Beno Kakolanya asaini mkataba wa miaka miwili Simba sports club

Msimu mzima wa Ligi kchezea Azam match ngapi?
Hajacheza mechi yoyote! Kule mbao ndiko anakostahili na mbao kacheza mechi chache tu!

Pengine hufuatilii mechi za mbao inapocheza na timu za daraja lake mara nyingi Metacha hachezi Golikipa aliyeko timu ambayo hastahili kuwepo kama kawaida ni kutoka kwa wajelajela Aron kalambo.
 
Biashara united inacheza Ligi Kuu au daraja la Chini lipi unalozungumzia hapa?
Biashara kucheza ligi kuu haina maana ina daraja sawa na Simba au Yanga.

Timu za daraja la juu Tanzania zipo tatu, timu za daraja la kati tuna Mtibwa sugar, Tanzania prison, Kagera sugar, n.k

Timu za daraja la chini tuna Biashara, KMC, Mbao, Lipuli, Mwadui n.k sijui unaelewa nini na maanisha?
 

Unatumia Vigezo gani kupanga hayo madaraja?
 
Unatumia Vigezo gani kupanga hayo madaraja?
Kigezo namba moja ukongwe, namba mbili mafanikio.

South Africa kuna timu inaitwa Polokwane ni kongwe vibaya mno imeanzishwa miaka ya 1800 huko ila haina mafanikio yoyote ila kinachoifanya kuwekwa katika orodha ya timu za daraja la kati ni ukongwe wake.
 
Mchawi wa BENO alikuwa Zahera ili Kindoki apate namba...
 
Kweli kabisa upo sawa, angekuwa na akili kama alikosa timu yoyote ya nje angeenda hata Azam au kmc kuliko kwenda kukaa benchi. Itakuwa vigumu kumtoa Manula .
Akili anayo... angeng'ang'ania timu ambayo haimlipi ndio angekuwa hana akili.
 
Mkuu tuvute tu subiri na muda utaongea, huyu Kakolanya kajimaliza, bora hata angeenda zake Azam fc au hiyo KMC
Anajiamini.. huko Azam aende Kabwili au Kindoki
 
Huku ni kutotumia akili vizuri unakataa dili la Biashara United Mara ambapo utakuwa na uhakika wa kucheza kila mechi unasaini Simba Sports Club ambayo ina makipa wanne, huna uhakika na namba yako ambapo unaenda kukaa Benchi muda wote!
Hata Yanga alikuwa na uhakika wa kucheza mechi nyingi... Yaani Mfano unataka De gea atoke MAN U aende Watford?..
Huko biashara aende Kindoki, BENO IS RED
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…