Benchi la ufundi la Yanga SC linapaswa kumkanya kipa Diara apunguze kujiamini sana, ipo siku ataitumbukiza timu kwenye shimo la hewa

NALIA NGWENA

JF-Expert Member
Joined
Oct 6, 2016
Posts
10,587
Reaction score
13,425
Nilitazama mchezo wa Yanga vs Mtibwa Fc niliona kabisa alipaswa kuondoka na Clean sheet bila wasi wasi lakini kilichotokea alifungwa goli la kizembe/la kujitakia.

Mashabiki /wadau wa mpira hawakupiga kelele kwa kua Yanga iliibuka na ushindi mnono wa goli 4 kwa 1.

Ukitazama goli la Mtibwa sugar mfungaji alilifunga akiwa katikati ya uwanja baada yakuona Diara katoka golini akapiga mpira wakapata goli la kufutia machozi.

Hii siyo Mara ya kwanza Diara amekua na Tabia ya kutoka golini ipo siku timu itakosa point tatu muhi kwa uzembe/kujiamini sana kwa Diara.

Mfungaji wa goli la Mtibwa alisema "madhaifu ya kipa Diara ni kujiamini sana na ndiyo maana nilipiga mpira golini nikafunga"

Nichukue Fursa hii kuliambia benchi la ufundi la Yanga Sc kuwa waongee na Diara apunguze over confidence ipo siku ataikost timu kimasihara sihara.

Nawasilisha hoja.
 
Upo sahihi na hizi back pass za kucheza na backline zisizo na ulazima sana rejea mechi na ihefu .
Hii ni kazi ya kocha wa makipa
NAKAZIA MKUU UPO SAHIHI
 
Modern football inahitaji kipa ajiamini awe half beki kuanzia kwa Allison Becker, David Raya, Enderson , Andre Onana, Manuel Neuer , Donnaruma, Mike Maignan , Ter Stegen.
Na goli alilofungwa Djigui Diarra ni moja ya Changamoto ambayo haiepukiki kwa makipa ambao ni ball play
 
Hakatazwi kujiamni angalia kwanza nilichokiandika Kisha ukoment.

Huyo Andre onana unayemzungumzia hao Man u wenyewe hawana hamu nae.
 
ngoja nikwambie,goli lile sio kosa la diara,refa alishapuliza filimbi ya faulo,sasa diara hakuona umuhimu wa kuuzuia mpira,cha ajabu akaruhusu goli na faulo,sasa alitoa faulo ya nini,na ataruhusuje goli?
 
Diara anafanya modern goalkeeping. Ukipa wa zamani ukipata mpira unapiga mbele msajilini Hamis Kinye. Magoli kama yale EPL yamefungwa Tangu enzi za kina David Beckham tena yeye alifunga akiwa nusu yake uwanja.
 
ngoja nikwambie,goli lile sio kosa la diara,refa alishapuliza filimbi ya faulo,sasa diara hakuona umuhimu wa kuuzuia mpira,cha ajabu akaruhusu goli na faulo,sasa alitoa faulo ya nini,na ataruhusuje goli?
Kwani Diara kutokea vile ni Mara ya kwanza.?!

Haya Kama Refa alipuliza Filimbi ya Faulo kwa Nini lilihesabika goli mzee ??

Sikatai kuwa Diara ni Bora lakini over confidence itakuja kuwalaza wanayanga na viatu.
 
Diara anafanya modern goalkeeping. Ukipa wa zamani ukipata mpira unapiga mbele msajilini Hamis Kinye. Magoli kama yale EPL yamefungwa Tangu enzi za kina David Beckham tena yeye alifunga akiwa nusu yake uwanja.
Mimi nimezungumzia Over confidence Sasa wewe unapokuja lawama utadhani mimi nimekataa ubora wa Diara
 
Kwani Diara kutokea vile ni Mara ya kwanza.?!

Haya Kama Refa alipuliza Filimbi ya Faulo kwa Nini lilihesabika goli mzee ??

Sikatai kuwa Diara ni Bora lakini over confidence itakuja kuwalaza wanayanga na viatu.
Refa alikua kasha puliza foul kaangalie marudio uone
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…