Benki tatu kuwekwa chini ya uangalizi: Hii ni sawa na kusema baada ya miezi hiyo zitafungwa

Wakuu,
Hivi benk kufa na taasisi za kifedha huwa ni dalili za ugonjwa gani vile....!?

Aaaah, naota kwa sauti. Nisamehewe bure.
 
Kengele imeshapigwa sasa, kila mwenye pesa zake aende faster kuchomoa pesa zake zote. Hakuna tena kulala hapo.

Na kama wewe ni mjanja zaidi(Mwizi??), kwa muda huu ndio wakati mzuri wa kwenda kuvuta mkopo kwenye hizo benki na kusepa zako maana hawataweza kuja kukufuatilia zaidi ikitokea wamefirisiwa.

Tahadhari nyingine kuu kwa watu wengine wenye pesa zao nyingi kwenye benki zingine ambazo ziko salama kwa sasa ni kuhakikisha salio la Akiba kwenye Akaunti benki halizidi 1.5milioni ili ikitokea zimefirisika basi unavuta mkwanja wako ukiwa vile vile.
 
kwa kuziweka chini ya uangalizi watu wengi watatoa pesa zao na kuzifanya zikose sifa hivyo uwezakano mkubwa zitafungwa
BOT haiangalii amana za wateja inaangalia mtaji wa benki husika. Ukiwa na amana za kutosha lakini mtaji kiduchu utafungiwa tu.
 
BOT ilikosea san ku publicize hizo bank tatu. Maan hapo kitakachofanyika wateja wote wataenda kutoa pesa zao na benki hizo zitashindwa kufikia target . Ni bora wangefanya kimya kimya tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…