SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 7,895
- 12,975
Benchikha alipokuja tu Simba, niliwahi kuja na nyuzi mbili nikitoa tahadhari kuwa mafanikio yake yanaweza kuwa duni kutokana na hali aliyoikuta Simba. Kwanza niliongelea suala la quality ya wachezaji aliopewa aende nao vitani. Pili nikaja kuongelea athari za kurithishwa migogoro kati ya wachezaji na viongozi ambayo yangeathiri utendaji wake wa kazi.
Yote niliyoyasema yameenda kutimia. Benchikha ameachwa amtegemee Ntibazonkiza kwa kile kinachosemekana na wengi kuwa mkataba wake unamlazimisha kumtumia. Kama hiyo haitoshi akanyang'anywa kina Phiri akaletewa kina Freddy. Leo hii eti watu wanasema kocha hana mbinu za ushindi. Yale yale ya siku zote kumuangushia kocha jumba bovu ili wengine wapone.
Benchikha ninayemjua mimi ni huyu katika clip hi hapa chini. Ni kocha anayetaka ikibidi kumkunja shati mchezaji wake asiyefuata maelekezo aweze kufanya hivyo. Sasa amekuja kwenye timu anakuta wachezaji wanaitwa magodfather, amekuta macaptain hawaeleweki, wengine ndiyo hao kina Chama wanapelekwa kamati za kina Sirro halafu kesi zao zinaisha juu kwa juu wakati yeye mwenyewe angeweza kulimaliza suala lake. Hapo sijawazungumzia kina Zimbwe, Inonga na Manula. Benchikha aliyeitwa General kabaki kuwa kocha wa kujikunyata kwenye benchi baada ya mechi.
Hana meno. Muondoleeni yoyote yule anayetaka aondoke na mleteeni yoyote yule anayemtaka. Hapo akishindwa ndiyo mumlaumu.
Pitia nyuzi hizi mbili kujua nilichowahi kusema kuhusu Benchikha pale alipokuja tu Simba.
Kwa Benchikha, Simba imeonyesha jeuri ya pesa sasa tunasubiri tuione pia kwa wachezaji wapya
Kosa kubwa limefanyika kumrithisha Benchikha migogoro ya zamani
Yote niliyoyasema yameenda kutimia. Benchikha ameachwa amtegemee Ntibazonkiza kwa kile kinachosemekana na wengi kuwa mkataba wake unamlazimisha kumtumia. Kama hiyo haitoshi akanyang'anywa kina Phiri akaletewa kina Freddy. Leo hii eti watu wanasema kocha hana mbinu za ushindi. Yale yale ya siku zote kumuangushia kocha jumba bovu ili wengine wapone.
Benchikha ninayemjua mimi ni huyu katika clip hi hapa chini. Ni kocha anayetaka ikibidi kumkunja shati mchezaji wake asiyefuata maelekezo aweze kufanya hivyo. Sasa amekuja kwenye timu anakuta wachezaji wanaitwa magodfather, amekuta macaptain hawaeleweki, wengine ndiyo hao kina Chama wanapelekwa kamati za kina Sirro halafu kesi zao zinaisha juu kwa juu wakati yeye mwenyewe angeweza kulimaliza suala lake. Hapo sijawazungumzia kina Zimbwe, Inonga na Manula. Benchikha aliyeitwa General kabaki kuwa kocha wa kujikunyata kwenye benchi baada ya mechi.
Hana meno. Muondoleeni yoyote yule anayetaka aondoke na mleteeni yoyote yule anayemtaka. Hapo akishindwa ndiyo mumlaumu.
Pitia nyuzi hizi mbili kujua nilichowahi kusema kuhusu Benchikha pale alipokuja tu Simba.
Kwa Benchikha, Simba imeonyesha jeuri ya pesa sasa tunasubiri tuione pia kwa wachezaji wapya
Kosa kubwa limefanyika kumrithisha Benchikha migogoro ya zamani