mr gentleman
JF-Expert Member
- Aug 1, 2012
- 3,222
- 4,689
Ameandika hivi kwenye facebook. page yake
"Tahadhari /Ombi:
Kuhusu wimbo "Mdogo Mdogo" wa Msanii Diamond uliofanyiwa remix na kuingizwa maneno ya kampeni yenye mvuto na ladha ya kipekee na kusambazwa Watsap Groups.Pamoja na nia njema nyuma yake,Kwanza naomba nikiri tuna vijana wenye vipaji vikubwa
vya ubunifu .
Pili,kwa unyenyekevu mkubwa naomba waliobuni na kusambaza wimbo huu wasitishe kwa sababu ;
1: Muda wa kampeni bado
2:Sheria namba 7 ya mwaka 1999 inalinda hakimiliki na hakishiriki ya kazi za wasaniii(Ant-Piracy Law.Sidhani kama Mwanamuziki Diamond amelipwa au ametoa ridhaa yake
3:Unakinzana na msimamo wangu na wa chama chetu kisera katika kupigania haki za wasanii.
4:Nitakosa "moral authority" ya kukemea unyonyaji wa haki za wasanii na hivyo taasisi nitakayoiongoza itakosa nguvu ya kimaadili katika kusimamia haki
5:Hata kama kungekua na malipo ,kipaumbele tungewapa wanamuziki ambao wamejipambanua hadharani kuwa wanaunga mkono harakati za
mabadiliko.Wapo ndani ya chama chetu.Kwa kufanya hivyo tungekua tumetoa mchango wetu kwa wasanii hao 'Universal brotherhood'.
Sasa basi kwa kuwa kwenye remix ya wimbo huo kama wengi mlivyousikia imetajwa "Team ya Ushindi,Team Ben Saanane',Ninao wajibu wa kimaadili (Moral Responsbility ) wa kuomba radhi
kwa Msanii Diamond na pia kwa wasanii waliopo hapa kwa niaba ya wasanii wote.
Tunaendelea kuonyesha mfano bora kwa wanasiasa wanaotumia wasanii kinyonyaji na tumeendelea kuonyesha kwa vitendo kile tunachohubiri .
Tuendelee kuwa na msimamo mkali katika kulinda na kupigania haki za wasanii Wasanii Karibuni CHADEMA,Tunakotenda tunayohubiri juu ya kupigania haki .
Aluta Continua,Victory Ascerta...!"
"Tahadhari /Ombi:
Kuhusu wimbo "Mdogo Mdogo" wa Msanii Diamond uliofanyiwa remix na kuingizwa maneno ya kampeni yenye mvuto na ladha ya kipekee na kusambazwa Watsap Groups.Pamoja na nia njema nyuma yake,Kwanza naomba nikiri tuna vijana wenye vipaji vikubwa
vya ubunifu .
Pili,kwa unyenyekevu mkubwa naomba waliobuni na kusambaza wimbo huu wasitishe kwa sababu ;
1: Muda wa kampeni bado
2:Sheria namba 7 ya mwaka 1999 inalinda hakimiliki na hakishiriki ya kazi za wasaniii(Ant-Piracy Law.Sidhani kama Mwanamuziki Diamond amelipwa au ametoa ridhaa yake
3:Unakinzana na msimamo wangu na wa chama chetu kisera katika kupigania haki za wasanii.
4:Nitakosa "moral authority" ya kukemea unyonyaji wa haki za wasanii na hivyo taasisi nitakayoiongoza itakosa nguvu ya kimaadili katika kusimamia haki
5:Hata kama kungekua na malipo ,kipaumbele tungewapa wanamuziki ambao wamejipambanua hadharani kuwa wanaunga mkono harakati za
mabadiliko.Wapo ndani ya chama chetu.Kwa kufanya hivyo tungekua tumetoa mchango wetu kwa wasanii hao 'Universal brotherhood'.
Sasa basi kwa kuwa kwenye remix ya wimbo huo kama wengi mlivyousikia imetajwa "Team ya Ushindi,Team Ben Saanane',Ninao wajibu wa kimaadili (Moral Responsbility ) wa kuomba radhi
kwa Msanii Diamond na pia kwa wasanii waliopo hapa kwa niaba ya wasanii wote.
Tunaendelea kuonyesha mfano bora kwa wanasiasa wanaotumia wasanii kinyonyaji na tumeendelea kuonyesha kwa vitendo kile tunachohubiri .
Tuendelee kuwa na msimamo mkali katika kulinda na kupigania haki za wasanii Wasanii Karibuni CHADEMA,Tunakotenda tunayohubiri juu ya kupigania haki .
Aluta Continua,Victory Ascerta...!"