Benki ya Dunia yaipatia Tanzania mkopo wa 1.8 Trillion. To be paid after 40 Years

mulisaaa

JF-Expert Member
Joined
Jun 16, 2017
Posts
6,969
Reaction score
7,027
Benki ya Dunia yaipa Tanzania Sh1.8 trilioni
Benki ya Dunia (WB)imeipatia Tanzania mkopo wa Sh1.8 trilioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi endelevu ya usambazaji maji vijijini na usafi wa mazingira katika wilaya 86 nchini.

BY Aurea Simtowe,Mwananchi asimtowe@mwananchi.co.tz

Mikoa ya Iringa, Mbeya, Tunduma na Sumbawanga imetajwa kuwa wanafuika wa fedha kwa kuunganishiwa umeme kutoka Zambia huku mkopo kwa ajili ya kufikisha umeme mkoani Kigoma ukiwa katika hatua za mwisho.

Dar es Salaam. Benki ya Dunia (WB)imeipatia Tanzania mkopo wa Sh1.8 trilioni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi endelevu ya usambazaji maji vijijini na usafi wa mazingira katika wilaya 86 nchini.

Pia fedha hizo zitatumika kuendeleza uunganishaji wa umeme kutoka Zambia katika mikoa minne ya kusini mwa Tanzania.

Katika fedha hizo Sh1.04 trilioni zimetengwa kwa ajili ya usambazaji wa umeme huku Sh800 bilioni ni kwa ajili ya utekelezaji wa miradi ya maji na usafi wa mazingira.

Akizungumza leo Septemba 7 katika hafla ya utiaji wa saini kati ya Benki ya Dunia na Tanzania, Katibu mkuu Wizara ya Fedha na Mipango, Dotto James amesema mkopo huo wenye masharti nafuu utasaidia katika kupunguza tatizo la maji kwa wananchi na kuhakikisha nishati ya umeme inawafikia watu wengi zaidi.

"Ni jukumu letu kama serikai kuhakikisha wananchi wanapata maji safi na kuwa katika mazingira rafiki lakini kwa upande wa vijijini bado ni changamoto kubwa hivyo ni lazima tuhakikishe tunawafikia kupitia vyanzo vya ndani au mikopo," amesema James

Kwa upande wa umeme, James amesema mkopo huo utaisaidia Taasisi katika kuongeza uzalishaji wa umeme na upanuzi wa Miundombinu ya kusafirishia umeme.

"Njia ya usafirishaji umeme kati ya Iringa, Kisada, Mbeya, Tunduma na Sumbawanga utakuwa na uwezo wa 400-kV, Vituo vidogo vya uzalishaji kati ya Sumbawanga, Tunduma, Kisada, Mbeya vitakuwa na 400kV huku ujenzi wa njia ya usafirishaji umeme kutoka Tunduma hadi Mpaka wa Zambia ukiwa na 330kv," amesema James.

Mkurugenzi Mkazi wa Benki ya Dunia, Bella Bird amesema licha ya kuwa Tanzania inakabiliwa na uchafu wa mazingira unaosababisha magonjwa kama kipindupindu lakini bado watanzania wanaonekana kuendelea kuboresha nyumba zao, amesema Bella.
 
Noooooo!!! Sasa hii tutauza Nchi ya Tanzania to repay the loan.
 
Noooooo!!! Sasa hii tutauza Nchi ya Tanzania to repay the loan.
After 40Years not bad we will pay. Tunawekeza kwenye maendeleo hasa vijijini. Nabado kuna mkopo mwingine world Bank watatoa. Hii ni soft loan.
 
πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ Uzuri ni kwamba tunakopesheka tena kwa kubembelezwa

Kuna mmoja huko alienda kwa Xi juzi kulazimisha pesa aliosaini akiwa na akili timamu kama mkopo on the spot iwe msaada ha πŸ˜‚ πŸ˜‚ πŸ˜‚ 😊

Xi kamuambia arudi kwanza nyumbani kwa vipimo zaidi pia majibu ya ombi lake atayapokelea huko huko aondoe kwanza jam Beijing

Ama kweli bangi nibangue nyanya ninyanyue
 
Hamna cha vipimo, hiyo ni geresha tu, asiaibike mbele ya wananchi wake, hawataki mkopesha kabisa.
 
own goal hio...wenzako hapa kila uchao wanaimba kenya mikopo mikopo mikopo.... tanzania tunajenga kwa hela yetu...tunanunua bidhaa kwa cash.....kisha wewe hapa unakuja kutangaza mkopo toka world bank we huoni umejipiga bao
Ni world Bank sio China or US and to be paid within 40 years. 1 trillion for electric power in rural areas and 800 billion for water supply in rural areasπŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ We put the money were the mouth is. World Bank has confidence with TZ. Kenya WB hamuwezi tia guu lenu kwa sasa.
Pia kuna pesa nyingine wanatoa muda sio mrefu. πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
Magufuli hasafiri lakini pesa zinakuja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…