Benki ya Posta mna mambo ya kizamani. Mnataka viambata vingi kutoka kwa Watumishi ili muwakopeshe. Ambao hatutaki usumbufu tutaendelea kuwakimbia

Benki ya Posta mna mambo ya kizamani. Mnataka viambata vingi kutoka kwa Watumishi ili muwakopeshe. Ambao hatutaki usumbufu tutaendelea kuwakimbia

Mwamuzi wa Tanzania

JF-Expert Member
Joined
Apr 7, 2020
Posts
15,486
Reaction score
45,256
Wiki iliyopita nilienda Benki ya Posta kuomba mkopo ili nifanye miradi yangu.
Dhamana kuu ni mshahara wangu.
Sasa cha ajabu naambiwa nilete
  • Picha zangu
  • Barua yangu ya mkono
  • Nakala ya kitambulisho cha NIDA
  • NAKALA YA KITAMBULISHO CHA KAZI.
  • Barua ya mwajiri
  • Barua ya kuajiriwa
  • Barua ya Kuthibitishwa kazini
  • Salary slips zenye muhuri
  • n.k, n.k
Niliwashangaa sana. Nikawaambia nakuja.

Nikaondoka mazima.
 
Cha ajabu ni bank ya serikali, itakua ilipewa mtaji kutoka kw apesa za wananchi lakini riba yake iko juu sana kama mabenki mengine.

TPB (Tanzania Commercial Bank) hawako smart kabisa.
 
Sio kwamba mabenki mengine ndio yana mambo ya kisasa zaidi. Kupata viambata vya kutosha ni muhimu kuhakikisha hakuna defaulters ukizingatia hii Bongo yetu ya wapigaji na watu wapenda shortcut, hio yote mkuu ni ya kujilinda na kulinda mali ya wadau wao.
 
Kwani pesa si wanatoa baada ya kujiridhisha kuwa mwajiri wangu ameingiza makato yao. Sasa usumbufu wote wa nini?
Mwajiri wangu atafanya uhuni?
Sio kwamba mabenki mengine ndio yana mambo ya kisasa zaidi !!!, Kupata viambata vya kutosha ni muhimu kuhakikisha hakuna defaulters ukizingatia hii Bongo yetu ya wapigaji na watu wapenda shortcut..., hio yote mkuu ni ya kujilinda na kulinda mali ya wadau wao...
 
Nadhani mashirika ya umma uangekuja na modality yenye u-private maana mfano pale Morogoro kwa wiki x4 hakuna network ila ukienda bank jirani network ipo plus TTCL ambao ni pacha wao ndio wenye fiber😩😩
 
Hizo benki waachiwe wahenga na makada wa CCM,sisi wengine hatuziwezi.
 
Back
Top Bottom