mjingamimi
JF-Expert Member
- Aug 3, 2015
- 42,209
- 51,004
Aende tu wakasugulishane benchi na Manula, Dida, NdutaTETESI: Inaelezwa kuna uwezekano katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo Simba ikamuacha golikipa wake Said Mohamed 'Nduda' ambaye anaonekana hana nafasi na nafasi yake ikazibwa na Beno Kakolanya.
Source: Shaffih Dauda IG
NB: Naona hapa ndio anaenda kuuwa kiwango chakeView attachment 967879
kwahiyo wachenzaji wenzake hawana familia, aende akanye huko
Anashauriwa na meneja wake ambae ni mnazi na kiongozi wa Mikia FC.
Sasa timu iko ktk hali ngumu kifedha, Mashabiki na wapenzi wa soka wanajua, wachezaji, kocha n benchi la Ufundi wote wanafahamu, sasa ww Kipa ni nani ugome ktk mazingira haya ushinikize ulipwe, wakati hali unaijua....wachezaji wengine nao wakifuata mkumbo na kugoma kutakuwa na timu kweli....Binafsi pamoja na Dai lake la haki, nasema atafute timu nyingine akacheze....kuvuruga team spirit iliyopo Yanga sasa ni sawa na kuvuruga kazi nzuri inayofanywa na Kocha Zahera......aende hata Simba aende tu....
Mchukueni nyie wenye hela
We unatia Kinyaa..Unatia huruma
Vya bure siku hizi vichache saana! kama mnataka awafanyie kazi hamna budi kumlipa. kwa yanga sishangai juzi tu sijui yondani sijui ajibu na bado.Anashauriwa na meneja wake ambae ni mnazi na kiongozi wa Mikia FC.
Umeongea vizuri kwa upande wa klabu lakini ukweli sisi kama mashabiki was Mpira tuwe tunaangalia na upande wa mchezaji beno kazungushwa sana kulipwa pesa zake za usajili toka msimu uliopita na pia hajalipwa mishahara inasemekana sasa ni miezi minne na huku yeye ana familia inamtegemea kutoka kwenye hiyo kazi yake yeye hajalipwa lakini anaona wachezaji wengine wanasajiliwa pia wanalipwa pesa hata kama cyo zote unafikiri yeye atajisikiajeAaaa! Beno hasomi alama za nyakati, kazi yake ya ugolikipa ni kazi takatifu haitaki vitendo kama hivyo alivyofanya. Hii ni sawa na kuitia najisi kazi yake ya ugolikipa.
Hakuna timu makini duniani itapenda golikipa mwenye historia ya tabia kama hiyo ya kugoma anapokuwa na shida hasa ya kifedha. Hii inamaanisha kuwa golikipa kama Beno ana uwezo wa kuchukua fedha kutoka timu pinzani na kuiuza mechi ili kukidhi shida yake ya kifedha ambayo mwajiri ameshindwa kuiona au kuitimiza.
Aliyemshauri Beno kufanya hivyo alikosea sana kupita kiasi. Beno hataaminika pahala popote duniani kucheza kama golikipa, maana hawatajua akikasirishwa na uongozi atachukuwa hatua gani kama sehemu suluhisho ya shida yake.
Namshauri Beno aende Yanga akapige magoti kuomba msamaha kwa alichofanya ili kujisafisha. Yeye bado mdogo sana, anazo kesho nyingi sana ambazo zitahitaji umakini na trust ya hali ya juu wa wadau mbalimbali anaowafahamu na asiowafahamu.
Aendelee na mgomo wake atalipwa zikipatikana...lkn hatuwezi kuacha kulipa waliopo na wanaitumikia klabu sasa kwa kidogo kinachopatikana, eti alipwe aliye ktk mgomo. nashauri alipwe pale inapotokea kuna Ziada...na afunguliwe mlango wa kutokea... hata Dodoma United ni timu aende akadake ukoUmeongea vizuri kwa upande was klabu lakini ukweli sisi kama mashabiki was Moira tuwe tunaangalia na upande wa mchezaji beno kazungushwa sana kulipwa pesa zake za usajili toka msimu uliopita na pia hajalipwa mishahara inasemekana sasa ni miezi sita na huku yaye ana familia inamtegemea kutoka kwenye hiyo Nazi yake yeye hajalipwa lakini anaona wachezaji wengine wanasajiliwa pia wanalipwa pesa hata kama cyo zote unafikiri yeye atajisikiaje
Anataka kumfuata Niyonzima. Yetu macho tu.TETESI: Inaelezwa kuna uwezekano katika kipindi hiki cha usajili wa dirisha dogo Simba ikamuacha golikipa wake Said Mohamed 'Nduda' ambaye anaonekana hana nafasi na nafasi yake ikazibwa na Beno Kakolanya.
Source: Shaffih Dauda IG
NB: Naona hapa ndio anaenda kuuwa kiwango chakeView attachment 967879
Tanzania kuna timu yenye hela? mchezaji anatakiwa awe na nidhamu ndani na nje ya uwanja akilenga kwenda waliko akina Samatta, Msuva, Chilunda. Yanga, Simba, Azam liwe lango kuu la kutokea kwenda huko ziliko hela kwa wachezaji. Kakolanya amebugi, anataka kununua ndege akiwa hapahapa na timu za bongo. Nani mwenye akili timavu atamsajili mchezaji tena kipa mwenye CV kama ya Beno? Na mbaya zaidi kwake ameondoka lakini timu aliyoiacha inaendelea kufanya vizuri bila yeye. Dhambi ya aina hii itaendelea kumtesa milele kila atakakokwenda.Vya bure siku hizi vichache saana! kama mnataka awafanyie kazi hamna budi kumlipa. kwa yanga sishangai juzi tu sijui yondani sijui ajibu na bado.
Aende tuu huko Mikia,kila mbuzi hula urefu wa kamba yake. Nyie ndio mnajifanya hamuoni hali halisi ya kiuchumi ya Club. Amfuate Niyonzima.Hakuna mchezaji wa ligi kuu -TPL aliyenyanyaswa na yanga kama kama beno, apo alipo anadaiwa milioni 5 na timu aliyokuwa amesajiriwa nayo baada ya kutangaziwa na yanga kuwa anaachwa, apo alipo kwenye mkono wake wa kulia kuna mkataba wa milioni30 kutoka simba ambao bado hajausaini, mkono wa kushoto ana madeni chungu mzima yaliyo sababishwa na yanga na wanayanga tumeshindwa kumchangia japo milioni10 ili kumbakisha lakini kwa yondani iliwezekana.......alooo mistake tufunguke hapa yasiyo paswa....
Kucheza Yanga au Simba ni ndoto ya kila mchezaji Tz hata bila kulipwa shilingi yoyote, maana hapo ni mahali ambapo mchezaji anapata bahati ya kufundishwa na makocha wa kaliba ya juu sana kama Patrick, Zahera, Lwandamila, Prujim, nk ambao timu nyingine ndogo hawapatikani. Lakini kupata namba kwenye timu kubwa kama Simba, Yanga na Azam pia ni kazi kubwa na Simba, Yanga na Azam ni mahali ambapo mchezaji ni rahisi kucheza mechi za kimataifa. Beno hakuangalia mbali.....Umeongea vizuri kwa upande wa klabu lakini ukweli sisi kama mashabiki was Mpira tuwe tunaangalia na upande wa mchezaji beno kazungushwa sana kulipwa pesa zake za usajili toka msimu uliopita na pia hajalipwa mishahara inasemekana sasa ni miezi minne na huku yeye ana familia inamtegemea kutoka kwenye hiyo kazi yake yeye hajalipwa lakini anaona wachezaji wengine wanasajiliwa pia wanalipwa pesa hata kama cyo zote unafikiri yeye atajisikiaje
Huyu ana leta mahaba niue.yaani beno apigike pale golini.akumbane na uchawi pale golini akwepe mawe yasiyoonekana.mwisho wa mwezi una mwambia mshahara hamnaa?Akae golini na njaa,akiziona nyota 5!?.
Mimi nataofautiana na wewe, Beno anadai pesa yake kyweli uongozi kwa sasa hauna fedha maana naambiwa ata wachezaji wanasajiliwa na baadhi ya wadau wa yanga. Kinachotakiwa uongozi na wadau watafute namna ya kusaidiana kupunguza madeni makubwa ya wachezaji ili wachezaji wahisi wanathaminiwa. Beno namshauri atafute namna ya kulishughulikia tatizolake uku akiwa anacheza kulinda kipaji chake na nyota inayo ng'aa kwa sasa, kwa kiwango alicho nacho sasa akiendelea kukaa langoni huwezi jua, anaweza akapata timu nje ya nchi.Aaaa! Beno hasomi alama za nyakati, kazi yake ya ugolikipa ni kazi takatifu haitaki vitendo kama hivyo alivyofanya. Hii ni sawa na kuitia najisi kazi yake ya ugolikipa.
Hakuna timu makini duniani itapenda golikipa mwenye historia ya tabia kama hiyo ya kugoma anapokuwa na shida hasa ya kifedha. Hii inamaanisha kuwa golikipa kama Beno ana uwezo wa kuchukua fedha kutoka timu pinzani na kuiuza mechi ili kukidhi shida yake ya kifedha ambayo mwajiri ameshindwa kuiona au kuitimiza.
Aliyemshauri Beno kufanya hivyo alikosea sana kupita kiasi. Beno hataaminika pahala popote duniani kucheza kama golikipa, maana hawatajua akikasirishwa na uongozi atachukuwa hatua gani kama sehemu suluhisho ya shida yake.
Namshauri Beno aende Yanga akapige magoti kuomba msamaha kwa alichofanya ili kujisafisha. Yeye bado mdogo sana, anazo kesho nyingi sana ambazo zitahitaji umakini na trust ya hali ya juu wa wadau mbalimbali anaowafahamu na asiowafahamu.
Yeye alishaaminiwa na timu kubwa kama Yanga kuwa kipa namba moja. Angekuwa mimi ningecheza kwa nguvu bila hata senti moja ili timu zenye hela ndani na nje ya nchi zinione. Ona wachezaji wenye akili kama Asante Kwasi alicheza kwa moyo wake wote Mbao FC hadi timu zenye hela kama Simba zikamuona na kumsajili.
Ushauri mzuri lkn amechelewa....kwa Yanga asahau....Daima mbele Nyuma Mwiko....Mimi nataofautiana na wewe, Beno anadai pesa yake kyweli uongozi kwa sasa hauna fedha maana naambiwa ata wachezaji wanasajiliwa na baadhi ya wadau wa yanga. Kinachotakiwa uongozi na wadau watafute namna ya kusaidiana kupunguza madeni makubwa ya wachezaji ili wachezaji wahisi wanathaminiwa. Beno namshauri atafute namna ya kulishughulikia tatizolake uku akiwa anacheza kulinda kipaji chake na nyota inayo ng'aa kwa sasa, kwa kiwango alicho nacho sasa akiendelea kukaa langoni huwezi jua, anaweza akapata timu nje ya nchi.