Benk ya wafanyakaz wa serikar.

chipalila1

JF-Expert Member
Joined
Apr 6, 2012
Posts
259
Reaction score
32
Ndugu wana jf hivi wafanyakazi wote wa serikar ni lazima mishahara yao ipitie NMB? Kama n kweli kwann hivyo? Wanao jua tafadhar kuhusu hlo watujuze.
 
Sidhani kama wanalazimika kufanya hivyo. Except for waalimu. Taasisi zingine unatumia bank utakayo, ila tu malipo yanachelewa kwa siku kadhaa zaidi kwa ajili ya transactions. Na endapo unapata cheque zozote, inasumbua kama hauna nmb account.
 
Sidhani kama wanalazimika kufanya hivyo. Except for waalimu. Taasisi zingine unatumia bank utakayo, ila tu malipo yanachelewa kwa siku kadhaa zaidi kwa ajili ya transactions. Na endapo unapata cheque zozote, inasumbua kama hauna nmb account.

kwann wanachelewesha kama hujatmia Nmb acc?
 
hakuna ulazima wowote wa mtumishi wa serikali kupitishia fedha zake nmb (hususani kupitishia mishahara)
unaweza kutumia benki yeyote ile kutegemea na mazingira uliyopo.
NMB inatumika sana kwa sababu kwanza imesambaa karibu kila wilaya hapa tz sijui kwenye hizi wilaya mpya hivyo basi mtumishi wa serikali anayefanya kazi wilaya ambayo benki pekee iliyopo huko ni nmb kwa utashi mdogo tu lazima atumie nmb kupitishia mshahara wake kuepuka gharama za kuifata benki nyingine makao makuu ya mkoa.
pili serikali inatumia sana benki ya nmb kwa sababu serikali inamiliki shares nyingi sana kweye benki hii kumbukumbu zangu zianaonyesha kwamba serikali ilikuwa inamiliki 51% ya share hadi hivi karibuni ilipoamua kuuza 3% ya share zake kwa watumishi wa benki ya nmb.
Tatu watumishi wengi wa serikali tunatumia benki hii kupitisha mishahara yetu kwa sababu Serikali nayo inaitumia benki hii kuwalipa mishahara watumishi wake, mishahara ya watumishi wa serikali inapelekwa nmb benki ya nmb
ndiyo inasambaza kwenye benki nyingine, hapo sasa ndio kuna ucheleweshaji sisi ambao tunapitishia mshahara wetu nmb tutapata mapema, wale ambao wanapitishia benki nyingine wanachelewa manake hadi nmb waandike cheki nyingine kupeleka kwenye hizo benki kwa hiyo mlolongo unakuwa mrefu, sijui ni ujanja wao ili watumishi tupitishe mishahara yetu nmb. Kwa mf ofisini kwetu watumishi wanaopitishia mishahara yao nmb wanapata mishahara yao mapema kuliko wanaopitishia mishahara yao benki nyingine ambao watasubiri hadi nmb waipeleke kwenye hizo benki nyingine
 

mkuu ume eleza vzur mno nimekupata.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…