Bendera ya Tanzania Duniani

Kichuguu

Platinum Member
Joined
Oct 11, 2006
Posts
17,048
Reaction score
22,790
Elewa kuwa Tanzania ni kati ya nchi kumi tu tu duniani ambazo bendera zake zina diagonal strip. Ukiacha Brunei utashangaa kuwa nchi zote zenye bendera diagonals, ni za uchumi wa hali ya chini sana; ingawa Tanzania na Namibia tunaweza kujitutumua kwenye kundi hilo, lakini nyingine zote ni za maisha ya mashaka mashaka tu.

Bendera za nchi nyingine zote ama ni za rangi moja kubwa, au zina horizontal bars au zina vertical vertical bars au zina aina fulani ya msalaba wa kujumulisha (+) au wa kuzidisha (X). Kuna nchi ambazo bendera zake ni mchangayiko wa makundi hayo, kwa mfano Panama




Mifano ya bendera zenye msalaba ni kama vile Burundi, UK, Sweden na Jamaica kama zionekanavyo hapa chini


Mifano ya bendera zenye vertical bars ni pamoja na Ufaransa,Senegal, Romania na Nigeria kama hizi hapa


Mifano ya Bendera zeny horizontal bars ambazo ndizo nyingi zaidi dunaini ni pamoja na Kenya, Uganda, USA, na Ujerumani hapa chini


Bendera zenye rangi moja kubwa ni kama vile zile za Somalia, China, Uturuki na Saudi Arabia


Club ndogo special ya nchi zenye bendera za diagonal duniani ambamo Tanzania ni memba wake ni pamoja na:

(1) Republic of Congo -Tangu mwaka 1960

(2) Democratic Republic of Congo- tangu mwaka 1963 (ingawa ilibailishwa mwaka 197i lakini wakairudia tena mwaka 2006

(3) United Republic of Tanzania -Tangu mwaka 1964

(4) Brunei Darussalam- Tangu mwaka 1959

(5) Trinidad and Tobago -Tangu Mwaka 1962

(6) Solomon Islands -Tangu mwaka 1978

(7) St. Kitts and Nevis -Tangu mwaka 1983

(8) Namibia - Tangu mwaka 1990


(9)Bhutan -Tangu mwaka 1969

(10)Papua New Guinea


Ingawa kuna nchi nyingine, kwa mfano Marshall Islands na Seychelles, ambazo bendera zake zina pia diagonals, zao ziyo perfect diagonal kama ionekanavyo hapa
 

Attachments

  • 1657998098757.png
    3.4 KB · Views: 11
Hoja yako ya msingi ni nini sasa?
Maana sioni hoja hapo, unless kama hizo nyingine ulizo mention kama Burundi, Senegal etc pia zingekua ni diagonal!
Hii ni habari na hoja mchanganyiko, siyo siasa. Jifunze tu kelewa kuwa ni nchi chache sana dunaini zenye bendera diagonal na zote hazina maendeleo makubwa; ziko third world.
 
Kwahiyo nchi ni masikini kisa bendera yake ina diagonal strips?

So,ikibadili bendera yake na kua na hizo horizontal bar ndio itakua tajiri?
 
Kwenye katiba mpya inayokuja inabidi pia tubadilishe rangi ya bendera yetu angalau rangi nyekundu kuangazia maswala ya majanga ya vifo na mashujaa wa nchi yetu
 
Nakumbuka tu rangi ya kijani ni uoto wa asili,rangi ya bluu ni bahari,mito na maziwa,rangi ya njano ni madini(dhahabu), nyeusi ni rangi zetu waafrika...rangi nyeusi tena ile tiii kabisa yan dark kabisa, na ukiangalia rangi nyeusi kwa upande mwingine ni ushetani,nguvu za giza na vitu vibaya vibaya tu,kwanini rangi nyeusi kwenye bendera wakati Tanzania ina watu wa rangi mbalimbali au ndo uzalendo na kujikubali!...hiyo rangi ya njano iwakilishayo vito kama dhahabu, hivyo vito kweli vinatufaidisha?, mito,bahari na maziwa tunayatumia ipasavyo?...wakati mwingine nafikiri hata bendera za nchi zinahamasisha kitu fulani hivi cha kutia nguvu kidogo tu.
 
Kwahiyo nchi ni masikini kisa bendera yake ina diagonal strips?

So,ikibadili bendera yake na kua na hizo horizontal bar ndio itakua tajiri?
Hiyo ni conclusion yako ambayo ni mbaya na inatokana na kutokujua kusoma mambo viziru. Post haisemi kuwa nchi ni maskini kwa ajili ya bendera yake, kuna nchi nyingine ambazo bendera siyo diagonal lakini ni maskini zaidi. Nilichosema ni kuwa nchi zenye bendera hizi nyingi ni maskini; kwa mfano katika nchi zote za europe hakuna bendera diagonal.
 
Mkuu unajua maana ya question mark? sijafikia conclusion yeyote ile bali nimeuliza maswali.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…