wanaojitokeza mara nyingi kuunga mkono upande fulani hufuata sana mkondo huo wa ukabila.

Kwenye chaguzi za Kenya Profesa Mutahi Nguyi hutabiri kwa usahihi matokeo ya Uchaguzi kwa kuwa husema chaguzi za Kenya hufuata mkondo wa kikabila. Sasa huko watu kikuunga mkono chama "chao" na kukichangia ni rahisi sana na Kenya tuwe wakweli tu, kuna taasisi imara za kiraia kuliko huku.

Kwa mfano unaweza kuifananisha Knut na CWT?

Nikurejee tena kwenye hoja Yako hii ya kuruka ruka. Haya yapo kwenye mada:

Hakuna mahali popote Kenya (au kwingine) wanakodai kuwa hizi ni harakati za wajaluo au kuwa hata ni za kikabila, isipokuwa Tanzania."

Si Ruto, Gachagua au genge lao wanakosema kuwa wanakabiliwa na vuguvugu la kikabila. Uhuru, Musyoka, Karua, na wengi wanamwunga mkono Raila lakini si wajaluo.

Tatizo ni kuwa mtanzania ni mjuaji mno!

Ujuaji huu tumepandikizwa na ma CCM kiasi uwezo wa kujifunza kwa wengine umekuwa zero:

Makamanda tunayo ya kujifunza kwa Raila Odinga

Tujifunze vipi wakati tunajua Kila kitu?

Chadema ya leo ndiyo hii. Chadema haikuwa hivi:

Tuna Imani na CHADEMA hii, wala si nyingine

Ya nini kujaribu kujielekeza CWT wakati kwetu kunateketea?

Makamanda, elimu Haina mwisho:

Wafuasi wa Zumaridi wanapotoa Somo kwa Makamanda

Tusishupaze shingo tuanza na primaries za haki, wazi, huru na za kidemkrasia. Wagombea wajielekeze kwenye kujibu agenda na malengo yetu kwa vitendo.

Tuwapime kwa matokeo na wadumu kwa uungwaji mkono, si vinginevyo.
 
Hapa hatukomai tunayosimamia wala kiimani bali tunajadiliana kwa hoja kutambua changamoto zinazotukabili. Tofautisha mijadala ya kidini ambako tunayosimamia yaani imani ndiyo yanayojadiliwa.

Inafauhamika kuwa tofautiana kwa hoja kwenye harakati zozote za ukombozi ni jambo la afya tu ndugu.

"Kwamba iifano ninayotoa kuwa haiendani na unachokizungunzia?"

Ninadhani zaidi sana unachokizungunzia ni kuwa watanzania ni waoga. Hilo ninalipinga kwa hoja. Si sahihi kudhani JKNIA LIssu #1 au Kiluvha showdown zilikuwa nyepesi kama kihivyo.

View attachment 2590428

Hao walikuwa mamwela wavunja miguu ya watu wenyewe tena kwenye ubora wao.

Kipindi hicho Sirro na Mambosasa walitaka asiende mtu JKNIA vinginevyo angevunjwa miguu. Lissu Kiluvya njiani kwenda pwani ilikuwa hivyo hivyo.

Ninadhani hukuwepo kwenye matukio mawili haya kiasi kwamba kutaka kuyadogosha hivi ni mambo kushangaza sana. Hii ndiyo Ile waswahili wanasema mzigo wa mwenzio kwako ni kama kanda la sufi. Sidhani kama Lissu anakubakiliana na petty statements kama hizi za kuwa hizo zilikuwa sherehe.

Mengine uliyoandika sasa kwamba umeikana hadithi ya kuhalalisha kulamba asali, beberu anasema yanakuwa trivial. Yaani kwa kiswahili yanakuwa mwenye macho haambiwi tazama. Kimahesabu inakuwa ni sawa na namba + 0.

Hukuandika lolote kuhusu kuangaliana usoni kwa maana yake kamili. Mfano ziko moral obligations za waume wa ma COVID 19 kuendelea kuwa viongozi wetu?

Hukuandika lolote kuhusu nyomi ya angalau wanachadema 2,000 kwenye kuweka mazingira ya kutokamatwa Mbowe, wala hata kutambua tu kwamba BAVICHA ni Chadema pia.

Kwa sababu ya issues za muda niombe tuwe tayari kusoma rejea za posts na nyuzi. Kuandika jambo lile lile mara kibao hakuwezi kuwa na tija.

Kwa hapa ni kurejee kwenye post niliyomjibu bwana Allen Kilewella nikimwomba (bila mafanikio) tuwe na msingi mmoja wa majadiliano badala ya hii ya kuruka ruka huku na kule.

Kwangu post hiyo ni namba 124. Kwenye post hiyo nilikuwa nimeainisha hoja zake sita ambazo nilizijibu kwa mapana na marefu yake.

(a) Kwamba watanzania ni waoga.
(b) Kushindwa kutambua umuhimu wa Raila kwenye mapambano haya.
(c) Maandamano huratibiwa.
(d) Kumhusu Liz Truss.
(e) Siyo Kenya yote inayoandamana.

Ninatambua huyo bwana kama ilivyokuwa kina joni, Paskali na wenzao walichagua kutokuwa wameiona.
Una kipaji cha kuandika sana, Hongera.

Naamini ukijisoma vizuri kwanza utaona vile unavyojipinga mwenyewe licha ya maneno yako mengi.

Kwasababu kwanza unaonekana kulalamika watz wamekosa viongozi wa kuwa-organise, but ajabu, at the same time unamuonesha Lissu kama kiongozi aliyefanikiwa kwenye hilo, kwa hiyo hapa tunakubaliana viongozi tunao.

Sasa mpaka hapo tatizo letu ni viongozi, au ni sisi watanzania wenyewe?

Ndio maana nakwambia tatizo letu sio viongozi, tatizo letu ni sisi tunaolala licha ya maumivu tunayopata huku tukisubiri kuamshwa na viongozi, na huku kulala ndio uoga wenyewe.

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
 
Mkuu waache walale usingizi wakiamka itakuwa kumekucha. Watanzania tunafunzwa siasa mashuleni/vyuoni kama somo la lazima na huenda athari ya hilo ni haya tunayoshuhudia sasa. Tumekuwa watu wa maneno mengi vitendo hakuna.
Huko kulala usingizi unakopazungumzia ndio uoga wenyewe, sioni sababu ya kusubiri kuamshwa ikiwa bei ya vyakula inazidi kupaa na kumuumiza yule aliyelala, kwanini uendelee kulala kwenye mazingira magumu kama hayo?

Au ndio kuwasubiri viongozi? wale wanaweza kuwa hawaumizwi na ukali wa gharama za maisha kama raia wa kawaida, ni sisi raia ndio wenye jukumu la kuwaamsha viongozi ili watuongoze kule tunapotaka kwenda, but huwezi kuwaongoza watu waliopo vitandani!.

Hapo utaona raia ndio tunawakatisha tamaa viongozi, halafu ajabu tunajiuliza viongozi wako wapi, bado nasisitiza; tatizo letu ni ujinga wa kusubiri kuamshwa licha ya matatizo tuliyonayo, na uoga, unaotufanya tuendelee kulala vitandani licha ya maumivu tuliyonayo.

Case closed.

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
 
Una kipaji cha kuandika sana, Hongera.

Naamini ukijisoma vizuri kwanza utaona vile unavyojipinga mwenyewe licha ya maneno yako mengi.

Kwasababu kwanza unaonekana kulalamika watz wamekosa viongozi wa kuwa-organise, but ajabu, at the same time unamuonesha Lissu kama kiongozi aliyefanikiwa kwenye hilo, kwa hiyo hapa tunakubaliana viongozi tunao.

Sasa mpaka hapo tatizo letu ni viongozi, au ni sisi watanzania wenyewe?

Ndio maana nakwambia tatizo letu sio viongozi, tatizo letu ni sisi tunaolala licha ya maumivu tunayopata huku tukisubiri kuamshwa na viongozi, na huku kulala ndio uoga wenyewe.

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app

Sina shaka na uwezo wangu kujadiliana mambo kwa uwazi na kwa hekima.

Kwamba Lissu ni mmoja wa watu hawa kwenye list hii:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Hilo hata johnthebaptist na mambuzi wenziwe wote wakiwamo wa pale Lumumba wanalijua. Kwani Umewahi kuwasikia wakijibizana naye kihasara hasara?

Zingatia kauli hii ya JK, 2010:

Kikwete: Ni bora Slaa awe Rais kuliko Tundu Lissu kuwa mbunge

Kwamba Lissu ni zaidi ya Raila hilo pia linajulikana.

Tuliopo tunao usubiri wito wakr ni wengi wa kumwaga.

Alipo tupo.
 
Sina shaka na uwezo wangu kujadiliana mambo kwa uwazi na kwa hekima.

Kwamba Lissu ni mmoja watu hawa kwenye list hii:

Tusilaumiane: Wako wapi kina Nyerere, Maalim Seif, Mtikila, Julius Malema au kina Tutu

Hilo hata johnthebaptist na mambuzi wenziwe wote wakiwamo wa pale Lumumba wanalijua. Kwani Umewahi kuwasikia wakijibizana naye kihasara hasara?

Zingatia kauli hii ya JK, 2010:

Kikwete: Ni bora Slaa awe Rais kuliko Tundu Lissu kuwa mbunge

Kwamba Lissu ni zaidi ya Raila hilo pia linajulikana.

Tuliopo tunao usubiri wito wakr ni wengi wa kumwaga.

Alipo tupo.
Ndio maana nikauliza, huko kusubiri wito wao mpaka lini? una hakika naye anayapitia maumivu yetu wengine?

Kwanini sie tulale tukisubiri kuamshwa, kwanini tusiwaoneshe tuko tayari kupigania haki zetu, ili sasa nao watuone commitment yetu ili watu organise?!

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
 
Ndio maana nikauliza, huko kusubiri wito wao mpaka lini? una hakika naye anayapitia maumivu yetu wengine?

Kwanini sie tulale tukisubiri kuamshwa, kwanini tusiwaoneshe tuko tayari kupigania haki zetu, ili sasa nao watuone commitment yetu ili watu organise?!

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app

Ya kwako ni vicious cycle ambayo hakitakaa kutokea. Hivyo ni kama yale ya yai na kuku kipi kilianza.

Raila kahamasisha na katoa wito. Hizo ni kazi za viongozi.

Kwa nini hutaki wazifanye kazi hizo?

Wito hutolewa kiongozi wa shughuli. Hivyo ndivyo kote imekuwa.

Amefanya hivyo Raila. Kafanya hivyo Malema. Walifanya hivyo kina Maalimu Seif, Mandela, Tutu, Mtikila nk.

Wakifanya hivyo kina Dkt. Slaa na Chadema.

Tumeomba viongozi wasio tayari kuwaamsha watu na kuwaongoza kwenye harakati hizi wapishe au tuwaondoe.

Wenye ari za kina Lissu mbona wapo wengi wa kumwaga.

Kulikoni kuwaweka kina Mbappe au Messi benchi kwenye fainali world cup wakati timu zote mbili zinataka ubingwa?

Tuchague viongozi kufanikisha agenda na malengo yetu. Unaweza kaa, huwezi nje.

Taabu Iko wapi hapo ndugu?
 
Ya kwako ni vicious cycle ambayo hakitakaa kutokea. Hivyo ni kama yale ya yai na kuku kipi kilianza.

Raila kahamasisha na katoa wito. Hizo ni kazi za viongozi.

Kwa nini hutaki wazifanye kazi hizo?

Wito hutolewa kiongozi wa shughuli. Hivyo ndivyo kote imekuwa.

Amefanya hivyo Raila. Kafanya hivyo Malema. Walifanya hivyo kina Maalimu Seif, Mandela, Tutu, Mtikila nk.

Wakifanya hivyo kina Dkt. Slaa na Chadema.

Tumeomba viongozi wasio tayari kuwaamsha watu na kuwaongoza kwenye harakati hizi wapishe au tuwaondoe.

Wenye ari za kina Lissu mbona wapo wengi wa kumwaga.

Kulikoni kuwaweka kina Mbappe au Messi benchi kwenye fainali world cup wakati timu timu zote mbili zinataka ubingwa?

Tuchague viongozi kufanikisha agenda na malengo yetu. Unaweza kaa, huwezi nje.

Taabu Iko wapi hapo ndugu?
Kwasababu sisi tumelala ndio maana tunawasubiri viongozi mpaka wajiskie ndio watuamshe, Lissu alijiskia akatuamsha, basi tumsubiri akijiskia tena atatuamsha..

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
 
Hapo hakuna maajabu automaticaly mavuno yameshaanza kwahiyo ndani ya wiki mbili zijazo bei za vitu mbali mbali zitashuka maeneo karibu yote
 
Suala la utawala bora lina maana yoyote kwako? Au ni mpaka nikuwekee picha halisi za mabulungutu ya noti na wezi wetu?

View attachment 2588198

Wapi nilipo attack personality? Kulikoni kuniwekea maneno mdomoni ndugu?

Tofautisha swali na kauli (statement).

Angalizo: Vinginevyo inaweza kuwa muhimu kufahamu kiwango chako cha elimu Ili kujua scope ya mjadala.

"Kwa kweli tuna kazi kubwa sana ya kuutokomeza ujinga kama wako, Tanzania."
Mabulungutu yote hayo wameyaficha Uchina?
 
Hapo hakuna maajabu automaticaly mavuno yameshaanza kwahiyo ndani ya wiki mbili zijazo bei za vitu mbali mbali zitashuka maeneo karibu yote

Ndiyo Ruto, Gachagua au genge lao walivyokwambia mjomba? Tatizo la mtanzanzania ni ujuaji.
 
Huko kulala usingizi unakopazungumzia ndio uoga wenyewe, sioni sababu ya kusubiri kuamshwa ikiwa bei ya vyakula inazidi kupaa na kumuumiza yule aliyelala, kwanini uendelee kulala kwenye mazingira magumu kama hayo?

Au ndio kuwasubiri viongozi? wale wanaweza kuwa hawaumizwi na ukali wa gharama za maisha kama raia wa kawaida, ni sisi raia ndio wenye jukumu la kuwaamsha viongozi ili watuongoze kule tunapotaka kwenda, but huwezi kuwaongoza watu waliopo vitandani!.

Hapo utaona raia ndio tunawakatisha tamaa viongozi, halafu ajabu tunajiuliza viongozi wako wapi, bado nasisitiza; tatizo letu ni ujinga wa kusubiri kuamshwa licha ya matatizo tuliyonayo, na uoga, unaotufanya tuendelee kulala vitandani licha ya maumivu tuliyonayo.

Case closed.

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app

Sina uhakika ni kwa nini unahangaika mno kuona kuwa viongozi hawana wajibu wowote kwenye harakati za mapambano.

Raila, Musyoka, Karua na wenzao hawana njaa Lakini ndiyo walio vinara wa maandamano Kenya:

Maalimu Seif, Tutu, Mandela, Malema, Nyerere, Mtikila, Castro, Che Guevara, nk, hawajapigania haki kwa maana yako hiyo finyu kuwa walikuwa waathirika, waathirika zaidi, hawakuwa viongozi au kuwa walikuwa viongozi waliosukumwa na wafuasi wao.

Kwani uongozi maana yake nini?

Uongozi ni kitendo cha kuongoza kikundi cha watu. Kuongoza ni kujua malengo ya wale wanaoongozwa na njia ya kufikia malengo hayo.

Kiongozi asiyejua malengo ya wafuasi wake wala kujua njia za kuyafikia, huyo hafai.

Wajibu wa kiongozi ni kujua malengo ya wanaoongozwa na njia za kuwafikisha kwenye malengo hayo.

"Viongozi wasiojua malengo yetu wananchi, wala namna ya kutufikisha kwenye malengo yetu hayo, hao ni wa nini?"

Wajibu wa wafuasi ni kuona kuwa viongozi wanatekeleza wajibu wao. Katika hali kama hii ambapo viongozi hawatekelezi wajibu wao ipasavyo, wajibu wa wafuasi ni mmoja tu, wa kuwafurusha viongozi hao kutoka madarakani.

Ikumbukwe viongozi hawa wanalipwa na wanapogombea hujinadi kuwa wanayajua malengo yetu na wanayo mIarobaini ya kutufikisha.

"Gari halifiki wanakokwenda abiria analaumiwa vipi abiria?"

Ninakubaliana na nadharia ya usingizi kwa wananchi kulala kwa kuendelea kuwaendekeza madarakani viongozi kama hawa wasiokuwa na tija. Hatukupaswa kuwavumilia viongozi wa namna hii kwa kipindi chote hiki. Kwa hakika wametuchelewesha sana.

Wananchi tuna uchaguzi (options) gani kwenye hali hizi:

1. Kama vyama hivi ni vyetu, basi tuwang'oe sasa viongozi mamluki hawa wasiojua wajibu wao. Tuweke viongozi wazalendo watakao yaheshimu malengo yetu na kujua namna ya kutufikisha tuendako.
2. Kama vyama hivi si vyetu, basi ni vyama mamluki. Tuachane na vyama mamluki sasa visivyohitaji uwajibikaji. Tujiunge na vyama makini vya kizalendo vilivyopo kama vipo, au tuanzishe vyama vyetu vingine vitakavyoongozwa kama tunavyotaka sisi.

Kuku asiyekuwa na kichwa atembee kuelekea upande gani?

Cc: Zawadini
 
Kwasababu sisi tumelala ndio maana tunawasubiri viongozi mpaka wajiskie ndio watuamshe, Lissu alijiskia akatuamsha, basi tumsubiri akijiskia tena atatuamsha..

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app

Ukiwa unasema tumelala kwa kuwa hatujachukua hatua kivitendo kuwataka watoke madarakani utakuwa uko sahihi kabisa.

"Gari halifiki wanakokwenda abiria analaumiwa vipi abiria?"

Nadhani lawama pekee Kwa abiria ni kutomwajibisha dereva kwenye usukani mapema iwezekanavyo.

Ikumbukwe viongozi wana wajibu wa kujua malengo yetu na njia za kutufikisha tuendako kama tunavyotaka sisi.

Kama hawafanyi wajibu wao, itakuwa ni wa nini viongozi hao?
 
Huko kulala usingizi unakopazungumzia ndio uoga wenyewe, sioni sababu ya kusubiri kuamshwa ikiwa bei ya vyakula inazidi kupaa na kumuumiza yule aliyelala, kwanini uendelee kulala kwenye mazingira magumu kama hayo?

Au ndio kuwasubiri viongozi? wale wanaweza kuwa hawaumizwi na ukali wa gharama za maisha kama raia wa kawaida, ni sisi raia ndio wenye jukumu la kuwaamsha viongozi ili watuongoze kule tunapotaka kwenda, but huwezi kuwaongoza watu waliopo vitandani!.

Hapo utaona raia ndio tunawakatisha tamaa viongozi, halafu ajabu tunajiuliza viongozi wako wapi, bado nasisitiza; tatizo letu ni ujinga wa kusubiri kuamshwa licha ya matatizo tuliyonayo, na uoga, unaotufanya tuendelee kulala vitandani licha ya maumivu tuliyonayo.

Case closed.

Sent from my SAMSUNG-SM-G900A using JamiiForums mobile app
1. Huenda umeelewa vingine. Mimi nimeandika Kiswahili - lugha ya taifa. Ili kujua vyema nilichokiandika ni sharti uijue hiyo lugha niliyoiandikia.
2. Tatizo letu sio kupanda bei ya vyakula pekee. Tuna matatizo mengi na hili la bei likiwa ni moja tu ya mambo hayo.
3. Hilo unaloliita kusubiri kuamshwa wala haliko ktk mawazo yangu. Mimi nimesema "waache walale usingizi wakiamka ..." Hivi undhani waamshwe na nani? Hivi hizi kelele hawazisikii? Au ni kujitia pambani?
4. Katika mapambano mukianza kunyoosheana vidole hamtafika. Katika hili brazaj kajitahidi kuliweka sawa au kulitolea maelezo ambayo naamini yanaeleweka - kwa anayetaka kuelewa
 
rutomaize-jpg.2588177


Daa, jamaa yangu wanamchosa sana. Hasa huyo kibabu, haeleweki anataka nini, yeye ni vurugu tu.
 
rutomaize-jpg.2588177


Daa, jamaa yangu wanamchosa sana. Hasa huyo kibabu, haeleweki anataka nini, yeye ni vurugu tu.

Ni Tanzania tu ambako kudai haki kunaitwa vurugu. Bado tunayo safari ndefu. Hata baadhi ya CDM uchwara nao wanaita hivyo. Tulipo sasa tusubirie katiba ya kupewa. Kwamba hatutaki vurugu.
 
Ni Tanzania tu ambako kudai haki kunaitwa vurugu. Bado tunayo safari ndefu. Hata baadhi ya CDM uchwara nao wanaita hivyo. Tulipo sasa tusubirie katiba ya kupewa. Kwamba hatutaki vurugu.

Usikariri mambo, maandamano siyo njia pekee ya kudai haki.
 
Back
Top Bottom