Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 128,308
- 245,426
Taarifa zinaonyesha kwamba Wanasheria wake tayari wamewasilisha ombi hilo kwa viongozi wa Yanga
Binafsi naunga mkono madai yake
========
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Samwel Lukumayi amesema wapo tayari kuachana na kipa wao Beno Kakolanya baada ya kukaa na wanasheria wao.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, alisema wamepokea barua ya mchezaji huyo akiwataka kuvunja mkataba nao.
"Kakolanya ametuandikia barua ya kutaka kuachana naye kwamba mkataba umevunjwa, tumeipokea barua hiyo na tunaipeleka kwa wanasheria wetu kuona itakavyokua," alisema Lukumayi.
Alisema fedha zake za mishahara tayari walishamlipa kama ambavyo wachezaji wengine walivyotakiwa kuzipata.
Aliongeza kwamba hawana kipingamizi cha kuzuia kuvunja mkataba wa mchezaji huyo kama wanasheria wataizinisha hivyo.
Kakolanya alikosekana katika kikosi hicho tangu mechi ya Yanga na Mwadui iliyofanyika mkoani Shinyanga kwa kushinikiza kudai fedha zake na ndipo kocha Mwinyi Zahera aliibuka na kusema kwamba hamuhitaji mchezaji huyo katika kikosi chake kutokana na utovu wa nidhamu.
Chanzo: Mwananchi
Binafsi naunga mkono madai yake
========
Makamu Mwenyekiti wa Yanga, Samwel Lukumayi amesema wapo tayari kuachana na kipa wao Beno Kakolanya baada ya kukaa na wanasheria wao.
Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, alisema wamepokea barua ya mchezaji huyo akiwataka kuvunja mkataba nao.
"Kakolanya ametuandikia barua ya kutaka kuachana naye kwamba mkataba umevunjwa, tumeipokea barua hiyo na tunaipeleka kwa wanasheria wetu kuona itakavyokua," alisema Lukumayi.
Alisema fedha zake za mishahara tayari walishamlipa kama ambavyo wachezaji wengine walivyotakiwa kuzipata.
Aliongeza kwamba hawana kipingamizi cha kuzuia kuvunja mkataba wa mchezaji huyo kama wanasheria wataizinisha hivyo.
Kakolanya alikosekana katika kikosi hicho tangu mechi ya Yanga na Mwadui iliyofanyika mkoani Shinyanga kwa kushinikiza kudai fedha zake na ndipo kocha Mwinyi Zahera aliibuka na kusema kwamba hamuhitaji mchezaji huyo katika kikosi chake kutokana na utovu wa nidhamu.
Chanzo: Mwananchi